Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Leo Septemba 11, 2018. Jopo la Madaktari Bingwa wa MOI linalomhudumia Waziri wa Maliasili na Utalii Dr Hamisi Kigwangalla, limemruhusu kutoka wodini baada kujiridhisha kwamba afya yake imetengamaa na anaweza kurudi nyumbani ili kuja hospitali kama mgonjwa wa nje.
Jopo hilo la madaktari bingwa 5 wa kada za Mifupa, Usingizi na Magonjwa ya Ndani, limefikia uamuzi huo baada ya baada ya kumhudumia Dr Kigwangalla toka Agosti 12, 2018 alipohamishiwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI kwa ajili ya matibabu ya kibingwa ya mkono wake wa kushoto baada ya kupata matibabu mengine katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface amemtakia kila la heri Dr Kigwangalla katika kutekeleza majukumu yake ya Kitaifa kwani ni muda muafaka wa kwenda kuwatumikia wananchi.
"Kwa niaba ya Taasisi ya Mifupa MOI tunakutakia kila la heri katika kutekeza majukumu yako ya ujenzi wa Taifa, ilikuwa heshima kubwa kuwa nawe hapa kwa kipindi cha takribani mwezi mmoja, tunaamini umeridhishwa na huduma zetu na kama kuna mahali umeona mapungufu ni vema ukatujulisha ili turekebishe", alisema Dkt. Boniface
Kwa upande wake Dr Kigwangalla ameushukuru uongozi wa Taasisi ya MOI, madaktari na wauguzi ambao wamekuwa wakimhudumia kwa kipindi chote alipokuwa wodini.
Jopo hilo la madaktari bingwa 5 wa kada za Mifupa, Usingizi na Magonjwa ya Ndani, limefikia uamuzi huo baada ya baada ya kumhudumia Dr Kigwangalla toka Agosti 12, 2018 alipohamishiwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI kwa ajili ya matibabu ya kibingwa ya mkono wake wa kushoto baada ya kupata matibabu mengine katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface amemtakia kila la heri Dr Kigwangalla katika kutekeleza majukumu yake ya Kitaifa kwani ni muda muafaka wa kwenda kuwatumikia wananchi.
"Kwa niaba ya Taasisi ya Mifupa MOI tunakutakia kila la heri katika kutekeza majukumu yako ya ujenzi wa Taifa, ilikuwa heshima kubwa kuwa nawe hapa kwa kipindi cha takribani mwezi mmoja, tunaamini umeridhishwa na huduma zetu na kama kuna mahali umeona mapungufu ni vema ukatujulisha ili turekebishe", alisema Dkt. Boniface
Kwa upande wake Dr Kigwangalla ameushukuru uongozi wa Taasisi ya MOI, madaktari na wauguzi ambao wamekuwa wakimhudumia kwa kipindi chote alipokuwa wodini.