Dr Mwakyembe hapaswi kuhurumiwa, amevuna alichokipanda

Kauli ya kuwa Mwakyembe amevuna alichopanda ...inahitaji tafakuri ..kuweza kumuelewa mleta hoja.........,kwa wale wanaojuwa sheria za kijasusi .."...wanajuwa there is always a price to pay when you agree to be used ...".....

Ukiangalia historia ya mwakyembe ..siku zote amejitambulisha ...kama mzalendo na hatuna shaka juu ya hilo...hata mtakumbuka alipokuwa mjumbe wa bodi ya NBC alipata kujitoa kupinga mambo yaliyokuwa yanafanyika kinyume.....

Kosa kubwa alilofanya Mwakyembe kwenye sakata la tume yake ...ni kukubali kutumika na kikwete kwa kujuwa au kutokujuwa.....,mkikumbuka kwenye ripoti yake aliyosema hili pia alilitaja.."baadhi ya mambo kwenye ripoti yangu sintayasoma yote " ......kimsingi aliichuja ripoti yake ili kuepuka kumu implicate rais na amiri jeshi mkuu..........hili kwa upande mwingine lilikuwa jambo jema kwa usalama wa nchi...lakini kitendo cha kwenda hewani kuwa kuna mambo ameyaficha ..kinaweza kuwa lilitafsiriwa na Jk na wenzake ...kuwa mbeleni mwakyembe angeweza kuwajeuka na kuwafanyia blackmail.........
Kitu cha kwanza rais kufanya kilikuwa kumuweka Mwakyembe karibu naye ili asije akamgeuka......[kumbukeni uhusiano wa mwakyembe na serikali kabla ya ile tume haukuwa mzuri sana.alikuwa mpinzani mkubwa]........

Tume ya mwakyembe ilimfanya akawa na maadui wa aina mbili ...
ADUI wa kwanza kundi la Lowassa..ambao wanaamini kuwa Mwakyembe tume yake ilitumika kumuuwa Lowassa kisiasa.....
ADUI Wa pili akawa ni Kikwete mwenyewe ambaye pamoja na kumchekea kote na kumuingiza mwakyembe na makamu wake engineer manyanya stella serikalini....hajapata kuamini kuwa mwakyembe angekaa na siri yote hii kwa muda gani....na ilikuwa lazima amfanyie monitoring..........lakini mnajuwa ..what deserve a hostile ....."agent"...!...

Sasa katika makundi mawilli adui wa mwakyembe ..moja adui wa wazi[lowassa]....mmoja adui wa kijino pembe"kikwete"....Tunabaki na swali la yupi aliyekuwa na access ya kumdhuru mwakyembe ..kupitia...taulo na sabuni ndani ya ofisi yake....................na kwa walio uona waraka wajiulize waliotumwa kufanya hivyo ni kina nani na wako wapi....?..kama kweli wapo

Tulikua tunarusha mawe ya kweli kama haya enzi hizo. Ila kwa sasa ukirusha uchambuzi kama huu basi utaanza kuambiwa we ni fisadi au umenunuliwa! Watoto wamejaa sana humu! Hawana hata uchungu na nchi na magazeti yanatumika kufikiria badala ya wao kutumia bongo zao kufikiri
 
Mwakyembe ni adui wa nafsi yake, na hicho ndicho kinamsunbuwa. Hato lala wala kuamka kwa raha na hato kufa upesi. Hayo ni mateso, hata mwili wake haumtaki, unapukutika kumkimbia. ni mtu mmoja ambae hana thamani hata kidogo kwa aliyoyafanya. Ile tume ilimfanya awe na kiburi sana kupita kiasi kiasi cha kusahau kuwa anazuwa na kusema uongo ilimradi mambo yake yafanikiwe, alifikiri anajitengenezea kumbe anajimaliza. Amejimaliza kwa kuwadhulumu Watanzania. Nani asiojuwa yote ili ilikuwa ni kutafuta fedha za haraka za kufanya kila hila ili mkataba wa kampuni yake usainiwe na uwe "funded" kwa fedha za "emergency"? Lakini bila kutegemea, akaangukia pua. His best wasn't good enough.
 
