VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,800
Mhadhiri Mwandamizi wa UDSM, Dr. Kitila Mkumbo jana alimpa wakati mgumu Rais wa zamani wa Afrika Kusini Thabo Mbeki.
Hiyo ilikuwa ni katika wakati wa maswali kwa Mbeki baada ya hotuba yake katika ukumbi wa Nkrumah wa UDSM.
Swali la Dr. Kitila lilijikita katika kauli ya Mbeki, wakati akiwa madarakani, kuwa UKIMWI hauenezwi na ngono ila shida na umaskini wa wananchi. Dr. Kitila alimkumbusha Mbeki juu ya kifo cha mtoto wake (wa Mbeki) kilichosababishwa na UKIMWI. 'Unaendelea kusimamia kauli yako?' aliuliza Dr.Kitila
Mbeki aliacha kujibu hilo swali. 'I will not respond to that pinching question' alisema Mbeki. Na hapo ndipo ukawa mwisho wa maswali kwa Mbeki ingawa swali la Dr.Kitila lilikuwa la pili tu.Prof. Mukandala alimaliza muda wa maswali ghafla
Post Update - Kitila's question:
Hiyo ilikuwa ni katika wakati wa maswali kwa Mbeki baada ya hotuba yake katika ukumbi wa Nkrumah wa UDSM.
Swali la Dr. Kitila lilijikita katika kauli ya Mbeki, wakati akiwa madarakani, kuwa UKIMWI hauenezwi na ngono ila shida na umaskini wa wananchi. Dr. Kitila alimkumbusha Mbeki juu ya kifo cha mtoto wake (wa Mbeki) kilichosababishwa na UKIMWI. 'Unaendelea kusimamia kauli yako?' aliuliza Dr.Kitila
Mbeki aliacha kujibu hilo swali. 'I will not respond to that pinching question' alisema Mbeki. Na hapo ndipo ukawa mwisho wa maswali kwa Mbeki ingawa swali la Dr.Kitila lilikuwa la pili tu.Prof. Mukandala alimaliza muda wa maswali ghafla
Post Update - Kitila's question:
Katika swali langu sikuzumzungumzia chochote kufariki kwa mtoto wa Mbeki kwa sababu wala sijui hilo jambo. Swali langu lililenga kupata ufafanuzi juu ya madai ya Thabo Mbeki alipokuwa Rais kwamba UKIMWI hausababishwi na virusi vya UKIMWI bali unasababishwa na kuharibiwa kwa mfumo wa kinga mwili kwa sababu ya umaskini na lishe duni. Msimamo wake ulisababisha Afrika Kusini kukataa kupokea msaada wa ARVs na maelfu ya watu kufa bila sababu.
Kwa Kiingereza swali lilikuwa framed kama ifuatavyo:
In the 1990s, supported by scientists described as minority, dissident and maverick, you boldly and courageously claimed that AIDS is not caused by HIV, but by a collapse of the immune system due to poverty and poor nutrition. As a result of your stance, your Government refused to receive the ARV assistance from international pharmaceutical industries. Your stance also almost caused a moratorium in HIV prevention efforts not just in south africa, but in the whole continent. Recently, Harvard scientists published a study report showing that about 300,000 died in South Africa because of your policy stance. The findings of this study have been validated by my scientists, including those in South Africa.
i) Reflecting and looking back to your presidency, and given the pace at which South Africa has reduced the HIV infection rates and HIV related deaths, do you still maintain the same position regarding the cause of HIV?
ii) Do you have any regrets over your position?
Ukweli ni kwamba Mzee Mbeki alijibu swali lakini alisema angehitaji muda zaidi kufafanua. Aliendelea kusisitiza msimamo wake kwamba 'AIDS is a syndrome caused by many conditions'. Lakini tofauti na nyuma this time around alitaja, kimakosa, kwamba HIV kama moja ya conditions zinazosababisha AIDS. Kuhusu utafiti niliomtajia wa wana sayansi wa Havard alisema kwamba kuna utafiti mwingine unaopingana na huo, na akaahidi kunitumia ripoti yake.
Kwa hiyo sio sahihi kwamba hakujibu kabisa swali. Alijibu, lakini sio kikamilifu kwa sababu aliyosema ni kutokuwa na muda wa kutosha.
Sasa mimi sielewi kwa nini watu hapa JF wameanza kuwa na tabia za kujadili mambo nusunusu na kiupotoshaji, hasa pale inapotokea kwamba lugha iliyotumika ni Kiingereza. Nililiona pia hili juzi kwenye ushiriki wangu kwenye kipindi cha 'This Week in Perspective'. Watu wanatabia ya kudaka neno moja na kuibuka nalo na kufanya ndio mjadala. Sasa najiuliza tatizo ni udhaifu katika ujenzi wa hoja za kimantiki au hii lugha inayoonekana kutushinda sisi wa TZ?