Kina Ridhiwan au?Vyovyote vile lkn wapiga Dili mwisho wenu umefika tunataka Kodi yetu!
Kina Ridhiwan au?Vyovyote vile lkn wapiga Dili mwisho wenu umefika tunataka Kodi yetu!
Kodi kawapige maiti mortuary ufurahi!
Ha ha ha!Kwa nini maiti walipe kodi? Wao yao yalishakwisha!
Huko Nzega hawa jamaa wa Resolute wameacha shimo la kina kirefu pamoja na uharibifu wa mazingira wa kutosha. Nina imani NEMC wanajua na wanafuatilia hambo hilo.Resolute wamelipa kodi kiasi gani kwa miaka yote waliokuwepo hapa kwetu? Nenda Nzega ukaone wameacha nini, na wananchi wamefaidika vipi na dhahabu yao iliyochukuliwa yote, au Barrick aka Acasia wamelipa nini? Tanzanite yetu Tanzaniteone wamelipa nini kwa wananchi wetu nenda Mererani ukawaulize Wananchi wamepata nini miaka yote ya kuwepo kwa Tanzanite?
Hivi nani aliyeingia nao mkataba? Hao unaowatetea hawakujua hayo mambo? Nani asiyejua ulaji uliokuwa unapatikana ndani ya chama? Ccm wenyewe ndiyo wakwanza kuliga dili. Mda huu hatuongelei porojo. Jibu hoja za kafumu na dangote kinadharia na siyo kimaneno. Dangote hana miaka miwili kuanzia aanze uzalishaji, mkubwa wenu hakuwepo kwenye baraza la mawaziri? Kwa nini hakuliona hilo?Resolute wamelipa kodi kiasi gani kwa miaka yote waliokuwepo hapa kwetu? Nenda Nzega ukaone wameacha nini, na wananchi wamefaidika vipi na dhahabu yao iliyochukuliwa yote, au Barrick aka Acasia wamelipa nini? Tanzanite yetu Tanzaniteone wamelipa nini kwa wananchi wetu nenda Mererani ukawaulize Wananchi wamepata nini miaka yote ya kuwepo kwa Tanzanite?
Hayo maarifa ya huyo jamaa ni kuuza nchi, haiwezekani watu wenye akili tmamu mumpe vitu hivyo vyote kwa unafuu huo, haiwezekani!!tunaangamia kwa kukosa maarifa" ...haijaandikwa kwamba 'tunaangamia kwa kukosa nguvu au silaha'.
Ha ha ha!
Una kumbukumbu fupi!
Kaipige kodi UFI, SUNGURATEX, MWATEX, Urafiki, AirTanzania.
Kodi nyingi ipo hapo!
Naona una ugeni akilini.Unaleta masikhara wewe, leo hauna zamu nini ya kulinda kwa Lowasa au amesafiri?
Na nyie wazungusha viuno mnaua viwanda huku mnaimba nchi ya viwanda labda nchi ya VITANDA siyo viwanda nnavyovijua mimi.Wazungurusha mikono na washika ukuta mmeona suala la Dangote ndiyo point yenu kisiasa kuikosoa serikali yetu pendwa, fukuzeni mafisadi mnaowalea kwanza.
Unajua kiwanda cha Dangote kimetoa ajira kwa watanzania wangapi? Uwe unajiongeza kabla ya kuandika pumbaHayo maarifa ya huyo jamaa ni kuuza nchi, haiwezekani watu wenye akili tmamu mumpe vitu hivyo vyote kwa unafuu huo, haiwezekani!!
Mnajitahidi kuua kila chanzo cha kodi kwa bidii kubwa!Mpiga dili huyo akafie mbele, sisi tunataka Kodi zetu kwa ajili ya maendeleo ya watu wetu!
Hizi habari za kufungwa kwa kiwanda cha Dangote eti, sababu ya kushindwa kukiendesha kutokana na gharama za uendeshaji kuwa kubwa sio za kweli hata kidogo. Taarifa sahihi na zenye ukweli ni kwamba, kiwanda cha Dangote kipo kwenye matengenezo makubwa ya mitambo yake baada ya kutokea hitilafu za kiufundi. Acheni upotoshaji usiokuwa na tija!DK. KAFUMU on DANGOTE (A must read).
"Hii ni shida yetu watanzania wote, wataalamu, viongozi wa serikali na pia wanasiasa. Kwanza tuko SLOW, sijui tunaogopa kutoa maamuzi? Sijui ni taaluma duni? Sijui ni nini? Mwekezaji DANGOTE, tuliahidi kumpa malighafi ya LIMESTONE kwa ajili ya kuzalisha SARUJI kwa unafuu mkubwa; tuliahidi kumpa ardhi kwa bei nafuu au bure; tuliahidi kumpa gesi nyingi tena kwa bei nafuu; tuliahidi kumpa makaa ya mawe kwa wingi tena kwa bei nafuu; tuliahidi kumpa nafuu ya kodi na mengine mengi; mazingira yaliwavutia (Dangote na wenzake) sana. Dangote wakavutika wakaja. Mimi (Dk. Kafumu) nikiwa Kamishna wa Madini wakati huo nilitimiza wajibu wangu wa kuwapa leseni ya utafutaji na uchimbaji wa LIMESTONE kadri ilivyohitajika. Nawashukuru sana STAMICO walinisikiliza na kiwanda kijajengwa. Awamu ya tano (ya JPM) imekuja na mambo mapya, ahadi zingine (kwa wawekezaji) zinasuasua, sijui ni nini! Prof Mjebda (anamtaja Prof. mwingine kwenye Whatsup Group) anaweza kutuelimisha hapa. Kiwanda hiki kikubwa kikiimarika; manufaa ni makubwa ikiwa ni pamoja na nchi kupata kodi za kutosha; ajira zitapatikana; sekta ya majenzi (ujenzi) itaimarika; uchumi utaimarika. Ni muhimu tuwahamasishe (wawekezaji) tuangalie matokeo ya muda mrefu na siyo haya ya haraka. Kiwanda kikifungwa shida ni yetu, hebu tuwe na mioyo ya kibiashara siyo siasa za uzalendo uchwara. Samahani sana "
Dkt. Dalali Kafumu,
Kamishna Mstaafu wa Madini (Tanzania),
Mbunge wa Igunga (wa sasa),
Kada wa CCM.
[HASHTAG]#Note[/HASHTAG]; Nimehariri lugha kwenye maoni hayo ya kitaalamu ya Dk. Kafumu. Tujadili seriously.
JSM.
Mkuu watu wanacheza na uchumi wa nchi, hawajui kuna madhara mabaya sana.Nadhani wewe ni "chicken head" usiyefikiri as a normal human being!
Ivi wewe na wenzako hii posho mnayopata(7000) inasababisha mnasaliti ndugu zenu wanaokufa njaa uko vijijini, kwa nini nyeupe msiseme ni nyeupe na nyeusi ni nyeusi? Mmelishwa unga wa ndere? Ni nani atuletee unga wa rutuba tuiponye nchi hii dhidi ya vijana walolishwa unga wa ndere?Mpiga dili huyo akafie mbele, sisi tunataka Kodi zetu kwa ajili ya maendeleo ya watu wetu!
Kwa ufupi wawekezaji wa aina hii ni wazembe. Naamini angekuwa anawekeza ktk nchi serious, hata kama angeahidiwa hayo yote lazima angekataa. Huwezi kufanya investment ya mabilioni ya pesa halafu ukapewa ahadi nje ya written law, nawe ukakubali. Huyo investor ana mwanasheria au anapwaga tu kwa ahadi na kushikana mikono na kila rais aliyeko madarakani? Nahisi inachangiwa na asili ya utajili wao.Unaweza kweli ukawa serious kujadili, lakini bahati mbaya kipande hiki cha observation ya Dk Kafumu (nilivyoelewa mimi) imechotwa kutoka kwenye mjadala kwenye group lake la whatsap, hivyo hakuna mtiririko wa yote aliyonena huko, lakini angalau kipande hiki kinajaribu kuonyesha kuna tatizo mahali fulani, na kwa uelewa wangu ninaona kama Dk Kafumu ana expose mgongano uliopo katika ku-treat investors. Kipande cha andishi la Dk Kafumu linatoa angalizo kwamba sisi ni double standard kwa wawekezaji!