Dr. Kitila Mkumbo tunakutaka Iramba Magharibi!

kkitabu

Senior Member
Dec 27, 2011
140
47
Mimi ni kwetu ni Shellui nimeongea na wananchi wa hapa wamechoka na Mwigulu Nchemba wanasema kwamba Dr. Mkumbo uvute soksi kwani 2015 jimbo ni lako.
Ndugu wanajamvi leo nimeamua kuwaletea mpambano wa wanyiramba hawa wawili ambao wanatarajia kumenyana kwenye kinyang'anyiro cha ubunge mwaka 2015 kwenye jimbo la Iramba, wasomi hawa wamekuwa na mvuto wa tofauti katika jimbo la iramba.

Kwa upande wa Mwigulu Nchemba amekuwa kivutio pale anapofika jimboni na kugawa pesa kwa vijana wa stendi, sokoni na mitaa yote anayopita hivyo amefanikiwa kuwa na wafuasia wanaopenda pesa zaidi kuliko yeye mwenyewe hii ni kutokana na pale anapofika jimboni akiwa hana pesa huwa anaambulia matusi na kejeli kutoka kwa vijana wa iramba.

Kwa upande Dr. Kitila Mkumbo huwa akifika jimboni watu wengi hupenda kupiga nae picha, vijana hupenda kusikiliza nasaha zake ambazo huwa zinalenga ktk masuala ya elimu na ujasiriamali, anapenda sana kuwasaidia wazee wanaopendelea kunywa pombe za kienyeji kwa mfano ktk kijiji cha mugela aliwasaidia wazee kwa kuwaezekea kilabu chao cha pombe yao ya kienyeji maarufu kama mtukuru.

Kitila akifika jimboni hupendelea kupita kwenye shule za mkoa mzima kwa mfano aliwahi kupita kwenye shule za A-level za mwenge na tumaini kuwapa ushauri na hamasa ya umuhimu wa kusoma kwa bidii.

Kwa upande wa elimu zao Mwigulu anafanya PhD na kitila anafanya ya uprofesa hivyo kila mtu hapo anaitumia elimu yake kwa jinsi tofauti coz Mwigulu anaamini katika sera za Prof. Lipumba za kugawa pesa na Kitila anaamini katika kuwapa elimu bora wanyiramba ili waweze kufanya biashara zao vyema.

NAOMBA KUWASILISHA.
 
Kweli kabisa huyu Dr Kitilya mkumbo anakubalika. Tafadhali mpiganaji kubali wito huu.
Ila binafsi nasikitika sana jinsi hawa wasomi wetu madr na maprof wanavyoacha kazi zao za kufundisha vyuo vikuu na kukimbilia kwenye siasa hata kama huko ndio kuna ulaji mkubwa
 
Mimi ni kwetu ni Shellui nimeongea na wananchi wa hapa wamechoka na Mwigulu Nchemba wanasema kwamba Dr. Mkumbo uvute soksi kwani 2015 jimbo ni lako.

Mkuu mkakati huu utaanza rasmi mapema mwakani. Kuna wazee najaribu ku-organise ili wakamushauri Dr.Mkumbo aje kujenga Iramba yetu......pia kunajaribu kuwaalika makamanda wa makao makuu waje kutupa kampani M4C tarafa ya Shelui kama walivyofanya Iringa.....sisi ndo tuliyemweka Mwigulu na sisi ndo tutamuondoa
 
Mkuu mkakati huu utaanza rasmi mapema mwakani. Kuna wazee najaribu ku-organise ili wakamushauri Dr.Mkumbo aje kujenga Iramba yetu......pia kunajaribu kuwaalika makamanda wa makao makuu waje kutupa kampani M4C tarafa ya Shelui kama walivyofanya Iringa.....sisi ndo tuliyemweka Mwigulu na sisi ndo tutamuondoa

nakubali.doct.aende.mkome kuyaweka ma m2 majinga kama mugalu...mwakani mbali.naomba mkakati wa kumwondoa huyo mlevi wa sifa uwe january5 au j5.naomba nijulishwe.
 
naunga mkono hoja kabisa.dogo kalewa sifa hadi bsi.eti juzi kaenda ndago kuangalia kama yale mauaji wa katibu wa ccm yametulia,hyo damu itakulilia wewe mwigulu,
 
Mimi ni kwetu ni Shellui nimeongea na wananchi wa hapa wamechoka na Mwigulu Nchemba wanasema kwamba Dr. Mkumbo uvute soksi kwani 2015 jimbo ni lako.
Na mtaota na kusubiri sana na huyo kitila wenu. dr. gani hawezi hata kufanya analysis za kidaktari.
 