Nafikiri hii ndo moja ya hitimisho ya mwakyembe zanzibar, kama sijakosea, maana nimeona watu wamegusia vurugu za zanzibar.



240. Tume inaamini kwamba hakuna chanzo ambacho peke yake
ndiyo kilisababisha yote yaliyotokea. Kulikuwa na mlimbikizo
na mwingiliano wa sababu zilizotajwa katika ujumla wake na
ndiyo chanzo cha matukio haya.
Mapendekezo
241. Tume inapendekeza ifuatavyo ili kuepusha yaliyotokea:
a. Kuimarishwa kwa elimu ya uraia ambayo itasisitiza mambo
yafuatayo kati ya mengi.
• Kubadilika kifikra kuwafanya watu wafikirie utaifa zaidi
kuliko ubinafsi. Iwafanye wote kuelewa na kukubali kuwa
wa-Tanzania ni wamoja bila ya kujali eneo mtu atokako,
rangi au dini.
• Watu waachane na historia inayojenga chuki na uhasama.
• Watu, na hasa viongozi kuelewa kuwa uchaguzi ni njia ya
kujichagulia uongozi na kwamba maadamu wengi hushiriki,
wapo watakoshinda na wapo watakaoshindwa. Hivyo, katika
kudumisha demokrasia wanaposhindwa wakubali matokeo.
• Maadili ya kuendesha mfumo wa vyama vingi.
b. Kuimarisha uwazi, uadilifu na ufanisi katika kuandaa na
kuendesha uchaguzi ili kila mtu aone na kuelewa
kinachotendeka katika kila hatua kuepusha lawama na shutma.
c. Viongozi waheshimu utawala wa sheria
d. Wananchi wadai haki zao lakini pia watambue kuwa hakuna
haki isiyokuwa na wajibu.
 
Hapa anaonekana ana imani na serikali pamoja na polisi, lakini leo anawaandama polisi nafikiri ndiyo hoja ya mtoa hoja.



245. Baada ya kutafakari hali ya maandamano hayo, Serikali iliamini
kwamba maandamano yasingekuwa ya amani na usalama. Hivyo
ilitoa taarifa kwa njia ya radio na television kuwataka viongozi wa CUF
kuacha kutekeleza azma yao ya kufanya maandamano hayo kama
ifuatavyo:-
a. Inspekta Jenerali wa Polisi alitoa tamko hilo tarehe 23 Januari,
2001.
b. Waziri wa Mambo ya Ndani alitoa tamko la kukataza
maandamano tarehe 23 Januari, 2001.
c. Waziri Mkuu alitoa tamko kama hilo tarehe 25 Januari, 2001.
d. Makamu wa Rais naye alitoa tamko la kukataza maandamano
tarehe 25 Januari, 2001.
246. Tume iliarifiwa kuwa Jeshi la Polisi baada ya kupata taarifa kwamba
juhudi za kuwashawishi viongozi wa CUF kusitisha maandamano
kutofanikiwa, lilianza kuchukua hatua za kuhakikisha kwamba
maandamano hayo hayatafanyika. Kamishna wa Polisi Zanzibar alitoa
Amri ya Utendaji Na.2 ya 2001 iliyohusu operesheni ya kuzuia uhalifu
wa uripuaji mabomu na kufanya maandamano ya tarehe 27 Januari,
2001. Amri hiyo iliagiza, pamoja na mambo mengine, yafuatayo:
a. Kuweka ulinzi madhubuti katika maeneo yote muhimu,
 
265. Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Temeke (OCD) alitoa pingamizi. Hata
hivyo, Mbunge huyo aliendelea kuandaa mkutano huo.
266. Tume iliarifiwa kwamba tarehe 25 Januari, 2001, majira ya saa 7.30
mchana Polisi walipokea taarifa kwamba, wafuasi wa CUF wameanza
kukusanyika wakitokea vitongoji mbalimbali Wilayani humo wakiwa
wamevaa sare za CUF na kuelekea Mbagala katika uwanja wa
Zakheem.
 
Tathmini na maoni ya Tume kuhusu kilichotokea tarehe 26 na
27 Januari, 2001
354. Tume baada ya kufanya tathmini ya maelezo ya mashahidi kuhusu
kilichotokea imeridhika kuwa maandamano yalifanyika Wete, Chake
Chake na Micheweni kwa Pemba, Unguja Mjini na Dar es Salaam; na
amri ya Serikali kupiga marufuku maandamano hayo haikufuatwa.
Waandamanaji walijitokeza kwa wingi katika maeneo yaliyotajwa
mwanzo.
355. Tume pia imeridhika kwamba amri ya kutawanyika ilitolewa na Polisi
katika maeneo mengi lakini waandamanaji hawakuisikiliza. Tayari
walikuwa wameshahamasika kuaandamana na baadhi waliendelea na
azma yao hiyo hata baada ya wenzao kupigwa risasi na kufariki.
356. Polisi, katika jitihada ya kuyazima maandamano hayo walitumia
nguvu. Yapo maeneo, kama vile Wete na Micheweni ambapo makundi
ya waandamanaji yalikuwa makubwa sana na ya watu wenye hamasa.
Kwa vile baadhi ya wenzao wameshauawa na wengine kujeruhiwa, na
upande wa polisi nao jazba iko juu kwa kuwa mwenzao ameshachinjwa
na wengine kujeruhiwa na hivyo wanajihami na kutaka kuyadhibiti
maandamano basi ikawa ni mapambano. Katika mazingira hayo, Tume
imeridhika kuwa nguvu zilizotumika zilikuwa ni za lazima.
357. Tume imeridhika pia kwamba yapo maeneo mengine ambayo nguvu
ya ziada ilitumiwa na Polisi bila ya kuwepo sababu za msingi za
kufanya hivyo. Wapo wananchi waliopigwa risasi wakiwa majumbani
mwao baada ya maandamano na mmoja kufariki; wapo waliopigwa
wakati wanakimbia kusalimisha maisha yao na wapo wengi zaidi
waliopigwa na kuteswa wakati wakiwa katika ulinzi wa Polisi.
358. Kuhusu hoja iliyoletwa na Polisi kwamba wandamanaji waliazimia
kuteka vituo vya Polisi hasa vya Wete na Micheweni, Tume baada ya
kupokea ushahidi wote muhimu imeridhika kwamba hoja hiyo
haikujitokeza wala kufahamika kama ilikuwepo wala kujadiliwa na
vikao vya Polisi na Kamati za Ulinzi na Usalama kabla ya tarehe 27
Januari, 2001. Tume imeridhika kwamba dhana hiyo imekuja wakati
wa mapambano kama ilivyoelezwa katika aya 4.10 ya Taarifa hii.
 
61. Ipo haja ya kutoa elimu ya uraia kwa viongozi wa vyama vya siasa na
wananchi ili nao waelewe siyo haki zao tu bali pia wajibu wao kama
raia wa nchi hii.
362. Mwisho, Tume inashauri, kadri hali itakavyo ruhusu umuhimu wa
usalama wa vituo vya Polisi uzingatiwe bila ya kuathiri uwezo wa raia
kuingia kituoni bila taabu.
 
556. Kutokana na uhaba wa shughuli za uzalishaji mali kama vile viwanda
na nyingine za michezo na starehe, wananchi wengi wa Pemba
walijikuta wanatumia muda mwingi katika mambo ya siasa: ama
walikuwepo mikutanoni au walibaki vikaoni wakicheza bao, karata na
wakizungumzia masuala ya kisiasa. Hakukuwa na mazungumzo ya
kuinua na kuendeleza uchumi - bali lawama za kukosa maendeleo.
 
mwakyembe ni adui wa nafsi yake, na hicho ndicho kinamsunbuwa. Hato lala wala kuamka kwa raha na hato kufa upesi. Hayo ni mateso, hata mwili wake haumtaki, unapukutika kumkimbia. Ni mtu mmoja ambae hana thamani hata kidogo kwa aliyoyafanya. Ile tume ilimfanya awe na kiburi sana kupita kiasi kiasi cha kusahau kuwa anazuwa na kusema uongo ilimradi mambo yake yafanikiwe, alifikiri anajitengenezea kumbe anajimaliza. Amejimaliza kwa kuwadhulumu watanzania. Nani asiojuwa yote ili ilikuwa ni kutafuta fedha za haraka za kufanya kila hila ili mkataba wa kampuni yake usainiwe na uwe "funded" kwa fedha za "emergency"? Lakini bila kutegemea, akaangukia pua. His best wasn't good enough.

kumbe mwakyembe alikuwa na lake jambo!
 
Mbona unasema kwa wasiwasi weka mambo wazi ili tukuelewe mana ukifichaficha itakuwa ni majungu
 
Domokaya (Mleta hoja) ni Mzushi. Aina hii ya uandishi ni ya kizushi. Anaonyesha ana upeo mdogo sana wa kuelewa mambo. Wakati ule Mwakyembe alitofautiana na wengi hasa waandishi kuhusu Posho za wabunge. Jambo ambalo sio la muhimu kama mleta udaku anavyotaka ieleweke. Inaonyesha huyu ni mwandishi wa Ijumaa wikienda.
Si jambo jema kusubiri mtu apate matatizo ndio uanze kutafuta mabaya yake.

Hapana si mzushi Domokaya ni miongoni mwa waliohusika kumwekea sumu Dr. Mwakyembe. Wajua JF ina subscribers wengi sana sasa hivi na jamaa zetu wa usalama wanaitumia sana kukoroga vichwa vyetu. Wanajua hapa ndo maoni yanapotoka na mtandao wao ni mpana wale msiosoma kati ya mistari mwaweza kuchanganyikiwa. Huyu jamaa yuko kwenye kundi la waliodhamiria kumuua Dr. Mwakyembe na nia yake ni kujenga hoja kwa watu ili wamchukie. Nimesikitika watu tumechangia sana thread hii isiyo na nia njema najua ni kwa sababu ya mapenzi yetu kwa huyu mpambambanaji. Nadhani inatosha. Tumwache a-conclude au kama alikuwa anapima afanye analysis kujua maoni ya watu yakoje. Mfumo wa ufisadi umejichimbia sana tuwe na tahadhari na watu kama kina Domokaya.
 
Hivi Dr Mwakyembe alisomea elimu ya FORM FIVE na SIX secondary (high school) ipi?.

Nakumbuka miaka ile ONLY vichwa walikua wanaenda form five maana shule zilikua chache. Layer ya pili ilikua inaelekea chuoni kwenye certificates ili kuongeza nguvu kazi kama ilivyo VETA sasa hivi.

Au nimetoka nje ya mada? LOL
 
Dr Mwakyembe wakati anasulubu na kutafuta mabaya ya Richmond-Dowans baadaye haku declare conflict of interest, kua anachunguza kampuni ambayo ipo in the same line oof business (and potential competitor) na idea yake au kampuni yake ya kufua umeme kwa upepo huko Singida.

Pili alipogundua kua sio EL anahusika DIRECTLY na Richmond hakutaka kusema ukweli au kurudi nyuma. Akaamua kusaidia usalama wa nchi (nampongeza somehow) na kutupunguzia gharama za uchaguzi (hongera pia). Ila msaada wake wa nchi ukaja kwa gharama ya kumvunkia heshima EL na wenzake.

Dr alijua kabisa kua kwa kutowaeleza ukweli wananchi anawakosea ila akachagua kujiunga na mafisadi halisi na kuwabambikia wengine ufisadi feki.

Malipo ni hapa hapa duniani.
 
Narudi nyuma miaka kadhaa wakati DR Mwakyembe alipoona siasa inalipa kuliko taaluma alipoamua kukimbia chaki Chuo Kikuu cha Dar es laam na kwenda kugombea ubunge wa Afrika Mashariki. Mwakyembe kwa kutaka kupendwa na chama chake aliyatamka maneno ambayo yalikuwa dhihaka kwa wananchi wa nchi hii, maneno ambayo, yaliidhalilisha taaluma yake, maneno yaliyodhalilisha wasomi na maneno yaliyodhalilisha jumuiya ya chuo kikuu cha Dar es salaam. Aliyasema hayo kwani alijua chama chake kinapenda kuyasikia, na alisema akijua akiyasema hayo atapata nafasi moja ya kuwa mbunge kilaini.

Nakumbuka yote, nakumbuka kila kitu. Nakumbuka hasira za wenye tafakuri nziti zilivyomrukia na kumsuta, alionekana dhahiri anajitongozesha kwa gharama ya wananchi kuumia ili yeye aneemeke. Nakumbuka jinsi alivyomuudhi Jenerali Ulimwengu hata wakaanza kujibizana kwa kalamu na maneno ya vinywani.

Nakumbuka, sijasahau ni Dr Mwakyembe huyu huyu chaguo kipenzi cha CCM. Alishirikiana nao kuwagandamiza wananchi, akataka kwenda mbali kushiriki zaidi kuwagandamiza ili aendelee kufaidi na kuneemeka yeye na familia yake. Alipowekewa kigingi akijifanya yeye na wanafiki wenzake eti wanatetea wananchi. Kumbe wapi wamekutana na kichaka cha simba sasa wanataka sapoti ya kukishinda, wote wao na kile kichaka lengo lao ni kutufanya kitoweo.


Dr Mwekyembe ni mmoja wa watengenezaji mifumo hiyo michafu na ya kinyama ambayo leo imemrudi yeye mwenyewe. Wanajua na wanajuana namna ya kuzitengeneza hizo sumu na kuwalisha sijui kuwagusisha watu. Wameshawau wengine wengi tu leo imefika zamu yao wanapiga kelele.

Wenye kumbukumbu nzuri watakubaliana nami kuwa Mwenyekiti wa CCM alilizungumzi hili katika sherehe za kuzaliwa chama mwaka juzi. Alisema wazi watu ndani ya chama wamehasimiana kiasi cha kushindwa kuachiana glasi mezani.

Hivyo ndivyo siasa za CCM zilivyo na kila mwenye upeo kidogo tu anafahamu hilo achilia mbali DR wa sheria. Ukiwa nao fanya kama wanavyofanya wao na malengo ya chama chao. Uongo, uzandiki, wizi, uzabizabina, kujipendekeza, ulafi, majivuno, dharau na uchafu mwingine mwingi waufanyao. Ukikiuka haya umekiuka miiko, umekuwa msaliti lazima uadhibiwe.

Kuna waliosema chama kimekosa dira na mwelekeo wakakiona cha moto. Kuna alioaga kwenda London eti akirudi awaambie watanzania ukweli kuhusu nchi yao ilivyotafunwa na kubaki makapi, lakini thubutu yake hakurudi. Mifano ni mingi hata ile ya waliotaka kusema ukweli kuhusu jambo fulani wote wamepotea, kuanzia Stan Katabalo mpaka ile tume ya unga wa ngano wa sumu, tume nzima ilipotea. Walipita kulalamika kuwa wanataka kuuliwa hakuna aliyewasikiliza, wakaishia. Yote haya Mwakyemba anayafahamu na bado akaenda kujiunga na kusaidia kutekeleza haya, sasa leo zamu yake anang'aka. Anang'aka nini mwache aone shida wanazopata watanzania wengine ambayo kwa sababu ya yeye na wenzake kujenga mfumo wa kidhalimu kuna watanzania wanakufa kwa kukosa barabara za kuwafikisha mahosipitalini, aone jinsi watanzania wanavyojilundika hospitalini wakisubiri vifo vyao huku wakipozwa na panadol, bora yeye amepelekwa Appolo.

Hili liwe fundisho kwa watu wote wenye kutumia migongo yetu wanyonge kujipatia nafasi ya kujilimbikizia mali na madaraka. Kuna siku madaraka na mali havitatosha sasa wataanza kunyang'anyana walivyopeana kwani kila mtu atataka kumzidi mwenzie. Mbinu zingine zinaposhindikana na msaliti anapoelekea kutoa siri ndipo watarudi kwenye ile mbinu yao ya "Costra Nostra" maiti haisemi.

Dr Mwakyembe na wenzake wasilie kama zamu yao imefika basi wajue kuwa hata wenzao waliowatanguliza walipitia machungu hayo hayo, zaidi wajue kuwa maisha ya watanzania waliootaabika na kufa kwa ajili ya udhalimu wao ni dhaidi ya wao kunyweshwa sumu. Wanavuna walichopanda
Wewe nadhani upo kwenye kundi walilo mnywesha sumu Mwakyembe.
 
Mleta thread hana lolote nae ni muuaji tu anafurahia walichofanya kwa Dr. Mwakyembe lakini wajue hakuna marefu yasiyo na ncha!
 
Back
Top Bottom