Dr. Kitila Mkumbo Anafaa Kugombea Urais wa Tanganyika Kwa Tiketi ya CHADEMA

Ama humfahamu Mkumbo au unapiga propaganda.

Nakwambia, tukiacha chaguzi za wabunge na Rais, hakuna uchaguzi ulio mgumu kama wa Rais wa wanafunzi wa Chuo Kikuu, na hili Kitila alifanikiwa vizuri sana katika kujenga mvuto na kuchaguliwa. Lakini pia aliongoza vizuri.

Ukimsikia Mkumbo anaelezea Vision yake ya kukabiliana na changamoto zilizo mbele yake katika jukumu analotaka kulichukua, utamkubali tu!!!

Kuwa Rais wa chuo siyo kigezo cha kuwa Rais wa Tanganyika, kama ni hivyo hata Mtatiro naye anaweza kuwa Rais wa Tanganyika.

Ukitaka kumpima Kitila mwambie agombee nafasi ya Katibu Mkuu au Mwenyekiti ndani ya chama chake cha Chadema kama Kaskazini watakubali hata yeye mwenyewe analijua hilo.
 
Ndiyo kazi mliyotumwa na ccm propaganda za kijinga kijinga!
Kuwa Rais wa chuo siyo kigezo cha kuwa Rais wa Tanganyika, kama ni hivyo hata Mtatiro naye anaweza kuwa Rais wa Tanganyika.

Ukitaka kumpima Kitila mwambie agombee nafasi ya Katibu Mkuu au Mwenyekiti ndani ya chama chake cha Chadema kama Kaskazini watakubali hata yeye mwenyewe analijua hilo.
 
Wizara ya elimu inamfaa sana. in fact Dr. Kitila ni Kiongozi wa kuzaliwa na siasa za majukwaani hazimfai sana. Ukimpa u waziri wa elimu Kitila ujue mabadiliko makubwa kwenye wizara na wala sio routine ya Dr. Kawambwa ya sasa
 
Kwa umbea wako wa kuandika vitu visivyo kuwepo, wenda ungefanikiwa kuwalaghai wanakijiji na wangeipa CHADEMA kwa mwamvuli wa Mkumbo.
Mkuu hakuna uongo nilioandika. Kama ni uongo weka habari sahihi.

Kitila Mkumbo alikuwa Rais wa Wanafunzi wa UDSM (DARUSO) mwaka 1998/99 na ilikuwa kwa kufanya kwake kampeni na kukubalika na watu. Kama ni uongo niambie Rais wa wanafunzi mwaka huo alikuwa nani.

Nikiongezea tu, makamu wake alikuwa Dr. Francis Michael Kasabubu wa Idara ya Human Resources Management.

Kwa kuongezea, Kitila pia amekuwa mwenyekiti wa Umoja wa Wahadhiri wa UDSM (UDASA) mpaka mwaka jana, ambapo sasa Mwenyekiti ni Dr. Francis Michael. Serikali ilikuwa haifurahii kuwepo kwake kwenye uongozi wa UDASA na wakawa wanampiga vita [h=1]Mpango wa kumtimua UDASA Dr. Kitila Mkumbo wasukwa[/h]
Kuhusu Iramba, Kitila hakuwa kwenye timu ya kupiga kampeni Iramba. Ikumbukwe kuwa mpaka sasa yeye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu, na ana majukumu ya uongozi. Ni mkuu wa kitivo cha elimu katika chuo kikuu kishiriki cha elimu, Dar es Salaam yaani (Dean, Faculty of Education at the Dar es Salaam University College of Education). Kazi hizo na kazi za kufundisha hazimpi nafasi ya kwenda Iramba kwa kampeni.

Kitila amekuwa akienda Iramba mara kwa mara kwa sababu ya kuitwa mahakamani kwenye kesi ya kubumbwa na Mwigulu Nchemba.

Jibu kwa facts kama unazo.
 
Kuwa Rais wa chuo siyo kigezo cha kuwa Rais wa Tanganyika, kama ni hivyo hata Mtatiro naye anaweza kuwa Rais wa Tanganyika.

Ukitaka kumpima Kitila mwambie agombee nafasi ya Katibu Mkuu au Mwenyekiti ndani ya chama chake cha Chadema kama Kaskazini watakubali hata yeye mwenyewe analijua hilo.
Ni kweli si kigezo cha kutosha. Lakini kumbuka siongelei tu kuwa alikuwa Rais, bali alikuwa kiongozi mzuri sana akiwa Rais.
 
Inaonekana kabisa kuwa CCM mnamwogopa sana ndio maana mnatoa kauli za mfa maji. Sisi wanachadema tunajua jamaa ni jembe, kama wewe huoni shauri yako
Ujembe wa Kitila Mkumbo ni wa lipi? au kushiriki usaliti yeye na Zitto Kabwe? Kilaza kabisa wewe. Profesa Abdallah Safari ndio awe mgombea wa Chadema kwa Tanganyika.
 