Mimi ni kwetu ni Shellui nimeongea na wananchi wa hapa wamechoka na Mwigulu Nchemba wanasema kwamba Dr. Mkumbo uvute soksi kwani 2015 jimbo ni lako.
KOSA LILIKUWA LETU MA KING MAKER (wa kinampanda ) HATUKUWA SERIUS HADI TUKARUHUSU WATOTO KUINGIA CHUMBANI KWA BABA NA MAMA! 2015 ....MKUMBO NJOO KINAPANDA TUONGEE ,ANGALAU TUNAWEZA KUKUSIKILIZA!
 
nenda mpiganaji,takribani miaka 51 ya uhuru wanyiramba watakuwa wamepata mtu sahihi. Kama mwakilishi wao!hima katoe elimu ya uraia huku ukitumia mwanya wa kiuchumi uliupo kupitia kilimo cha alizeti kupunguza umaskini na idadi ya tembe.hapo kwenye kichwa cha mada, nimesema uanze kazi 2014,(uhakikishe cdm inazoa viti vingi kwa serikali za mitaa.hyo itakuwa simpo kwako 2015.nina hakika utapata kura za kutosha kuanzia makunda,anakotoka mrithi wa mikoba ya sheh yahya.mwigulu kwa kusema kwa kikwao tyunu mao(hakiamama).cdm haiwezi shinda hata nusu ya nchi nayo inakufa 2015.hayo yalitamkwa kibaha katika kuwaelezea wana kibaha jinsi walivyotekeleza kiini macho chao kiitwacho ilani.
 
Na mtaota na kusubiri sana na huyo kitila wenu. dr. gani hawezi hata kufanya analysis za kidaktari.
Dr Mkumbo kipanga sana na ndie anastahili kuwa mbunge Iramba si Mwigulu ambaye anakariria tu hana ubongo.
 
Pole pole wana JF,mda si mrefu Mwigulu anaweza anza okota makopo kwani akisikia jina la Dr. Kitila Mkumbo network inakata gafla.
 
msimpoteze mwenzenu akakosa kazi bure mwigulu jimboni kwake hata muamie CDM yoote hamtamuweza
 
Pole pole wana JF,mda si mrefu Mwigulu anaweza anza okota makopo kwani akisikia jina la Dr. Kitila Mkumbo network inakata gafla.

msimdanganye dr kitila akaacha ugali wake bure jimbo la mwigulu hata mpeleke masangoma yenu hamuambulii kitu
 
Tetesi nilizonazo kutoka kwa chanzo cha habari cha uhakika hawa vijana watapambana wakipitishwa na vyama vyao kwenye kinyang'anyiro cha Ubunge 2015.

Je ni nani anafaa na atafaa kwa ajili ya kusaidia kazi za kibunge, kuwakilisha wana Iramba, Kutunga sheria, kuisimamia serikali na kuwatetea wana Iramba kupata haki yao ya msingi ya maendeleo.

Compare and contrast between the two.

Tuangalie jimbo la Iramba tangia uhuru likiwa chini wa wabunge wa chama kimoja na wakati huu wa siasa za ushindani. Je kuna maendeleo yeyote au matumaini zaidi ya siasa za kila siku? Je kijana mdogo kabisa mwenye vyeo vya kutosha ndani ya chama chake ameweza vipi kuharakisha maendeleo ya jimbo lake kwa kutetea mgawo wa jimbo lake kwa kipindi alichoweza kulitumikia??

Je Dr Mkumbo akishinda nini matumaini ya wana Iramba kwake?
Does records matters??

Je nani mwenye sifa safi za kiuongozi??

Mzee wa Kinepi kutoka Iramba - Tunaomba mwakilishi mtendaji na si jina.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom