Dkt. Hastings Kamuzu Banda: Haya ni kweli kumhusu?

Kumekuwa na habari nyingi mtaani kuwa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Malawi Dokta Hasting Kamuzu Banda alihasiwa ili aweze kuwa Daktari wa Malikia Elizabeth wa II? Je fununu hizi zina ukweli kiasi gani?

Pia kuna habari nyingine zinadai huyu jamaa hakuwahi kupata mtoto enzi za Maisha yake Duniani, je nayo ni kweli?

Wabobezi wa Historia na Intelijensia njooni mtuweke sawa. Karibuni
 
Kumekuwa na habari nyingi mtaani kuwa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Malawi Dokta Hasting Kamuzu Banda alihasiwa ili aweze kuwa Daktari wa Malikia Elizabeth wa II? Je fununu hizi zina ukweli kiasi gani?

Pia kuna habari nyingine zinadai huyu jamaa hakuwahi kupata mtoto enzi za Maisha yake Duniani, je nayo ni kweli?

Wabobezi wa Historia na Intelijensia njooni mtuweke sawa. Karibuni
Ata mm nilisikia alihasiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumekuwa na habari nyingi mtaani kuwa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Malawi Dokta Hasting Kamuzu Banda alihasiwa ili aweze kuwa Daktari wa Malikia Elizabeth wa II? Je fununu hizi zina ukweli kiasi gani?

Pia kuna habari nyingine zinadai huyu jamaa hakuwahi kupata mtoto enzi za Maisha yake Duniani, je nayo ni kweli?

Wabobezi wa Historia na Intelijensia njooni mtuweke sawa. Karibuni
Kamuzu Banda alizaliwa karibu na Kasungu, Malawi iliyokuwa wakati ule sehemu ya eneo lindwa la Afrika ya Kati ya Kiingereza (baadaye Nyasaland). Wazazi walikuwa Mphonongo Banda na Akupingamnyama Phiri. Tarehe ya kuzaliwa haijulikani ilhali wakati ule hakukuwa na utaratibu wa kuandikisha watu. Alikubali baadaye matokeo ya utafiti wa rafiki kutoka Marekani aliyekadiria ya kwamba alizaliwa mnamo Machi au Aprili 1898.

Jina lake Kamuzu lamaanisha "mzizi mdogo" kwa sababu alizaliwa baada ya mama yake kutumia dawa ya mitishamba kwa kusudi la kupata mimba. Banda lilikuwa jina la baba yake, na jina la Hastings alijiongezea baada ya kubatizwa kwa heshima ya mmisionari mmoja kutoka Uskoti aliyependwa naye.

Mnamo 1915–1916 Banda aliondoka kwao akisafiri kwanza Rhodesia ya Kusini (sasa Zimbabwe) na mwaka 1917 aliendelea hadi Johannesburg katika Afrika Kusini alipopata kazi kwenye migodi ya Witwatersrand. Wakati ule alijiunga na kanisa la African Methodist Episcopal Church na hapo askofu wa kanisa lile aliona kipaji chake akamkubali kwa masomo. Mwaka 1925 Banda aliondoka kwenda Marekani.

Young_Dr_Banda.jpg


Alisoma kwa miaka 3 kwenye Wilberforce Institute iliyokuwa chuo cha Kanisa la A.M.E. akaendelea kwa miaka 2 Bloomington, Indiana, kwa maandalizi ya masomo ya tiba.

Kutoka huko alikaribishwa kuhamia Chuo Kikuu cha Chicago alipokuwa msaidizi wa profesa wa lugha aliyetunga kamusi na sarufi ya lugha ya Chichewa, akajisomea historia akamaliza bachelor. Kwa msaada wa wafadhili aliweza kuendelea kusoma elimu ya tiba kwenye Meharry Medical College huko Tennessee alipomaliza mwaka 1937.

Kwa kurudi kwao kama tabibu alihitaji mtihani kufuatana na mfumo wa Uingereza, hivyo alihamia Chuo Kikuu cha Edinburgh alipopokea vyeti vya tiba na upasuaji mwaka 1941. Alianza kufanya kazi ya tabibu huko Uingereza katika miaka 1941-1951.