When will we stop this nonsense.

Watu kama wewe ndiyo hamuitakii mema CHADEMA!.

Charity begins at home.

Kama watu wa kijijini kwake hawakuweza kumpatia au kumpandisha kwenye ladder ya uongozi, wewe ndiyo unafikiri watanzania wengine ni wajinga kwa kiasi hicho unachofikiri?.

You're just destroying him instead of nurturing him.
 
Hakuna kitu kama raisi wa Tanganyika. Wamesema Tanganyika na Zanzibar we na magavana. Ugavana na uraisi vitu viwili tofauti.
 
Mkuu hakuna uongo nilioandika. Kama ni uongo weka habari sahihi.

Kitila Mkumbo alikuwa Rais wa Wanafunzi wa UDSM (DARUSO) mwaka 1998/99 na ilikuwa kwa kufanya kwake kampeni na kukubalika na watu. Kama ni uongo niambie Rais wa wanafunzi mwaka huo alikuwa nani.

Nikiongezea tu, makamu wake alikuwa Dr. Francis Michael Kasabubu wa Idara ya Human Resources Management.

Kwa kuongezea, Kitila pia amekuwa mwenyekiti wa Umoja wa Wahadhiri wa UDSM (UDASA) mpaka mwaka jana, ambapo sasa Mwenyekiti ni Dr. Francis Michael. Serikali ilikuwa haifurahii kuwepo kwake kwenye uongozi wa UDASA na wakawa wanampiga vita [h=1]Mpango wa kumtimua UDASA Dr. Kitila Mkumbo wasukwa[/h]
Kuhusu Iramba, Kitila hakuwa kwenye timu ya kupiga kampeni Iramba. Ikumbukwe kuwa mpaka sasa yeye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu, na ana majukumu ya uongozi. Ni mkuu wa kitivo cha elimu katika chuo kikuu kishiriki cha elimu, Dar es Salaam yaani (Dean, Faculty of Education at the Dar es Salaam University College of Education). Kazi hizo na kazi za kufundisha hazimpi nafasi ya kwenda Iramba kwa kampeni.

Kitila amekuwa akienda Iramba mara kwa mara kwa sababu ya kuitwa mahakamani kwenye kesi ya kubumbwa na Mwigulu Nchemba.

Jibu kwa facts kama unazo.

Jitihada zako za kumtetea Mkumbo kuwa yeye ni jembe haziwezi kuzaa matunda kwani humu JF tuna mfahamu kuwa Mkumbo ni mweupe tu.

Umeeleza kwenye maelezo yako ya awali kuwa alifanikisha kuwatuliza wana-COET kwa ushawishi wake, huu ndio uongo mkuu. Kuhusu kuwa rais wa DARUSO hilo sipingi.

Pia umemtetea kuwa yeye hakuwa kwenye timu ya kampeni iliyo ongozwa na zezeta Ally Bananga, ni kweli, ila labda hukuwa makini katika kuisoma post yangu.

Nimesema, kama wanakijiji wangemjua kuwa Kitila ni jembe, wangeichagua CHADEMA kwa mwamvuli wake, maana hata sababu ya Kitila kufunguliwa kesi na Mwigulu ni kwa sababu ya kusimama kwake majukwaani na kukashifu watu badala ya kufanya siasa safi.

Mtu wa namna hii asie kuwa na maadili wala staha nani ampe urais?
 
Mmh, hizi sifa zote, kazipata kwa kazi gani kubwa alowahi fanya kitaifa? Uzoefu wake ukoje?

Unaweza kuwa anapafomu sababu yuko kwenye comfort zone yake, ukimtoa nje ya hapo ni magumu, unakumbuka Mwantumu Mahiza enzi za uwaziri, alikuwa haoni hata mlango, lakini kuwekwa Mkuu wa Mkoa unaoa hata anakukuruka.

Lakini, kingine, kuwa mkosoaji mzuri haimaanishi ni mtendaji mzuri

Na kitaifa anajulikana na kukubalika kisi hicho?

Haya jipimeni wenyewe.

Nikipepesa macho, namwona kijana msomi, mwenye uwezo mkubwa wa kiuongozi, mwenye hoja nzito, mnyenyekevu, asiyependa makuu, asiye na majivuno, asiye na doa, anayekubalika kwa watu wa rika zote, mchapa kazi na mzalendo wa kweli, huyu si mwingine ni Dr Kitila Mkumbo.
 
Mtu hajawahi hata kuwa katibu kata watu wakampima uwezo wake katika masuala ya kisiasa utawezaje kumpa nafasi kubwa ya urais wa Tanganyika.

Mpaka leo hajaweza kusema alitumia vigezo gani katika kuchaguwa wabunge wa viti maalum Chadema.

Nadhani angeanza kwanza kugombea ubunge huko Singida.
Mkuu kuwa Rais wa Chuo kikubwa kama UDSM bado hana uwezo naanza kushikwa na wasiwasi juu ya uelewa wako
 
Tusubir rasimu ya katiba ya Tanganyika itakuja na vipengele gani!

Wanaweza wakaweka vifungu vya kishetani vinavyosema:"mtu aliyewahi kuwa lecturer wa chuo chochote cha serikali TZ HANA sifa ya kugombea nafasi ya Rais wa Tanganyika"
 
Kitila Mkumbo ni jembe binafsi namkubali sana, natamani aje kuwa waziri wa elimu Tanganyika kwani sekta ya elimu ataimudu vizuri sana.
 
Last edited by a moderator:
When will we stop this nonsense.

Watu kama wewe ndiyo hamuitakii mema CHADEMA!.

Charity begins at home.

Kama watu wa kijijini kwake hawakuweza kumpatia au kumpandisha kwenye ladder ya uongozi, wewe ndiyo unafikiri watanzania wengine ni wajinga kwa kiasi hicho unachofikiri?.

You're just destroying him instead of nurturing him.
Mkuu sio lazima aanzie nyumbani!!!! Urais haupatikani kwa ukabila wala udini kama mnavyofikiria nyinyi CCM. Rais anachaguliwa na watanzania wote na siyo sehemu uliyozaliwa tuu
 
Mtu hajawahi hata kuwa katibu kata watu wakampima uwezo wake katika masuala ya kisiasa utawezaje kumpa nafasi kubwa ya urais wa Tanganyika.

Mpaka leo hajaweza kusema alitumia vigezo gani katika kuchaguwa wabunge wa viti maalum Chadema.

Nadhani angeanza kwanza kugombea ubunge huko Singida.
bora tupate mtu fresh,kuliko hao waliopitia uwenyekiti uvccm,uwaziri bure kabisa.DR.Kitila akigombea kura yangu atapata
 
Ujembe wa Kitila Mkumbo ni wa lipi? au kushiriki usaliti yeye na Zitto Kabwe? Kilaza kabisa wewe. Profesa Abdallah Safari ndio awe mgombea wa Chadema kwa Tanganyika.

Wewe ndiyo kilaza unatutajia Prof. Safari hajawahi kuwa hata mjumbe wa kata, kama unampenda labada kampe urais wa nyumbani kwenu.
 
Umeeleza kwenye maelezo yako ya awali kuwa alifanikisha kuwatuliza wana-COET kwa ushawishi wake, huu ndio uongo mkuu.
Kitila alikuwa Rais wa DARUSO UDSM main campus 1998/99 na mimi pia nilikuwa kwenye serikali hiyo ya wanafunzi. Najua ninachokisema, kwa kuwa I was an insider.

Nikukosoe pia kuwa wakati ule sisi tunasoma pale Engineering ilikuwa kitivo na haikuwa COET bali ilikuwa FoE (Faculty of Engineering).
Nimesema, kama wanakijiji wangemjua kuwa Kitila ni jembe, wangeichagua CHADEMA kwa mwamvuli wake, maana hata sababu ya Kitila kufunguliwa kesi na Mwigulu ni kwa sababu ya kusimama kwake majukwaani na kukashifu watu badala ya kufanya siasa safi.
Naomba niseme tu kuwa ushindi wa CCM kwenye viti vya vijiji Iramba si kipimo cha kukubalika kwa Kitila kwa kuwa Kitila hakuwa mgombea na wala hakuwa kwenye timu ya kampeni.

Kitila hakashifu watu, kama una ushahidi wa kashfa tuwekee hapa. Kitila anakosoa, shida ya CCM ni kuwa anayewakosoa wanaona anawakashifu.

Mtu wa namna hii asie kuwa na maadili nani ampe urais?

Naomba nitofautiane nawe na dhana ya maadili unayoleta. Kukosoa walioko madarakani ni jukumu la viongozi wa vyama vya upinzani na haihusiani na maadili.
 
Mtu hajawahi hata kuwa katibu kata watu wakampima uwezo wake katika masuala ya kisiasa utawezaje kumpa nafasi kubwa ya urais wa Tanganyika.

Mpaka leo hajaweza kusema alitumia vigezo gani katika kuchaguwa wabunge wa viti maalum Chadema.

Nadhani angeanza kwanza kugombea ubunge huko Singida.
Mkuu na mimi naona nitagombea urais kwa tkt ya chadema, nimeamua kurudi
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom