mku
Member
- Mar 27, 2011
- 88
- 9
Ndugu wanajamvini!
Napenda kumfananinisha Dr. Kafumu na mwindaji aliyeenda kutafuta kitoweo na baada ya kupata kitoweo kalejea nyumbani. Zamani enzi zile za gari la moshi la kuchochea kwa kuni, na zile enzi za mashirika ya usafiri kama ya KIRETCO, AMTCO nakadharika kijana au baba mwenye mji ulikuwa ukitoka nyumbani asubuhi na mbwa wako kama sio kumi basi kumi na tano na mishale mikali yenye sumu kwenda kuwinda. Siku ikiwa njema na ukaja na swala nyumbani au kama sio pofu basi watu walikuwa wanasimama njiani wanakushangilia kama mwindaji hodari na wanakupa sifa kedekede. Sherehe ilikuwa inafanyika nyumbai kwako maana ndo hapo utakapolia nyama yako na nyama inaakuwa vizuri kama mnakula na watu wa nyumbani ukiwa unasimulia jinsi ilivyokuwa. Ni jambo liliwazi kuwa wana Igunga wamelamba dume maana kitendo cha CCM kumfanyia sherehe ya kumkaribisha na kumpongeza Kafumu dar ni kiashiria kuwa alienda kuwinda kura na kazipata na kaja kulia nyumbai kwake na ndugu na jamaa. Alienda kuwinda porini(Igunga) na karudi na nyama(Ubunge) kwenye bega nyumbani(Dar)..
Hakuna mantiki ya kufanya sherehe na kutumia pesa mingi dar na huku wananchi waliokupa kura leo pale choma chankore hawana maji na wanalia na shida zao....Ila mwishowe huwa nawaza kuwa ngoja wakome maana hawataki kubadirika ila huwa siamini hili maana najua huwa wanalazimisha kwa njia moja au nyingine......Nawasilisha