Mwaka 1946 Banda aliombwa kuhudhuria mkutano wa Pan-African Congress mjini Manchester (15-19 Oktoba 1945) kama mwakilishi wa Nyasaland. Tangu mkutano huu alishiriki katika siasa. Alijulikana kwake Nyasaland kama Mwafrika mwenye elimu ya juu zaidi kutoka nchi yake.

Baada ya miaka kadhaa huko Gold Coast (Ghana) aliombwa na wanasiasa Waafrika arudi Nyasaland akafika mwaka 1958. Kwenye mkutano wa chama cha Nyasaland African Congress (NAC) alichaguliwa mara moja kuwa kiongozi. Alikuta nchi yake Nyasaland kuwa sehemu ya Shirikisho la Afrika ya Kati ambako walowezi wa Rhodesia ya Kusini walikuwa na athira kubwa na kuendeleza ubaguzi wa rangi. Banda alipinga kuwepo kwa shirikisho hili.

Alizunguka nchini akiwahutubia watu na kudai uhuru wa Unyasa. Kutokana na muda mrefu wa kukaa mbali na nyumbani alihitaji wafasiri maana alishindwa mwanzoni kutumia Lugha mama yake.

Wananchi wengi walimfuata na hadi mwaka 1959 harakati ya uhuru iliongezeka kiasi kwamba serikali ilitangaza hali ya dharura. Banda alikamatwa na kuwekwa jela kwa miezi 11. Chama cha NAC kilipigwa marufuku lakini wanachama nje ya gereza waliunda badala yake chama cha "Malawi Congress Party" (MCP) na kumtangaza Banda kuwa mwenyekiti ingawa bado alikaa jela.

Wakati huo wanasiasa katika Uingereza walianza kukazia uhuru kwa makoloni yake. Kwa hiyo Banda aliachishwa gerezani kwenye Aprili 1960 akapelekwa London kwa majadiliano kuhusu uhuru wa nchi.

Baada ya uchaguzi wa Agosti 1961 ulioleta kura nyingi kwa chama chake Banda alikuwa waziri wa ardhi na serikali za mitaa. Tarehe 1 Februari 1963 alikuwa waziri mkuu wa Nyasaland.

Mwaka 1964 aliongoza nchi kwenye uhuru kamili. Banda aliamua kubadilisha jina kutoka Nyasaland kuwa "Malawi".

Jomo_Kenyatta_escorts_Dr_Banda_at_the_end_of_the_latters_visit.jpg


Wakati wa Agosti na Septemba 1964 Banda alijikuta mara ya kwanza mbele ya upinzani wa mawaziri wengi. Walilalamika juu ya Banda kutoshauriana nao akifanya maazimio, kuendelea kwa uhusiano wa kidiplomasia na Afrika Kusini (iliyofuata siasa ya apartheid) na Ureno iliyotawala makoloni ya Msumbiji n.k.

Banda aliachisha mawaziri watatu tarehe 7 Septemba. Mawaziri wengine waliwafuata wakijiuzulu. Maandamano nchini yalifuata na wafuasi wa Banda walipigana na hao wa mawaziri. Mawaziri wengi waliondoka nchini. Wawili walijaribu kuingia pamoja na wanamgambo wenye silaha kutoka Msumbiji lakini walishindwa.

Mwaka 1966 Malawi ikawa jamhuri na Hastings Banda rais wake wa kwanza na chama cha MCP kilikuwa chama pekee cha kisiasa.

Mwaka 1970 alitangazwa kuwa mwenyekiti kwa maisha yote wa chama cha MCP. Hatua hii ilifuatwa na Banda kuwa rais wa taifa kwa maisha yake yote. Umoja wa vijana wa chama cha MCP ulihakikisha kukomeshwa kwa kila upinzani nchini pamoja na vyombo vya dola.

Wote walipaswa kumtaja kwa jina la "His Excellency the Life President Ngwazi Dr. H. Kamuzu Banda" kwa kuongeza "Ngwazi" ambalo ni neno la Chichewa lenye maana ya "shujaa". Kutamka maneno ya ukosoaji dhidi ya rais ilikuwa hatari.

Alitangaza mambo mengi kuwa marufuku Malawi, kwa mfano wanawake kuvaa suruali, kuonyesha magoti, wanaume kuwa na nywele ndefu au suruali fupi. Makanisa yalipaswa kutafuta kibali cha serikali, Mashahidi wa Yehova walipigwa marufuku. Wamalawi wenye asili ya Uhindi walipaswa kuachana na nyumba zao na kuhamia maeneo ya pekee katika miji. Magazeti, vitabu na filamu vilichunguliwa na wakaguzi wa serikali.

Banda alifaulu kutunza amani nchini wakati wa utawala wake lakini aliongoza kama dikteta. Mwaka 1983 mawaziri watatu wa serikali yake waliuawa. Banda mwenyewe alianzisha majadiliano kuhusu kukubali vyama vingi nchini. Mawaziri watatu waliunga mkono hoja hii na mara moja rais aliachisha baraza lote la mawaziri akaita mkutano wa bunge na kuachisha wabunge wote. Mawaziri watatu walifungwa katika chumba bungeni na kupigwa. Mbunge mmoja aliingia katika chumba hiki na kuwaona wakiteswa alikamatwa pamoja nao. Wote wanne walipatikana wamekufa katika gari la Peugeot lililopinduka. Serikali ilizuia kufunguliwa kwa majeneza wakati na mazishi yaliyotokea usiku. Walitangazwa kuwa wahanga wa ajali lakini baadaye ilijulikana waliuawa kwa kupiga misumari katika vichwa vyao kabla ya kuweka maiti katika gari na kulisukuma katika korongo.

Hadi mnamo 1990 nchi za magharibi zilisaidia au angalau kuvumilia serikali ya Banda kwa sababu alikuwa mpinzani wa ukomunisti, pia kati ya nchi chache za Afrika zilizoendelea kuwa na uhusiano na Afrika Kusini. Lakini kuporomoka kwa ukomunisti kulisababisha badiliko. Wafadhili wa miradi ya maendeleo walidai mabadiliko ya kuheshimu haki za binadamu. Serikali ya Uingereza ilisimamisha usaidizi wote kwa Malawi.

Katika Machi 1992 maaskofu Wakatoliki wa Malawi walitunga waraka kwa Wakristo walipotamka ukosoaji wa Banda na serikali. Wanafunzi wa vyuo walichukua upande wa maaskofu na kuandamana. Vyuo vikafungwa.

Hadi Oktoba 1992 Banda alipaswa kukubali kura ya wananchi kuhusu swali la kukubali vyama vingi. Kura hii ilileta asilimia 64 kwa ajili ya demokrasia ya vyama vingi. Mwaka huohuo halmashauri mpya ilitangaza katiba mpya na kuondoa "urais wa maisha". Jeshi la Malawi lilivamia vituo vya Umoja wa Vijana wa MCP na kukamata silaha zote zilizowahi kupewa kama mkono wa utawala wa chama. Katika uchaguzi wa mwaka 1994 Banda aligombea tena urais lakini alishindwa na Bakili Muluzi. Chama kipya cha Muluzi kilipata wabunge wengi.

Mwaka 1995 Banda alikamatwa na kupelekwa mahakamani kwa mashtaka ya kuhusika katika mauaji ya mawaziri ya mwaka 1983. Aliachishwa kutokana na upungufu wa ushahidi.

Banda aliendelea kuwaangalia Wamalawi kama "watoto wa siasa" akatabiri ya kwamba wanahitaji "mkono wa chuma".

Mwaka 1997 aliugua akapelekwa kwa matibabu Afrika Kusini alipofariki tarehe 25 Novemba 1997 akiwa na umri wa miaka 99 hivi.
 
Kumekuwa na habari nyingi mtaani kuwa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Malawi Dokta Hasting Kamuzu Banda alihasiwa ili aweze kuwa Daktari wa Malikia Elizabeth wa II? Je fununu hizi zina ukweli kiasi gani?

Pia kuna habari nyingine zinadai huyu jamaa hakuwahi kupata mtoto enzi za Maisha yake Duniani, je nayo ni kweli?

Wabobezi wa Historia na Intelijensia njooni mtuweke sawa. Karibuni
Yaani unaamini daktari mwafrica amtibu malkia kwa wakati huo? practically impossible!
 
Back
Top Bottom