Dr. Emerson Mnangagwa aliponzwa na waganga wa kienyeji

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,606
696,708
849x493q70sally-mugabe-emmerson.jpg
kwa wasiomfahamu huyu bwana ndie aliyekuwa makamu wa rais wa Zimbabwe mpaka juzi alipofutwa kazi na rais Mzee kuliko wote... Pengine dunia nzima mzee babu Robert Mugabe
Intelijensia ya Mugabe kali lakini pia tunaweza kusema ni ya aina yake na ya kushangaza pia kama si kuchekesha... Ana mapandikizi informers mpaka kwa matabibu wa nguvu za giza...!!!
Makamu wa rais baada ya kusubiri sana babu afe ama walau ang'atuke na kumwachia madaraka makubwa kama alivyofanya Mwl. J. K. Nyerere mwaka 1984 na kumwachia Mzee Mwinyi....! Akaona hakuna hata dalili za kufa ama kuachia madaraka... Waswahili wana msemo wao.... Ngoja ngoja yaumiza tumbo!
Dr Mnangagwa akachoka kusubiri, akashindwa kabisa kungoja, akajiuliza hiki kikongwe. Kimekula nini mpaka katika umri huu wa miaka 93 hakifi tuu!? ... Akaamua apate jibu lake kupitia nguvu za giza, wataalam wa kupuliza walau wamsaidie kumwambia ni lini babu anaweza ku rest in piece ⚰... Ni katika kuhangaika huko kumbe kati yao kuna mapandikizi ama Mzee babu ni mteja wao.... Wakaenda kumsemea kwa siri, wakamwambia mzee kama hujui jua sasa...! msaidizi wako mkuu kazini anatuuliza tumwambie UTAKUFA LINI!??? Yani hawakutaka kuzunguka walienda direct moja kwa moja....
Khaa mzee babu akaona hii ni treason kabisa! Neno la kiingereza hili ile lugha ya malkia Queen Elizabeth wa ngapi sijui pale Birmingham Uscotsh.. Tamka uskotishi... Yaani msaidizi wangu ninayemuamini ananichulia kifo!? Akaiona hatari kubwa iliyo mbele yake...
Haikuchukua masaa 24, akamfuta kazi mazima.... Sasa hivi Makamu wa rais wa Zimbabwe bwana Emarsson Mnangagwa yuko South Africa kwa wazulu, kakimbilia huko... MUGABE HATAKAGI UPUUZI KABISA
faff41d521dccea196b20633aa2143cc--african-tribes-african-art.jpg
 
Ingekuwa mugabe nawaambia mapandikizi wangu hilo jibu litoeni uhai badala ya kulivua wadhifa
 
And the worst part of it, kafukuzwa bora angejipndoa mwenyewe hapo angeeleweka

Mara nyingi Guerilla leader baada ya ushindi wale macomrade wake wa karibu sio watakaomrithi. Wengi hugeuka maadui. Wanaobaki, hutumika tu kumwezesha atawale vizuri. Wakitamani madaraka yake nao hugeuka maadui pale pale. Inasikitisha kuwa wanapopigania "uhuru" wa mataifa yao "mashujaa hao", wanaonesha taswira ya upendo, utu wema, wasio na ubinafsi, na mengi mengine yenye mvuto. Wakipata utawala hali hugeuka na wanakuwa tofauti sana. Inasikitisha sana "briliant marxist revolutionaries wa miaka ys 60" , waliokuja kutawala mataifa yao miongoni mwao wamekuwa "political bourgeoisie'" wa miaka ya 80 na 90 na 2000. Wamengangania madarakani, ni matajiri
 
Mnangagwa ni kama mamba ambae alikuwa hajitambui na pia haelewi ujazo wa maji na kina cha mto alokuwamo.

Ni sawa na mtu ambae hujawahi kuishi karibu na mlima lakini unaanza kujenga Imani potofu kuhusu ule mlima.

Lakini hapo hapo kandokando ya mlima wapo watu wanaishi na kukata kuni na kuendelea na shughuli zao mbalimbali kama kawaida.

Lakini cha kushangaza ni mlima huohuo kuanza kujenga imani potofu juu yake wenyewe na watu kutoka pande zingine wakaanza kujenga imani potofu juu ya mlima huohuo.

Hivyo basi Emerson Mnangagwa alikuwa ni kama mamba na pia alikuwa ni kama mlima.

Lakini hakuna siku hata moja milima inaweza kukutana na hivyo ndivyo jinsi ilivyotokea kwamba mzee Bob ukiwa ni mlima mwingine ulio mbali, akaona amwondoe Emerson Mnangagwa ambae wameshiriki wote kupigania uhuru wa Zimbabwe.

Mnangagwa ni mmoja wa watu hatari kabisa kuwahi kutokea kwenye serikali ya mzee Bob.

Alipoondolewa Joyce Mujuru mwaka 2014 Mnangagwa akapewa umakamu wa raisi kupitia mkono wa idara maalum iiltwayo "Lacoste", idara inayoshirikisha makachero na majasusi wote ambao wanaitwa "the invisible hand".

Lakini ni haohao "Lacoste" ambao wamemuondoa Mnangagwa kwa ajili ya kumpisha mtu mwingine ambae atajulikana baadae.

Kama unafuatilia hii power struggle ndani ya serikali ya mzee Jongwe basi bila shaka utakuwa unakumbuka jina la profesa Jonathan Moyo.
 
Mara nyingi Guerilla leader baada ya ushindi wale macomrade wake wa karibu sio watakaomrithi. Wengi hugeuka maadui. Wanaobaki, hutumika tu kumwezesha atawale vizuri. Wakitamani madaraka yake nao hugeuka maadui pale pale. Inasikitisha kuwa wanapopigania "uhuru" wa mataifa yao "mashujaa hao", wanaonesha taswira ya upendo, utu wema, wasio na ubinafsi, na mengi mengine yenye mvuto. Wakipata utawala hali hugeuka na wanakuwa tofauti sana. Inasikitisha sana "briliant marxist revolutionaries wa miaka ys 60" , waliokuja kutawala mataifa yao miongoni mwao wamekuwa "political bourgeoisie'" wa miaka ya 80 na 90 na 2000. Wamengangania madarakani, ni matajiri
Watu wanapigania matumbo yao hasa Africa
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom