Domy
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 4,700
- 1,084
Pamoja na mambo mengine akiongea katika kipindi cha changamoto kinachorushwa na startv Dr.Kitila Mkumbo wa Udsm amesema kushangilia utekelezaji wa majukumu ya serikali ni uzuzu.
"Watu wanashangilia kama mazuzu eti serikali imetujengea barabara ya lami wakati ni haki yao kujengewa barabara na huo ni wajibu wa serikali kuwaletea wananchi maendeleo hakuna haja ya kushangilia na kuwapongeza mawaziri"
Amesema miongoni mwa mambo yanayofanya huduma za jamii kuwa mbovu ni pamoja na gharama kubwa ya uendeshaji wa serikali(utawala),"serikali inaacha kuwajengea wananchi zahanati,shule lakini inakimbilia kuongeza mikoa na wilaya jambo ambalo ni mzigo mkubwa kwa mwananchi wa kawaida."Hiyo mikoa mipya inamsaidia nini mwananchi?amehoji.
"Ukitaka kuharibu taifa ua elimu,Somalia wamefika pale walipo kwa sababu waliua elimu na ndio maana mpaka leo wako vile walivyo.
Akiongelea Swala la katiba mpya amesema ilitakiwa utaratibu wa ukusanywaji wa maoni uboreshwe zaidi kwa kushirikisha mawazo ya vyama vya siasa kama Chadema na vinginevyo,Amesema mwananchi hana haja ya kujua maana ya katiba bali aseme nini anataka kifanyike kwa ajili ya maisha yake.
Nawasilisha kwa mjadala zaidi wa kauli hizi.
"Watu wanashangilia kama mazuzu eti serikali imetujengea barabara ya lami wakati ni haki yao kujengewa barabara na huo ni wajibu wa serikali kuwaletea wananchi maendeleo hakuna haja ya kushangilia na kuwapongeza mawaziri"
Amesema miongoni mwa mambo yanayofanya huduma za jamii kuwa mbovu ni pamoja na gharama kubwa ya uendeshaji wa serikali(utawala),"serikali inaacha kuwajengea wananchi zahanati,shule lakini inakimbilia kuongeza mikoa na wilaya jambo ambalo ni mzigo mkubwa kwa mwananchi wa kawaida."Hiyo mikoa mipya inamsaidia nini mwananchi?amehoji.
"Ukitaka kuharibu taifa ua elimu,Somalia wamefika pale walipo kwa sababu waliua elimu na ndio maana mpaka leo wako vile walivyo.
Akiongelea Swala la katiba mpya amesema ilitakiwa utaratibu wa ukusanywaji wa maoni uboreshwe zaidi kwa kushirikisha mawazo ya vyama vya siasa kama Chadema na vinginevyo,Amesema mwananchi hana haja ya kujua maana ya katiba bali aseme nini anataka kifanyike kwa ajili ya maisha yake.
Nawasilisha kwa mjadala zaidi wa kauli hizi.