Mimi ni kwetu ni Shellui nimeongea na wananchi wa hapa wamechoka na Mwigulu Nchemba wanasema kwamba Dr. Mkumbo uvute soksi kwani 2015 jimbo ni lako.
Ndugu wanajamvi leo nimeamua kuwaletea mpambano wa wanyiramba hawa wawili ambao wanatarajia kumenyana kwenye kinyang'anyiro cha ubunge mwaka 2015 kwenye jimbo la Iramba, wasomi hawa wamekuwa na mvuto wa tofauti katika jimbo la iramba.
Kwa upande wa Mwigulu Nchemba amekuwa kivutio pale anapofika jimboni na kugawa pesa kwa vijana wa stendi, sokoni na mitaa yote anayopita hivyo amefanikiwa kuwa na wafuasia wanaopenda pesa zaidi kuliko yeye mwenyewe hii ni kutokana na pale anapofika jimboni akiwa hana pesa huwa anaambulia matusi na kejeli kutoka kwa vijana wa iramba.
Kwa upande Dr. Kitila Mkumbo huwa akifika jimboni watu wengi hupenda kupiga nae picha, vijana hupenda kusikiliza nasaha zake ambazo huwa zinalenga ktk masuala ya elimu na ujasiriamali, anapenda sana kuwasaidia wazee wanaopendelea kunywa pombe za kienyeji kwa mfano ktk kijiji cha mugela aliwasaidia wazee kwa kuwaezekea kilabu chao cha pombe yao ya kienyeji maarufu kama mtukuru.
Kitila akifika jimboni hupendelea kupita kwenye shule za mkoa mzima kwa mfano aliwahi kupita kwenye shule za A-level za mwenge na tumaini kuwapa ushauri na hamasa ya umuhimu wa kusoma kwa bidii.
Kwa upande wa elimu zao Mwigulu anafanya PhD na kitila anafanya ya uprofesa hivyo kila mtu hapo anaitumia elimu yake kwa jinsi tofauti coz Mwigulu anaamini katika sera za Prof. Lipumba za kugawa pesa na Kitila anaamini katika kuwapa elimu bora wanyiramba ili waweze kufanya biashara zao vyema.
NAOMBA KUWASILISHA.