Darren2019
JF-Expert Member
- Nov 23, 2019
- 1,112
- 2,379
Ni kweli kabisa YONO,MAJEMBE,kwa dhati kabisa warudi mashambani sasa,wajiunge nasi katika kilimo cha kisasa.
Kwahiyo mnada utafanyika kupitia tovuti ya TRA au vipi na kutakuwa na uwazi kiasi gani kuwa walioweza kutoa dau kubwa ndio wameshinda
TRA yasitisha minada ya hadhara, sasa kufanyika kielektroniki
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk. Edwin Mhede amesitisha kuuza bidhaa balimbali kwenye minada ya hadhara ambayo awali ilikua ikitumia madalali.
Amesema minada hiyo kwa sasa itakuwa kwa njia ya mtandao na kulipiwa kwa njia hiyo licha ya kwamba mteja ataruhusiwa kuona bidhaa alizochagua kwa njia ya mtandao.
Amesema hayo leo jijini Dar es Salaam na kuongeza kuwa utaratibu uliokuwa ukitumika awali wa minada ya forodha kwa bidhaa mbalimbali ulikuwa ukifanywa kupitia dalali aliyepewa kandarasi na TRA kufanya minada hiyo.
“Wakati tulikuwa tukitumia madalali kumejitokeza changamoto mbalimbali ikiwamo kufanyika mara moja kwa wiki na kusababisha bidhaa hizo kutouzwa kwa wakati hivyo serikali kutokomboa kodi kwa wakati pia.
“Pia washiriki wa mnada wamekuwa ni wale wale kwa kujirudia rudia na hata hivyo wengi wao kutokuwa wanunuzi na mara kadhaa kuingilia minada na kuharibu na kufanya wanunuzi wenye nia kushindwa kununua bidhaa hizo,” amesema.
Aidha, amesema kumekuwa na vitendo vya kuzuia wengine na kupanga bei ambayo ni kinyume na busara ya msingi ya uchumi kunakofanywa na baadhi ya watu wenye hila kwa mtandao waliouweka.
Pamoja na mambo mengine, amesema pia tuhuma mbalimbali na vitendo vya rushwa vikihusisha hata baadhi ya Maofisa wa TRA.
Chanzo: Mtanzania
Yule mama mkurugenzi wa yono auction, atakula wapi tena.du .dar kumekucha.madalali wakalime Sasa.TRA yasitisha minada ya hadhara, sasa kufanyika kielektroniki
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk. Edwin Mhede amesitisha kuuza bidhaa balimbali kwenye minada ya hadhara ambayo awali ilikua ikitumia madalali.
Amesema minada hiyo kwa sasa itakuwa kwa njia ya mtandao na kulipiwa kwa njia hiyo licha ya kwamba mteja ataruhusiwa kuona bidhaa alizochagua kwa njia ya mtandao.
Amesema hayo leo jijini Dar es Salaam na kuongeza kuwa utaratibu uliokuwa ukitumika awali wa minada ya forodha kwa bidhaa mbalimbali ulikuwa ukifanywa kupitia dalali aliyepewa kandarasi na TRA kufanya minada hiyo.
“Wakati tulikuwa tukitumia madalali kumejitokeza changamoto mbalimbali ikiwamo kufanyika mara moja kwa wiki na kusababisha bidhaa hizo kutouzwa kwa wakati hivyo serikali kutokomboa kodi kwa wakati pia.
“Pia washiriki wa mnada wamekuwa ni wale wale kwa kujirudia rudia na hata hivyo wengi wao kutokuwa wanunuzi na mara kadhaa kuingilia minada na kuharibu na kufanya wanunuzi wenye nia kushindwa kununua bidhaa hizo,” amesema.
Aidha, amesema kumekuwa na vitendo vya kuzuia wengine na kupanga bei ambayo ni kinyume na busara ya msingi ya uchumi kunakofanywa na baadhi ya watu wenye hila kwa mtandao waliouweka.
Pamoja na mambo mengine, amesema pia tuhuma mbalimbali na vitendo vya rushwa vikihusisha hata baadhi ya Maofisa wa TRA.
Chanzo: Mtanzania
Madalali, Kumekucha Sasa Mambo Mengi Sana Muda Mchache. TRA Wamekwenda Kugonga Kisu Cha Mfupa
Yule Mama Yono Na Nywele Zake Kisogoni 😄😅
Hata Kwa Kulumangia Ugali
Mkuu mambo yote yanaishia kwenye ka TECNOJe mitandao yetu ya Internet itaweza kweli ama ni siasa,Unajikuta unaenda tra,tpa ama ofisi nyingine ya serikali wakati wa malipo utasikia jamani msubiri network haipo vizuri,Sasa tpa imejidhatiti vipi na hilo swala
Leseni ya biashara hutolewa halmashauri husikaUpande wa leseni zinatolewa na BRELA ni kwa kielectronic