Dkt. Mathayo na Ana Kilango: Same "Wachina" wa Tanzania mpaka "VILAZA" wa Kilimanjaro

Mimi ninachoona hapa ni ushabiki mkubwa unaofanywa na FMES bila kujibu tuhuma halisi zilizotolewa na Bangusule. Bangusule ametoa tuhuma kadhaa kubwa. Moja ni kuhusu wilaya ya Same kufanya vibaya kielimu, pili ni suala la ugonjwa uliokumba zao la mpunga, tatu ni ubovu wa barabara, na nne ni ufyekaji wa misitu ambao umesababisha kuharibiwa kwa vyanzo vya maji. FMES anakuja na hoja kwamba mbunge Anne Kilango amechimba visima 30 na kutoa msaada wa baisikeli 20 kwa walemavu. Huu ni upotoshaji mkubwa wa mada na hakuna jibu liliotolewa kuhusu tuhuma alizotoa Bangusule.

Mkuu FMES, tuambie katika tuhuma nne alizotoa Bangusule, mbunge wako Anne Kilango amefanya nini katika kuzitatua? Visima vya maji siamini kama vinatumika kumwagilia mpunga. That is insane! Taumbie visima vyako 30 vinahusiana vipi na ugonjwa uliokumba zao la mpunga. Tuambie visima vinahusiana vipi na wanafunzi kufanya vibaya katika mitihani yao. Tuambie visima vinahusiana vipi na ufyekwaji wa misitu na uharibifu wa vyanzo vya maji.
 
hali ya maendeleo katika wilaya ya Same imedorora tangu Dr.Mathayo na Anna Kilango wachaguliwe kuwa wabunge wa same magharibi na same mashariki. hali ya ELIMU ni mbaya sana. wilaya ya same imeshika mkia katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba na ule wa kidato cha nne. katika suala la KILIMO ule mradi maarufu wa kilimo cha umwagiliaji Ndungu una hali mbaya sana. kuna maradhi ya mpunga yameingia na wakulima hawana msaada wowote toka kwa mbunge wao Anna Kilango. milimani upande wa Dr.Mathayo ukataji MITI na uharibifu wa MISITU ambayo ni vyanzo vya maji umezidi kuongeza. BARABARA ya mkomazi-bendera-ndungu-gonja-kisiwani-same bado ni kero kubwa kwa wananchi.

Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kuisifu wilaya yetu na kutuita "Wachina" wa Tanzania. nina hakika akifufuka leo na kushuhudia uongozi mbovu wa Dr.Mathayo na Anna Kilango, akaona na matokeo ya mitihani ya watoto wetu atageuza kauli yake na kutuita "VILAZA" WA KILIMANJARO.


Mtanzania

.....umeeleza vizuri sana ni kw anji agani kiongozi anahitajika kwa jamii.....na anategemewa vipi.......

........bangusule kaleta concern....which is ok as a concern citizen....na concern yake.............does apply sehemu nyingi tu nchini.........

.....now.......check hiyo highlight ya kwanza in red...........tell me how do one arrive to such a conclusion.......!!!

....sidhani kama itakuwa ni kumtendea haki Mh Mbunge kumsema Mbunge eti kuna maradhi ya mpunga na yeye hakuwa na msaada wowote kwa wakulima.........how do one substantiate this claim...........kwa ambao tumekulia kule kajunjumele....tunatakiwa tulielewe hili jambo better than anybody........nafikiri unanisoma............

........Mtu unaweza kuwa na hoja nzuri sana........lakini ukishindwa namna ya kui-present.............mtu anaweza kuku-ignore.....ukashangaa........

......bangusule ana valid concerns......lakini zinaelea......na ndio maana akina Ogah.....wame-comment walivyo -comment..........

.......bangusule should now tell us amelifanyia nini au ana mpango wa kulifanyia nini jimbo lake.........

Kuna mtu hapa kazungumzia suala la wabunge kuwa na ToRs na Performance indicators........wow it might be good idea to start with.....however, we should be able to see and say Mh Mbunge did 1, 2, 3..........to the satisfaction of who......this is debatable.......
 
Bangusule hakusema hawa wabunge ni vilaza. Alichosema ni kuwa Mwalimu akifufuka atawaita watu wa Same ( yeye mwenyewe akiwemo) kuwa vilaza wa Kilimanjaro. Kuuita uongozi wa wabunge waliopo mbovu ni haki yake kama mpiga kura. Mimi sioni alipotukana.

Re: Dr.Mathayo na Ana Kilango: Same "Wachina" wa Tanzania mpaka "VILAZA" wa Kilimanja
Mimi ninachoona hapa ni ushabiki mkubwa unaofanywa na FMES bila kujibu tuhuma halisi zilizotolewa na Bangusule. Bangusule ametoa tuhuma kadhaa kubwa. Moja ni kuhusu wilaya ya Same kufanya vibaya kielimu, pili ni suala la ugonjwa uliokumba zao la mpunga, tatu ni ubovu wa barabara, na nne ni ufyekaji wa misitu ambao umesababisha kuharibiwa kwa vyanzo vya maji. FMES anakuja na hoja kwamba mbunge Anne Kilango amechimba visima 30 na kutoa msaada wa baisikeli 20 kwa walemavu. Huu ni upotoshaji mkubwa wa mada na hakuna jibu liliotolewa kuhusu tuhuma alizotoa Bangusule.

Mkuu FMES, tuambie katika tuhuma nne alizotoa Bangusule, mbunge wako Anne Kilango amefanya nini katika kuzitatua? Visima vya maji siamini kama vinatumika kumwagilia mpunga. That is insane! Taumbie visima vyako 30 vinahusiana vipi na ugonjwa uliokumba zao la mpunga. Tuambie visima vinahusiana vipi na wanafunzi kufanya vibaya katika mitihani yao. Tuambie visima vinahusiana vipi na ufyekwaji wa misitu na uharibifu wa vyanzo vya maji.

- Unajua hata mwenye makengeza hawezi kumbiwa ona hapa, wewe huwezi kuiuliza hoja au kutoa ushauri kwa kiongozi uliyekwisha muita kilaza, that is insane kama sio insanity, halafu ukategemea kujibiwa kwa heshima na hoja, ndio hasa upunguani, ukitaka hoja utajibiwa kwa hoja, lakini ukishaita kiongozi ni kilaza basi wewe ndiye kilaza wa kwanza na hutakiwi kujibiwa kwa ustaaarabu zaidi ya kuambiwa wazi kwamba wewe ni kilaza sasa mebngine yote yanakuwa ni pure nonesense hata kama unasaidiwa na wengi walio na mawazo kama yako yaani yanayoona kuitwa kwa Mbunge aliyechaguliwa na wananchi wa Same East, kwamba ni kilaza kwa sababu unazozijua wewe ambaye hukumchagua na wala huwezi fanya anything kuhusu ubunge wake.

- Kwenye topic moja hapa JF, hivi hivi mliwaita wandishi wa habari vilaza nilipowajibu on vilaza line, forums nzima ikaja juu kwamba kilaza ni matusi na yasiruhusiwe hapa JF na topic ikafungwa, sasa leo mmegeuka wale wale kwamba eti kumuita kiongozi kilaza wakati kilaza ni wewe mwenyewe kwa sababu huna sababu za msingi zaidi tu ya kutaka kujionyesha huku ukiungwa mkono na mnaofanana kwa akili, kama unataka kujadili hoja kwa ustaarabu basi next time ondoa matusi ambayo naona hata Mods wameyakubali, hapana wakuu hatuwezi kubadili the rules of the game kwa sababu tu ya kumtukana Mama Kilango, amelifanyia mema mengi sana taifa letu, kama kuna ambao hamuwezi kuonyesha shukrani kwake, kuna ambao tunaouthamini sana mchango wake kwa taifa hili ana atakumbukwa sana na vizazi vivyajo kwa kuweza kusimama na kuhesabiwa.
 
1. Mimi ninachoona hapa ni ushabiki mkubwa unaofanywa na FMES bila kujibu tuhuma halisi zilizotolewa na Bangusule.

2. Bangusule ametoa tuhuma kadhaa kubwa. Moja ni kuhusu wilaya ya Same kufanya vibaya kielimu, pili ni suala la ugonjwa uliokumba zao la mpunga,

3. tatu ni ubovu wa barabara, na nne ni ufyekaji wa misitu ambao umesababisha kuharibiwa kwa vyanzo vya maji.

4. FMES anakuja na hoja kwamba mbunge Anne Kilango amechimba visima 30 na kutoa msaada wa baisikeli 20 kwa walemavu.

5. Huu ni upotoshaji mkubwa wa mada na hakuna jibu liliotolewa kuhusu tuhuma alizotoa Bangusule.

6. Mkuu FMES, tuambie katika tuhuma nne alizotoa Bangusule, mbunge wako Anne Kilango amefanya nini katika kuzitatua? Visima vya maji siamini kama vinatumika kumwagilia mpunga. That is insane!

7. Taumbie visima vyako 30 vinahusiana vipi na ugonjwa uliokumba zao la mpunga.

8. Tuambie visima vinahusiana vipi na wanafunzi kufanya vibaya katika mitihani yao. Tuambie visima vinahusiana vipi na ufyekwaji wa misitu na uharibifu wa vyanzo vya maji.

1. hali ya maendeleo katika wilaya ya Same imedorora tangu Dr.Mathayo na Anna Kilango wachaguliwe kuwa wabunge wa same magharibi na same mashariki.

2. hali ya ELIMU ni mbaya sana. wilaya ya same imeshika mkia katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba na ule wa kidato cha nne.

3. katika suala la KILIMO ule mradi maarufu wa kilimo cha umwagiliaji Ndungu una hali mbaya sana. kuna maradhi ya mpunga yameingia na wakulima hawana msaada wowote toka kwa mbunge wao Anna Kilango.

4. milimani upande wa Dr.Mathayo ukataji MITI na uharibifu wa MISITU ambayo ni vyanzo vya maji umezidi kuongeza. BARABARA ya mkomazi-bendera-ndungu-gonja-kisiwani-same bado ni kero kubwa kwa wananchi.

5. Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kuisifu wilaya yetu na kutuita "Wachina" wa Tanzania.

6. nina hakika akifufuka leo na kushuhudia uongozi mbovu wa Dr.Mathayo na Anna Kilango, akaona na matokeo ya mitihani ya watoto wetu atageuza kauli yake na kutuita "VILAZA" WA KILIMANJARO.

- Tatizo lako mkuu wangu ni kwamba unamalizwa sana na chuki za binafsi bila hata hoja ya msingi, sasa tizama hizi quote zako hapo juu kama zinafanana, ndio maana ninasema hivi wewe ndiye kilaza namba moja hapa kwa sababu huna hata clue ya unachokisema, one minute uansem one thing, halafu next minute unasmea another, make up your mind unataka nini hasa, maana hatuwezi kukusaidia kama wewe mwenyewe unajichanganya kama hapo juu.

Thanxs!
 
Quote; Zero

Kitu kimoja ambacho nimejifunza hapa JF ni kwamba kuna makundi mawili makuu ya waandishi. Kuna wachangiaji wa mada (positively) na washabiki wa mada. Kundi la kwanza, yaani wachangiaji wa mada wanaelewa umuhimu wa kuelimishana na wanaamini kabisa maoni na mchango wao unaleta impact fulani katika jamii. Kundi la pili, yaani kundi la washabiki, wanaamini kabisa kwamba hiki ni kijiwe cha wahuni tu waliokosa kazi na wanakuja kupoteza muda wao. Kundi hili linaweza kuamua kumshabulia mtoa mada negatively tu, hata kama wao wenyewe hawana ushahidi wa kutosha.

Nimesema haya baada ya kupitia posts zote zilizochangia hii thread. Kuna waliomponda Bangusule bila wao kutoa ushahidi wowote. Kuna waliomponda na kutoa ushahidi wao (kama alivyofanya FMES). Na kuna wale pia walioshabikia tu positively bila kuwa na vigezo. Labda ningependa kusema tu kwamba, kama huna ushahidi na yale unayotaka kuchangia, ni bora tu ukatoa maoni ambayo hayataathiri mtiririko wa mada. Bangusule katoa ushahidi wa matokeo ya kidato cha nne kama kielelezo kwamba wilaya ya Same inafanya vibaya katika masomo. Hili bado mnalipinga? Website ya matokeo ipo na mnaweza kwenda kuangalia. FMES katoa hoja kuhusu uchimbwaji wa visima. Hili hatuna ushahidi nalo, lakini FMES anaweza kuweka ushahidi wake.

1. Mimi ninachoona hapa ni ushabiki mkubwa unaofanywa na FMES bila kujibu tuhuma halisi zilizotolewa na Bangusule.

2. Bangusule ametoa tuhuma kadhaa kubwa. Moja ni kuhusu wilaya ya Same kufanya vibaya kielimu, pili ni suala la ugonjwa uliokumba zao la mpunga,

3. tatu ni ubovu wa barabara, na nne ni ufyekaji wa misitu ambao umesababisha kuharibiwa kwa vyanzo vya maji.

4. FMES anakuja na hoja kwamba mbunge Anne Kilango amechimba visima 30 na kutoa msaada wa baisikeli 20 kwa walemavu.

5. Huu ni upotoshaji mkubwa wa mada na hakuna jibu liliotolewa kuhusu tuhuma alizotoa Bangusule.

6. Mkuu FMES, tuambie katika tuhuma nne alizotoa Bangusule, mbunge wako Anne Kilango amefanya nini katika kuzitatua? Visima vya maji siamini kama vinatumika kumwagilia mpunga. That is insane!

7. Taumbie visima vyako 30 vinahusiana vipi na ugonjwa uliokumba zao la mpunga.

8. Tuambie visima vinahusiana vipi na wanafunzi kufanya vibaya katika mitihani yao. Tuambie visima vinahusiana vipi na ufyekwaji wa misitu na uharibifu wa vyanzo vya maji.

- Again tizama maneno yako mwenyewe, kule juu umesema nimetoa ushahid lakini chini kwa sababu nimekubana sana mbavu umebadilika na kujaribu kula mamneno yako mwenyewe, that is you na kujaribu kubadili hoja yangu kuhusu baiskeli yes kwangu ni big deal tena sana inagwa kwako sio kwamba wananchi walioshindwa kutoka nje almost all their life leo wamepatiwa chombo cha kuwawezesha kutoka nje na kushiriki kwenye maendeleo ya jimbo lao, kwako ni nothing na insane, labda kwa wasiokujua maana tunaokujua vizuri hizi ndio tabia zako za ajabu ajabu na kuropoka maneno bila kufikiri, kama vile wkenye ishu ya Dr. Masau, ukaropoka ropoka mpaka ulipokamamtwa.

- Eti unasema visima vya maji 30 vipya wka jimbo huko vijijini sio big deal na kuna watu wenye ehshima zao wanakuunga mkono maneno ya dhartau wka wananchi namna hiyo, je wewe uliwahi kutoa visima vingapi katika masiha yako mkuu kwa kijiji chochote kile cha Tanzania, licha ya Same East ambalo wala sio jimbo lako? Eti kabla ya hivi visima kuwekwa m,aji yalikuwa yanapatikana wapi? Au ni wewe ndiye uliyekua unawapa? Mkuu ukipata nafsi nenda Same East ukaone maendeleo, huyu Mama ni mpaka atakapoacha mwenyewe, hapewi ubunge na wewe huku JF, hapana anachaguliwa na wananchi, na wananchi wa Same East sio wajinga au vilaza kama wewe, shughuli za maendeleo na sifa za mbunge wao kwa kazi za jimbo na taifa zinafahamika sana mkuu, ngoja tuendelee kukuwekea ushahidi hapa chini.

Thanxs!
 
Kama wamefeli mwambie mkuu wa wilaya akawachape bakora hao walimu
 
Mkuu wangu naomba tuanze mwanzo, ona chini jinsi mbunge alivyoingia ubunge wa Same East, maana ni lazima tuanzie alikoanzia na hili jimbo alimtwanga mbunge fisadi.


By Guardian and PST Reporters, IPP Media
Fri, Aug 05, 2005


A number of senior cabinet ministers in the outgoing President Benjamin Mkapa’s government and party stalwarts face the prospect early exit as Chama Cha Mapinduzi’s preferential polling entered its final stages yesterday.

Some of the early results showed that Minister for Energy and Minerals Daniel Yona was one of the early casualties having been trounced resoundingly by nominated MP and wife of CCM national vice-chairman, Anne Kilango-Malecela, who polled 286 votes against Yona’s 60.
 
Jamaa anaona Same tu ndio wamefeli aulize Lindi,Mtwara mbona wanafeli miaka yote na hakuna anayeshtuka
 
Baada tu ya kupata ubunge wa Same East, Mbunge mpya alikwenda Malasyia na Indonesia, ambako akishirkiana na wabunge wengine wa huko Kilimanajro aliweza kuwaleta hawa wakulu ambao wamufanyia mengi sana kielimu mkoa mzima na hasa jimbo la Same East, soma chini hapa;-


Primary School Renovation and Support

All primary schools in this part of rural Tanzania were built by the local community with little or no money available for the completion of the buildings or for any maintenance. Consequently primary schools frequently have breeze block walls with holes left for the windows and doors, an earth floor and a corrugated iron roof.

Renovation work typically includes:

laying concrete floors
replacing and repairing corrugated iron roofs
putting in ceilings, windows and doors
repairing cracks, plastering and whitewashing walls
making tables, benches and blackboards
The result is that the schools become bright, comfortable places where learning is stimulated. There are medical benefits too, as jiggas - little fleas that live in earth floors - are no longer able to enter the children's skin and debilitate them.

The charity has now renovated the following primary schools: Mauo, Mshiri, Ashira, Samanga, Palangeny, Lyasomboro, Mbahe, Matala, Kochakindo and Kilaremo. Help with building has also been given to Lyakirimu, Nganyeni, Masia Marangu, Masia Mamba, Mbahe, Marimeni, Mseroe, Maande, Kotela and Nkweseko schools.
 
"People's participation is the focal point in PAMOJA's development practices."

PAMOJA facilitates the collaboration between local government, civil society and the private sector. The organisation does this by transforming mindsets and attitudes, based on the right of equal access to resources. It promotes the practice of Joint Action and participatory local governance often using international experiences in this area.


EDUCATIONAL ACTIVITIES

Many different activities have been funded and initiated by PAMOJA in the education sector. The establishment of the District Education Board in Same District was a first in Tanzania and has won much praise throughout the Region and country. PAMOJA's approach of Joint Action is an especially useful tool in realising the building of classrooms and has achieved remarkable success. The School Milk Project complemented the earlier dairy support project, while the support of the Mkombozi street children project links with the knowledge acquired in the District Education Boards.

The quality of education in Kilimanjaro Region has been greatly affected by the decline of coffee production due to low prices on the world market. Many parents can no longer afford school fees and children have been leaving school early in order to perform economic activities to sustain the family.

- Haya wewe unasema elimu imeshuka huko Same, kwa sababu ya mbunge wa sasa, hawa ambao ni wahusika wakubwa wa kuimarisha elimu kitaifa, walipokwenda huko Same na kilimanjaro kwa ujumla, hawakusema kuwa kushuka kwa elimu huko ni tatizo la mbunge au wabunge wa Kilimanjaro, kama unavyodai.
 
Je taifa linaonaje kazi ya Mama Kilango mbunge wa Same East, kwa jimbo lake na taifa pia? Hebu soma kidogo hapa chini;-


Habari za Kitaifa Habari zaidi! Slaa, Zitto, Anna Kilango wawika

Stella Nyemenohi
Daily News; Wednesday,March 19, 2008 @00:03


WABUNGE maarufu Dk. Wilbrod Slaa, Zitto Kabwe na Anne Kilango-Malecela, ni miongoni mwa waliowika jana baada ya kuchaguliwa kuwa wenyeviti wa kamati mbalimbali za Bunge.

Kamati hizo za Bunge zilifanya uchaguzi huo kwa mujibu wa kanuni, kwamba kamati hizo huundwa upya inapomalizika nusu ya mikutano ya Bunge. Mikutano 20 hufanyika katika kipindi chote cha Bunge. Katika kipindi kilichopita, zilikuwapo kamati 14 tofauti na sasa ziko 17.

Wakati Dk. Slaa ambaye ni Mbunge wa Karatu (Chadema), akipita bila kupingwa kuongoza Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Chadema kutoka Kigoma Kaskazini, alishinda uenyekiti wa kamati mpya ya Hesabu za Mashirika ya Umma.

Anne Kilango-Malecela ambaye kwa siku za karibuni jina lake limekuwa masikioni mwa wananchi wengi baada ya mchango wake katika sakata la kampuni ya umeme ya Richmond, sasa ataongoza moja ya kamati yenye nguvu bungeni, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.

Mbunge huyo alimshinda Mbunge wa Bahi (CCM), William Kusila, kwa kupata kura nane dhidi ya tatu za mpinzani wake huyo. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana baada ya kuchaguliwa, Dk. Slaa alisema kuchaguliwa kwa wapinzani kuongoza kamati, hakumaanishi kuwaziba midomo.

....Itaendelea..........!
 
Jamaa anaona Same tu ndio wamefeli aulize Lindi,Mtwara mbona wanafeli miaka yote na hakuna anayeshtuka

Looh! statements kama hizi ndio zinanisikitisha sana. Inaelekea kuna Watanzania wamekata tamaa kweli kweli mpaka wanaona kila jambo ni sawa tu.

Anayelalamika anaonekana ndio mjinga na wanaokaa kimya ndio wanajua hali halisi.

No wonder tuna wabunge vilaza bungeni na ukifika uchaguzi bado wanashinda tu. Halafu tunaanza kupiga kelele kwanini hatuendelei?
 
Again jhapa chini ni uchambuzi wa wataalamu wetu wa elimu Tanzania, ambao ni wasomi waliobobea kuhusu elimu, sasa nimesoma yote hapa chini ya uchambuzi wao, sijaona hata mahali pamoja wakilaumu wabunge kuhusu kushuka kwa elimu ya taifa zima na sio jimbo moja tu akama unavyotaka tuamini hapa mkuu, sasa kule elimu zaidi hapa chini ya sababu hasa ya kushuka kwa elimu ya shule zetu za msingi, haina anything to do na mbunge wa Same East, bwa! ha! ah! ah! ah!

Wasomi Nchini Wachambua Sababu za Kushuka Kwa elimu Ya Darasa La Saba.

Na Kizitto Noya

WASOMI wamechambua matokeo ya mtihani wa darasa la saba nchini na kueleza kuwa masomo ya ziada (tuition) na uwezo mdogo wa walimu katika masomo ya hisabati na kiingereza, vimechangia kushusha kiwango cha kufaulu wanafunzi. Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, wahadhili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, idara za Hisabati na Kiingereza walisema kushuka kwa kiwango cha kufaulu wanafunzi katika masomo hayo pia kumechangiwa na ukosefu wa motisha na maslahi kwa walimu.

Mhadhiri wa somo la hisabati chuoni hapo, Rashid Mohamed alisema ingawa hesabu ni tatizo la kidunia, walimu wake nchini hawana motisha hivyo hupoteza mori wa kazi ya kufundisha. "Somo la hesabu (hisabati) halina motisha kuanzia kwa mwalimu hadi mwanafunzi mwenyewe na serikali hailikumbuki kwa namna yoyote ile na matokeo yake wanafunzi wanalikimbia," alisema Mohamed. Alisema serikali inapaswa kutambua kuwa somo la hisabati ni msingi wa masomo mengine yote na ikaanza kuliwekea bajeti maalum kwa ajili ya kuwapa motisha walimu na wanafunzi wanaofanya vizuri darasani mabadiliko makubwa yatatokea.

Alibainisha kwa hali ilivyo sasa wanafunzi wameshindwa kufanya vizuri katika somo la hisabati kwa kuwa hawana mori ya kulipenda kwani halina matumizi ya moja kwa moja katika maisha ya kila siku. "Somo hili linahitaji moyo wa dhati wa mwalimu na mwanafunzi kuanzia ngazi ya shule ya awali hadi chuo kikuu na moyo huo utajengeka endapo kuna mazingira mazuri ya kazi na maslahi kwa walimu," alisema. Mahadhiri mwingine ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini aliulaumu mfumo mzima wa elimu nchini kuwa umechangia kushuka kwa kiwango cha kufaulu wa wanafunzi katika masomo ya Hisabati na Kiingereza.

Alisema Wizara ya Elimu imeshindwa kuwaandaa walimu na kuwatengenezea mazingira mazuri ya kazi kwa kuwaboreshea maslahi, matokeo yake walimu wanafanya kazi katika mazingira magumu na kushindwa kuwajengea wanafunzi wao mori wa kulipenda somo hilo. "Tatizo haliko chini, linaanzia juu serikalini. Kama mwalimu hujui hesabu zinamsaidiaje maishani utawezaje kumfanya mwanafunzi azipende?" alihoji. Alisema kutokana na hali hiyo wataalam wa hisabati wanapungua kadiri siku zinavyosonga wengi wakilazimika kukimbia kazi ya ualimu kutokana na kazi hiyo kutokuwa na maslahi mazuri.

"Hali itabadilika baada ya serikali kuanza kuwajali walimu na kuwathamini kwa maslahi mazuri vinginevyo somo la hesabu litaendelea kuwa tatizo la kitaifa," alisema Mhadhiri mwingine wa Hisabati na Kompyuta, Shaban Nyimvua alitaja masomo ya ziada maarufu kama tuisheni kuwa moja ya sababu zinazowafanya wanafunzi wa mijini kushindwa zaidi katika somo la hisabati kuliko wanafunzi wa vijijini. Alisema tuisheni ni hatari kwa wanafunzi kwani walimu wengi wanafundisha kama biashara kwa lengo la kuongeza kipato na katika kukabiliana na ushindani wa kibiashara, hiyo walimu wanafundisha mbinu za kujibu maswali ya mtihani badala ya misingi ya somo.

"Tuisheni imechangia kwani wanafunzi wanakaririshwa mambo badala ya kufundishwa. Serikali inapaswa kupiga marufuku tuisheni na kuboresha maslahi ya mwalimu ili kumfanya akidhi mahitaji yake kwa mshahara kusudi afundishe vizuri," alisema Nyimvua. Alisema vitendo vya walimu kuuza pipi madarasani na kujipangia muda wa kufundisha masomo ya tuisheni vinatokana na ukosefu wa maslahi ya kutosha kukidhi mahitaji yao. "Siri ya wanafunzi wa vijijini kufanya vizuri zaidi katika hesabu kuliko wanafunzi wa mijini ni tuisheni. Tuisheni inawaharibu watoto kwani wanakaririshwa mambo badala ya kufundishwa misingi yake," alibainisha.

Nyimvua aliishauri serikali kuboresha maslahi kwa walimu ili kuwavuta wenye uwezo kufanya kazi katika shule za msingi na kuinua taaluma badala ya kuwasahau na kuwafanya walimu wenye uwezo kukimbia kufanya kazi katika shule hizo. Profesa mmoja wa somo la kiingereza chuoni hapo ambaye hakutaka kutaja jina lake gazetini alisema kuwa tofauti na zamani ambapo ualimu ulikuwa wito, taaluma hiyo sasa ni ajira inayotafutwa kwa udi na uvumba na watu wasiokuwa na uwezo kuifanya. Alisema matokeo mabaya ya somo la Kiingereza yametokana na mfumo mbovu wa upatikanaji wa walimu wa kulifundisha ambapo kila mwalimu sasa anafundisha somo hilo bila utalaam nalo.

"Inawezekanaje mtu asiyejua kiingereza akamfundishe mwenzake?" alihoji Profesa huyo na kuongeza "Watoto hawafundishwi Kiingereza ila wanadokezwa na kufaulu hivyo kwao ni ndoto". Profesa huyo alitaja mambo yanayomfanya mwanafunzi afanye vizuri katika mitahani kuwa ni umakini wake katika kujifunza, uwezo wa mwalimu anayemfundisha, upatikanaji wa vitendea kazi na mazingira ya kujifunza. Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima nchini, Lambetha Mahai alisema ongezeko la masomo ya kufanyia mtihani mwaka uliopita ni moja ya sababu za wanafunzi hao kufanya vibaya katika mtihani uliopita. Alisema ni jambo la kawaida kwa mwanafunzi kufanya vibaya katika mtihani wake hasa baada ya kubadilishiwa mtaala na kueleza kuwa anatumaini kuwa hali hiyo itaboreka baada ya wanafunzi hao kuzoea.

"Zamani wanafunzi walizoea kufanya mitihani mitatu lakini kwa mara ya kwanza mwaka huu wamefanya mitihani mitano, sasa inategemea mwanafunzi ameelekeza nguvu wapi," alisema Mahai. Juzi Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Margaret Sitta alitangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba yaliyoonyesha kuwa kiwango cha ufaulu mwaka huu kimeshuka kwa asilimia 16.3 ikilinganishwa na mwaka jana. Waziri Sitta alisema kufaulu katika masomo ya hisabati na kingereza si mzuri ikilinganishwa na masomo mengine kwani kiswahili watahiniwa walifaulu kwa asilimia 80.23, sayansi 66.66, maarifa kwa asilimia 56.39, kingereza kwa asilimia 31.31 na hisabati kwa asilimia 17.42.

Alisema kati ya wanafunzi 301 wenye ulemavu waliofanya mtihani huo mwaka huu, wanafunzi 212 wakiwemo wasichana 103 na wavulana 109 wamefaulu mtihani huo. Katika matokeo hayo, mikoa ambayo imeshika nafasi 10 za mwanzo kwa kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi waliofaulu ni Kagera asilimia 73, Dar es Salaam (71), Iringa (70), Manyara (66), Tanga (64), Mbeya (63), Arusha (61), Pwani (58), Morogoro (56), Tabora (56) na Mwanza (52). Mikoa ambayo imetoa wanafunzi wachache waliofaulu ni Shinyanga (34), Dodoma (41), Mtwara (41), Kigoma (42), Ruvuma (44), Lindi (47), Mara (48), Kilimanjaro (48).

Hata hivyo, mikoa ambayo imefaulisha wanafunzi wengi ni Dar es Salaam (40,323), Mwanza (36,681), Iringa (29,858), Mbeya (29,723), Tanga (25,795), Kagera (24,172), Morogoro (21,442). na ambayo wanmefaulu wachache zaidi ni Lindi (8000), Mtwara (9,775) na Kigoma (13,473). Wanafunzi waliofanya mtihani mwaka huu walikuwa 773,550 sawa na asilimia 97.41 waliokuwa wameandikishwa na kwamba kati yao watahiniwa 419,198 sawa na asilimia 54.18 wamefaulu.

Alisema asilimia 90.26 ya wanafunzi 419,198 waliofaulu mtihani wa darasa la saba mwaka huu, wamechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza mwakani katika shule za sekondari za serikali. Naye Andrew Msechu,anaripoti kuwa watalaam wa masuala ya elimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wameelezea matokeo ya mtihani wa Darasa la saba kama changamoto ya kuweza kuangalia nini cha kufanya baada ya kuonekana kushuka kwa kiwango cha kufaulu mwaka huu.

Maoni hayo yanafuatia matokeo ya darasa la saba yaliyotangazwa juzi na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi akielezea kushuka kwa kiwango cha kufaulu kutoka asilimia 70 mwaka 2006 hadi asilimia 54 mwaka huu, pia wanafunzi kutofanya vizuri katika masomo ya hisabati na kiingereza. Wakizungumza na Mwananchi, mtaalamu wa masuala ya utafiti kuhusu elimu, Profesa Issa Omari na Mkuu wa Idara ya ufundishaji na Mitaala Profesa Peter Chonjo walisema kushuka kwa kiwango cha kufaulu kwa mwaka huu si jambo la kushangaza kutokana na mabadiliko yaliyotokea siku za nyuma.

Walisema ni mapema mno kutarajia matokeo mazuri sana ya MMEM kwa kuwa katika miaka ya hivi karibuni hasa kuanzia mwaka 2003 kumekuwa na mabadiliko yasiyo ya kawaida katika kiwango cha kufaulu kwa wanafunzi wa darasa la saba, suala ambalo ndilo linaloshangaza. Ongezeko la ghafla la kiwango cha kufaulu kwa shule za msingi kwa miaka ya hivi karibuni ndiyo suala la kushangaza, kwa mfano kiwango hicho kiliongezeka kwa ghafla mno kwa namna isiyoelezeka kutoka asilimia 27 mwaka 2002 hadi kufikia asilimia 70 mwaka 2006, ongezeko ambalo si la kawaida na halielezeki," alsiema.

Aliainisha kuwa ongezeko hilo la viwango si la kawaida kwa kuwa lilitakiwa kuongezeka taratibu, akitoa mfano wa matokeo ya mwaka 1998 ambao asilimia 21 ya wanafunzi walifaulu. Mwaka 1999 asilimia 19, mwaka 2000 asilimia 22, mwaka 2001 asilimia 29, mwaka 2002 asilimia 27 na kupanda kwa kasi mwaka 2003 hadi kufikia asilimia 40, asilimia 49 mwaka 2004, asilimia 62 mwaka 2005 na asilimia 70 mwaka 2006.

Wataalamu hao kwa pamoja walisema hali hiyo inaonyesha kuwa kuna hali isiyo ya kawaida katika ongezeko hilo la ghafla na kuwataka wadau wanaosimamia masuala ya elimu kufanya utaratibu wa kutafuta chanzo cha tatizo lililopo. Hata hivyo, wakizungumzia suala la kushuka kwa kiwango cha kufaulu kwa wanafunzi katika msomo ya Hisabati na Kiingereza walisema moja ya sababu ni ufundishwaji usiofaa wa wanafunzi kutokana na kuwa na waalimu wasiojua vyema masomo hayo. "Suala hapa ni kuangalia, mitihani inatungwa na watu wale wale, mtaala unaotumika ni ule ule, mtindo unaotakiwa kufundishia ni ule ule, lakini hapa tatizo kubwa linaweza kuwa ni kuwa na walimu wasioweza vyema masomo haya, hasa waalimu hawa walioingizwa kwa mkupuo wa MMEM,

Walisema inaonekana waalimu wengi wanaofundisha masomo hayo hawayajui hivyo ni bora wizara ikiangalia namna ya kuweka utaratibu wa kuwa na waalimu wa diploma (stashahada) kwa ajili ya kufundisha masomo katika shule za Msingi," alisema Profesa Chonjo. Wakati huo huo, Patricia Kimelemeta na Muhibu Said wanaripoti kuwa ongezeko la wanafunzi waliomaliza darasa la saba na kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka huu katika Mkoa wa Dar es Salaam limeongezeka na kufikia asilimia 16 ukilinganisha na mwaka jana.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Afisa Elimu wa Mkoa huu Bernad Makali, jumla ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza ni 40,323 kati yao wasichana ni 17,773 na wavulana ni 22,550. Taarifa hiyo ilisema kuwa jumla ya watahiniwa 56,825 waliofanya mtihani huo,wavulana walikuwa 27,951 na wasichana 28,874 ambayo ni sawa na asilimia 97 ya wanafunzi wote waliosajiliwa, ambao walikuwa 58,326. Taarifa hiyo ilisema kuwa wanafunzi 1,501 hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za utoro,ugonjwa,vifo,mimba na wengine kuhamia mikoa mingine. Ilisema kuwa idadi ya wanafunzi ambao walikuwa watoro wa shuleni ni 1,163,waliokuwa wagonjwa 29, waliofariki 25, waliopata mamba 15 na wengine ambao waliamishwa katika mikoa mingine ni 269.

Ilisema kuwa katika uchaguzi jumla ya wanafunzi 68, wakiwemo wavulana 34 na wasichana 34 walichaguliwa kujiunga na shule za watoto wenye ufaulu mzuri (vipaji maalum). Taarifa hiyo ilisema kuwa wanafunzi 74, wakiwemo wavulana 63 na wasichana 11 wamechaguliwa kujiunga na shule za bweni ufundi. Ilisema kuwa, wanafunzi 76, wakiwemo wavulana 42 na wasichana 34 wamechaguliwa kujiunga na shule za bweni kawaida. Taarifa hiyo ilisema kuwa jumla ya wanafunzi 2,200 wakiwemo wavulana 820 na wasichana 1,380 watajiunga nashule za kutwa za Serikali kuu zilizoko katika mkoa wa Dar es Salaam.

Ilisema kuwa wanafunzi 25,274 wakiwemo wavulana 12,846 na wasichana 12,428 wamechaguliwa kujiunga na shule za wananchi 92 ambazo zimesajiliwa kisheria. Taarifa hiyo ilisema kuwa idadi ya wanafunzi 27,692 wa kidato cha kwanza 2008 waliochaguliwa katika awamu ya kwanza ni kubwa ikilinganishwa na kwana 2007, ambapo jumla ya wanafunzi 25,457 walichaguliwa awamu ya kwanza na ya pili, lakini mpaka sasa kuna ongezeko la wanafunzi 2,235 ambalo ni sawa na asilimia 8. Mkoa unatarajia kujenga jumla ya shule za sekondari mpya 22 ambazo zitachukua jumla ya wanafunzi 6,320 katika awamu ya pili ifikapo Aprili 2008.

Source: Mwananchi

....Itaendelea........!
 
Anayelalamika anaonekana ndio mjinga na wanaokaa kimya ndio wanajua hali halisi.

- Unapoamua kulalamika basi lalamikia panapotakiwa, lakini huwezi kukurupuka tu na maneno ya kuita wabunge waliochaguliwa na wananchi wao kuwa ni vilaza bila sababu maalum, otherwise inakuwa vigumu kujua kilaza hasa ni nani hapa, kabla hujaita mbunge mmoja kialza hebu tupe mifano wabunge ambao sio vilaza ambao in three years za ubunge wao wamebadilisha mifumo ya elimu katika majimbo yao na sasa wanaweza kuwa mfano wa kuigwa na wengine. Ni kweli kama huna ukweli ni vyema kunyamaza kuliko kuharibu majina ya viongozi bure, hapa Jf sio mahali pa kutukana tu kiongozi kwa sababu umeamka leo unajisikia kutukana kiongozi, naona kuna mnaoikubali hii tabia lakini hatutasita kuikataa kwa nguvu zote.

No wonder tuna wabunge vilaza bungeni na ukifika uchaguzi bado wanashinda tu. Halafu tunaanza kupiga kelele kwanini hatuendelei?

- Kwenye hili ukweli uko wazi kwamba tunaowachagua ndio vilaza zaidi, kwa sababu elimu imeshuka kwa taifa zima, sasa tunawarudishaje wabunge wale wale bungeni kama hii nayo ni hoja nzito?, ina maana sisi wananchi ndio vilaza zaidi tumewachagua weee lakini hakuna mabadiliko, tatizo ni letu wananchi kwanza baadaye ndio viongozi.

Kama ni ukilaza basi sisi wananchi ndio vilaza tunaowachagua, au?
 
The quality of education in Kilimanjaro Region has been greatly affected by the decline of coffee production due to low prices on the world market. Many parents can no longer afford school fees and children have been leaving school early in order to perform economic activities to sustain the family.

- Hivi ni mbunge gani anayeweza kuatatua tatizo hili hapo juu?
 
Mtanzania

.....umeeleza vizuri sana ni kw anji agani kiongozi anahitajika kwa jamii.....na anategemewa vipi.......

........bangusule kaleta concern....which is ok as a concern citizen....na concern yake.............does apply sehemu nyingi tu nchini.........

.....now.......check hiyo highlight ya kwanza in red...........tell me how do one arrive to such a conclusion.......!!!

....sidhani kama itakuwa ni kumtendea haki Mh Mbunge kumsema Mbunge eti kuna maradhi ya mpunga na yeye hakuwa na msaada wowote kwa wakulima.........how do one substantiate this claim...........kwa ambao tumekulia kule kajunjumele....tunatakiwa tulielewe hili jambo better than anybody........nafikiri unanisoma............

........Mtu unaweza kuwa na hoja nzuri sana........lakini ukishindwa namna ya kui-present.............mtu anaweza kuku-ignore.....ukashangaa........

......bangusule ana valid concerns......lakini zinaelea......na ndio maana akina Ogah.....wame-comment walivyo -comment..........

.......bangusule should now tell us amelifanyia nini au ana mpango wa kulifanyia nini jimbo lake.........

Kuna mtu hapa kazungumzia suala la wabunge kuwa na ToRs na Performance indicators........wow it might be good idea to start with.....however, we should be able to see and say Mh Mbunge did 1, 2, 3..........to the satisfaction of who......this is debatable.......

Mkuu Ogah,

Matatizo ni hayo hayo hata kule kwetu Kajunjumele. Si niliwahi kuandika, kwanini migomba
iwe na afya nzuri Rungwe, ukifika tu Kyela unakuta imefifia na hata mazao yake hovyo kabisa.

Tatizo kubwa ni uongozi. Enzi za Nyerere hao mabwana shamba walikuwa wanawajibika. Leo hii sijui kwanini hata tumeajiri mabwana shamba ambao wanakaa ofisini mjini na hakuna wanachofanya.

Hapo ndipo uongozi unapokuja, ukiwa na wanaoelewa wajibu wao kama ambavyo nimekuwa nikitumia mfano wa prof. Mwandosya, utakuta bado viongozi na watendaji wengi wa wilaya wanawajibika na hukutani na hilo tatizo sugu kwenye nchi yetu la elimu mbovu, kilimo kibovu nk. kwa kiasi kikubwa. Kuna wilaya zina nafuu sana kuliko wilaya zingine.

Ukipita kwenye wilaya za wasanii, waulize wananchi lini wamemwona bwana shamba? Huenda sasa hata hawaelewi bwana shamba anafanya kazi gani. Wanaonekana mabwana mifugo tu, wakivizia nyama wananchi wanapochinja mifugo yao.

Ukiwaambia wananchi wawabane viongozi wao kwa maendeleo duni, wapambe wanakuja juu, wanaanza kusema unajiandaa 2010. Ni ujinga ujinga mtupu umejaa!

Wenzetu wanajua kweli kulalamika, hata akianguka na kuvunjika mguu kwenye snow anawalalamikia council kwanini wameshindwa kusafisha barabara mpaka snow inaganda? Mpaka wanamlipa. Mbongo atakuambia wewe sio makini kwanini uanguke.

Mimi ushauri wangu ni mmoja kwa vijana mnaojua maana ya maendeleo na ambao kweli mnataka mabadiliko, hiyo 2010 inakaribia. Chukueni forms na huenda wakati umefika wa kuwaonyesha hao yes we can't kwamba yes we can kwa vitendo.

Ukiwa mchapa kazi na kama huna lengo la kushinda Dar na Dodoma ukivizia allowances kwenye kamati, kuna mambo mengi sana unaweza kuyafanikisha kule wilayani. Mambo mengi kinachotakiwa ni mobilization ya resources ile ile ambayo iko wilayani.

Hii ya wabunge kushinda Ulaya kutafuta vitabu na vifaa vingine ambavyo hata havikidhi haja ya kule kwetu, kisha kuongozana na waandishi habari wa kulipwa, lipenenge na mdundiko ni usanii wa hali ya juu mno! Mungu isaidie Tanzania.

Toka nimeanza kumfuatilia prof. Mwandosya sijawahi kuona akitafuta Waandishi wa habari wa kwenda kumwandikia anayoyafanya kule jimboni kwake. Aliyesema chema chajiuza na kibaya cha jitangaza hakukosea kabisa. Timiza wajibu wako, wananchi watajua, wala sio wajinga.
 
Originally Posted by Kaizer
Hivi kazi ya wabunge ni KULETA maendeleo?

Kumbe ni nini?

Swali la Kaizer ni la msingi.

Dhana hii ya kumwona Mbunge ndiye anayewajibika kwa maendeleo ya endeo lake ndiyo inayoturudisha nyuma kimaendeleo. Dhani hii inawatutumua Wabunge kujiona ndiyo wenyewe, wanayoyasema lazima yatekelezwe nk. Kibaya zaidi, ndiyo dhana inayolipeleka Taifa kwenye siasa zaidi kuliko utendaji.

Kimsingi, Mbunge ni mwananchi, ni mwakilishi wa wananchi katika maamuzi na kutunga sheria. Mbunge si Serikali, hana bajeti ya miradi ya maendeleo, hapokei kodi. Serikali ndiyo inayopokea kodi, ndiyo yenye bajeti. Ndiyo inayopaswa kutekeleza miradi ya maendeleo. Mbunge ni sawa na diwani katika kata na Halmashauri yake.

Kwa kuwa inadaiwa kuwa kodi zetu, pamoja na mapato mengine ya Serikali hayatoshelezi mahitaji ndipo suala la wananchi kuchangia ili kutekeleza miradi linakuja. Inapotokea suala la kushirikisha wananchi ndipo diwani na Mbunge wanapohitajika sana ili kupitisha maamuzi na kuwashawishi wananchi.

Msimamo wangu:
Mimi naomba hivi; tujenge tabia ya kuimarisha utendaji na watendaji. Tujenge tabia ya kuwafanya watendaji wawe wawajibikaji. Kazi ya diwani na wabunge iwe ni kusimamia Serikali kuu na serikali za Mitaa. Wanaopaswa kuwajibia wawe ni Serikali yaani watendaji.

Hofu yangu:
Tunapojenga mfumo au mtazamo 'Mbunge ndiye mleta maendeleo' tunakuwa tumemwinua sana kiasi cha kujiona yupo juu ya Serikali hali inayoweza kuathiri utekelezaji wa mipango ya maendeleo hasa ile ya muda mrefu. Mbunge atapenda mipango ya muda mfupi ili kuonyesha alichokifanya katika muda mfupi. Atafanya hivyo kwasababu anataka kura za ndiyo.

Hofu yangu ni kujenga Taifa la wanasiasa. Wanasiasa hawajengi nchi, wanaojenga nchi ni watendaji. Tunapokuwa na Taifa lililojaa wanasiasa, kitakachopewa kipaumbele ni michezo ya kisiasa badala ya kutafuta teknolojia na kutekeleza masuala ya maendeleo.

Kwa mfano Mkuu bangusilo anatoa hoja kuwa Mama Anne Malecela (MB) hafai kuwa Mbunge kwa kuwa kidato cha nne wamefeli mitihani. This is redicolous! Hapa Mbunge kama mwananchi, alaumiwe katika jambo ambalo hakulitekeleza.

Hoja ambayo ingeleta msingi, ilitakiwa kuwa, kwa mfano: walimu katika shule hizo hawapo/hawatoshi na katika bajeti kulikuwa na code ya kuajiri walimu, Serikali haikuajiri na Mbunge hajaihoji Serikali. au kulikuwa na tatizo la vitabu shuleni, serikali ilipendekeza vununuliwe lakini madiwani/Mbunge walikataa kupitisha bajeti ya kununua vitabu. nk,

Hoja za namna hii, ndiyo zenye maana yaani zinawajibisha wataalam/watendaji. Mbunge au diwani anawajibika kwa kuto wasimamia watendaji au kukwamisha mipango mizuri ya Serikali.
 
Swali la Kaizer ni la msingi.

Dhana hii ya kumwona Mbunge ndiye anayewajibika kwa maendeleo ya endeo lake ndiyo inayoturudisha nyuma kimaendeleo. Dhani hii inawatutumua Wabunge kujiona ndiyo wenyewe, wanayoyasema lazima yatekelezwe nk. Kibaya zaidi, ndiyo dhana inayolipeleka Taifa kwenye siasa zaidi kuliko utendaji.

Kimsingi, Mbunge ni mwananchi, ni mwakilishi wa wananchi katika maamuzi na kutunga sheria. Mbunge si Serikali, hana bajeti ya miradi ya maendeleo, hapokei kodi. Serikali ndiyo inayopokea kodi, ndiyo yenye bajeti. Ndiyo inayopaswa kutekeleza miradi ya maendeleo. Mbunge ni sawa na diwani katika kata na Halmashauri yake.

Kwa kuwa inadaiwa kuwa kodi zetu, pamoja na mapato mengine ya Serikali hayatoshelezi mahitaji ndipo suala la wananchi kuchangia ili kutekeleza miradi linakuja. Inapotokea suala la kushirikisha wananchi ndipo diwani na Mbunge wanapohitajika sana ili kupitisha maamuzi na kuwashawishi wananchi.

Msimamo wangu:
Mimi naomba hivi; tujenge tabia ya kuimarisha utendaji na watendaji. Tujenge tabia ya kuwafanya watendaji wawe wawajibikaji. Kazi ya diwani na wabunge iwe ni kusimamia Serikali kuu na serikali za Mitaa. Wanaopaswa kuwajibia wawe ni Serikali yaani watendaji.

Hofu yangu:
Tunapojenga mfumo au mtazamo 'Mbunge ndiye mleta maendeleo' tunakuwa tumemwinua sana kiasi cha kujiona yupo juu ya Serikali hali inayoweza kuathiri utekelezaji wa mipango ya maendeleo hasa ile ya muda mrefu. Mbunge atapenda mipango ya muda mfupi ili kuonyesha alichokifanya katika muda mfupi. Atafanya hivyo kwasababu anataka kura za ndiyo.

Hofu yangu ni kujenga Taifa la wanasiasa. Wanasiasa hawajengi nchi, wanaojenga nchi ni watendaji. Tunapokuwa na Taifa lililojaa wanasiasa, kitakachopewa kipaumbele ni michezo ya kisiasa badala ya kutafuta teknolojia na kutekeleza masuala ya maendeleo.

Kwa mfano Mkuu bangusilo anatoa hoja kuwa Mama Anne Malecela (MB) hafai kuwa Mbunge kwa kuwa kidato cha nne wamefeli mitihani. This is redicolous! Hapa Mbunge kama mwananchi, alaumiwe katika jambo ambalo hakulitekeleza.

Hoja ambayo ingeleta msingi, ilitakiwa kuwa, kwa mfano: walimu katika shule hizo hawapo/hawatoshi na katika bajeti kulikuwa na code ya kuajiri walimu, Serikali haikuajiri na Mbunge hajaihoji Serikali. au kulikuwa na tatizo la vitabu shuleni, serikali ilipendekeza vununuliwe lakini madiwani/Mbunge walikataa kupitisha bajeti ya kununua vitabu. nk,

Hoja za namna hii, ndiyo zenye maana yaani zinawajibisha wataalam/watendaji. Mbunge au diwani anawajibika kwa kuto wasimamia watendaji au kukwamisha mipango mizuri ya Serikali.

Mkuu Nziku,

Unapotosha kabisa dhana ya mbunge kuleta maendeleo au kusukuma maendeleo kwenye jimbo lake.

Haina maana yeye ndiye anaamua nini cha kufanya au yeye ndio anatoa resources za kufanya hayo maendeleo yatokee.

Mbunge ndio kiongozi aliyechaguliwa na wananchi ili awasaidie kutatua matatizo yao. Sasa kama kuna shule mbovu, ni wajibu wa mbunge kuwakutanisha wadau wote na kuangalia namna ya kuongeza ubora.

Kama kuna mabomba yamejengwa na wafadhili, wameondoka na maji nayo yamehama nao, ni wajibu wa mbunge kuangalia kutafuta solution kwa kushirikiana na viongozi wengine wa wilaya pamoja wananchi. Kwanini wafadhili wakiondoka na maji yakauke?

Kama kilimo cha kawaha au mpunga kinaanguka, ni wajibu wa mbunge kupata majibu ya kitaalamu kupitia vyanzo mbalimbali na ikiwezekana ku mobilize resources iliyopo ili kusaidia kutatua tatizo.

Kwa mimi ningetaka mbunge wangu awe a troubleshooter na sio mropokaji tu. Awe na uwezo wa kuwakutanisha watu pamoja kwenye mambo ya maendeleo na sio mtu wa kuwagawa watu.

Aweze kuibana serikali kuu, aweze kuibana halmashauri ya wilaya kwa niaba ya wananchi wake ili watekeleze ahadi walizoahidi, ili miradi wanayoendesha iwe value for money nk.

Nimeshangaa kuona idadi kubwa ya wana JF wanafikiri kazi ya mbunge wa Tanzania ni kwenda kupiga kelele kule Dodoma. Eti kukusanya matatizo ya wananchi na kwenda kuyawakilisha bungeni, nonsense, wala hata huhitaji kusubiri bunge kuwakilisha matatizo yalipo. Kama umeona tatizo, ni hapo hapo kuanza kutafuta solution, kama haiwezekani wilayani, basi huko mkoani, huko wizarani, huko bungeni nk.

Wasanii wetu wengi hawafanyi kitu, anapiga kelele siku moja bungeni, kisha anarudi kwa wananchi na kuwaambia mmenisikia bungeni?
 
Hapa sitashangaa Anna Kilango (aka Mrs John) asipokalia hicho kiti 2010. This is sabotage. Ukiwa mkweli siku zote watu watakuchukia>
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom