Nyalotsi
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 6,978
- 5,025
Yule daktari aliyeandikwa kwenye magazeti miezi michache iliyopita kwa tuhuma za kuhamishia vifaa vya dialysis vya mnh kwenye centre yake amekuja na stail mpya ya kuwafukuza wanachuo clinic. Wanachuo wa Md5 Muhas wanaorotate internal medicine wanatakiwa kuhudhuria wodini na clinic kwa kila kitengo ili kujifunza zaidi ikiwa ni sehemu ya patient oriented medicine. Lakini imejitokeza kwamba dr linda wa nephrology anawafukuza wanachuo hao kila anapowakuta clinic husika. Hali hii imesababisha kukosa mafunzo ya wagonjwa wa nje tofauti na wale waliolazwa wodini. Hili tukio hulifanya hata akiwakuta wanafundishwa na specialist mwingine japokuwa yeye huwa hafundishi kwani kuna group aliikuta ikifundishwa na dr Kisanga yeye akawaambia waondoke wanabana nafasi. Swala la kujiuliza ni, yale si majengo yanayojengwa na kodi zetu? Kwa nini mtu mmoja awanyanya madaktari watarajiwa wa watanzania maskini? Au analipiza kwa uhuni wao walioufanya na nyoni ukagundulika? Intern wanaporudi kufanya kazi huwa wanatukana kwamba hamjui kitu,sasa watajuaje huku wanafukuzwa? Au wamembania kuwa promoted kielimu na hasira zake amamalizia kwa md5? Kama hataki kuwafundisha si awaache wafundishwe na wenye nia na moyo wa kusaidia? Hata kama kuna msuguano wa muda mrefu kati ya mnh na muhas,mbona vitengo vingine hawafukuzi na wanafundisha wanachuo?