Dkt. Mwaka ajitafakari. Upendo ukiisha ni busara kukubali kuachia na maisha yaendelee

xox

JF-Expert Member
Sep 23, 2018
1,396
6,499

Kuna kipindi sisi wanaume huwa tunajipalilia maanguko yetu sisi wenyewe. Haijalishi umempenda mtu kiasi gani, ikifikia wakati upendo ukaisha ni busara kukubali kuachia na maisha yaendelee.

Kupitia hili sakata la Mwaka na mke wake, Mwaka anaweza akahisi ameshinda, ila daima mwanamke sio wa kumfanya adui yako, hasa mwanamke ambae anajua undani wako.

Bila kujua Mwaka anapigwa laana na machozi ya mkewe, watoto wake na hata watu wengine wanaouguswa na haya mambo.

Sio kwa kuwa biased, ila Mwaka ana kila traits za Sadisit (mtu anaepata faraja katika maumivu ya wengine) na hili halitamalizika vyema kwake.
 
View attachment 2510019

, ila daima mwanamke sio wa kumfanya adui yako, hasa mwanamke ambae anajua undani wako.

Bila kujua Mwaka anapigwa laana na machozi ya mkewe, watoto wake na hata watu wengine wanaouguswa na haya mambo.
Sio mwanamke tu, hata mwanaume hafai kufanya adui yako.

Yani nyie mguswe na situation ya familia yake, then mumpatie laana? Hakuna kitu kama hicho.

Halafu mkuu, ugomvi unaohusu mahusiano ya kimapenzi sio wa kuuingilia kichwa kichwa. Achana na haya wanayosema hadharani, kunakuwaga na mengi sana behind the scene. Watu ambao walikuwa wanalala uchi pamoja, kwa muda mrefu, leo wanageuka maadui, halafu wewe mtu Baki unakuja na simple explanation.? Acha kuweka conclusion kwenye kitu ambacho hujui mwanzo ni upi.
 
Sio mwanamke tu, hata mwanaume hafai kufanya adui yako.

Yani nyie mguswe na situation ya familia yake, then mumpatie laana? Hakuna kitu kama hicho.

Halafu mkuu, ugomvi unaohusu mahusiano ya kimapenzi sio wa kuuingilia kichwa kichwa. Achana na haya wanayosema hadharani, kunakuwaga na mengi sana behind the scene. Watu ambao walikuwa wanalala uchi pamoja, kwa muda mrefu, leo wanageuka maadui, halafu wewe mtu Baki unakuja na simple explanation.? Acha kuweka conclusion kwenye kitu ambacho hujui mwanzo ni upi.
Una akili mkuu.
Machozi ya mwanamke ni ngao tu kujihami lkn hatujui undani wa jambo
 
Halafu acheni huu ujinga wenu wa matatizo yenu ya ndoa kuihusisha mama samia na serikali yake. Serikali inahusu nini katika maisha yenu ya ndoa? Serikalini ina mambo mengi ya kufanya hali ya maisha ipo juu then ianze kujadili mlivyokuwa mnapigana miti!? Nendeni bakwata uko
 
Kila jambo lina pande 2. Machozi ya mwanamke si ya kuamini sana.
Kuna vitu vitatu muhimu sana kwenye hili sakata
1. Mwanamke ndio anataka talaka
2. Hataki kudhalilishana kwenye mitandao ya kijamii( hili nimempa big up sana)
3. Hataki kugombea mali anataka amani ya moyo aachwe alee wanae!
Kwa hizo point tatu unaweza kuona wazi tatizo liko upande gani
 
Mkishafika hapa haijalishi nani mkosaji the only solution ni talaka tu,

Mwaka ampe mkewe talaka mana hapa ameshasema hata hizo mali hataki tena anataka tu amani ya moyo na watoto wake!

Mimi nashangaa sana watu wanaosema huenda huyo mwanamke anajiliza tu, awe anasema ukweli au uongo the fact that ameomba apewe tu talaka na mali ataziacha zote that speaks volume about Dr. Mwaka!

Mwaka amwache huyo mama aende jamani, au mpaka tusikie mtu amecommit suicide?
Amani ya moyo ni kila kitu humu duniani!
 
Kuna vitu vitatu muhimu sana kwenye hili sakata
1. Mwanamke ndio anataka talaka
2. Hataki kudhalilishana kwenye mitandao ya kijamii( hili nimempa big up sana)
3. Hataki kugombea mali anataka amani ya moyo aachwe alee wanae!
Kwa hizo point tatu unaweza kuona wazi tatizo liko upande gani
Mbona inajulikana huyu bi mkubwa amepata bwana wa kumuoa ndio maana anaforce talaka unajua sababu iliyomfanya yule shekh mkuu kutenguliwa wadhifa wake?

Anajifanya hataki mali anataka amani ya moyo wake na talaka...ila akishapewa talaka ataanza kusumbua kutaka mali
 
Wanaume wa siku hizi hawaachiko kirahisi mpk zifanywe drama nyingi😂😂😂 kinachomuums dr makanjanja ni kutoa talaka akijua kuna mtu atachukua zigo😂😂

Hapa piga ua talaka yangu utatoa, atoe talaka wanaume wachukue zigo😂
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom