beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Rais wa Jamuhuri ya Demokrasia ya Congo, Félix Tshisekedi, aamua kuweka mpango wa kuvunja Serikali ya Muungano na wafuasi wa aliyekuwa rais wa taifa hilo, Joseph Kabila.
Katika hotuba yake kupitia matangazo ya televisheni Jumapili , bwana Tshisekedi alisema atachagua maofisa wapya kuunda Baraza jipya kwani Bunge la sasa lina wafuasi wengi wa Kabila ambao hawamsikilizi.
Alisema alikuwa amejiandaa kuvunja bunge lote kama kuna ulazima.
Takribani miaka miwili sasa, DRC iliunda serikali ya muungano, baina ya chama cha kabila na chama cha rais mpya Tshisekedi, vyama viwili ambavyo vilipingana kwa kipindi cha muda mrefu vilikubaliana kufanya kazi kwa pamoja, lakini baada ya siku chache tu mvutano ulianza kati ya vyama hivyo.
Baadhi ya wafuasi wa chama cha Tshisekedi walianza kususia ushirikiano huu, huku wakiwashutumu wafuasi wa chama cha kabila kumzuia rais mpya kutekeleza ahadi zake.
Hivi karibuni , katibu mkuu wa UN na kiongozi wa Umoja wa Afrika walieleza wasiwasi wao juu ya mvutano wa kisiasa wa pande zote mbili.
Katika hotuba yake kupitia matangazo ya televisheni Jumapili , bwana Tshisekedi alisema atachagua maofisa wapya kuunda Baraza jipya kwani Bunge la sasa lina wafuasi wengi wa Kabila ambao hawamsikilizi.
Alisema alikuwa amejiandaa kuvunja bunge lote kama kuna ulazima.
Takribani miaka miwili sasa, DRC iliunda serikali ya muungano, baina ya chama cha kabila na chama cha rais mpya Tshisekedi, vyama viwili ambavyo vilipingana kwa kipindi cha muda mrefu vilikubaliana kufanya kazi kwa pamoja, lakini baada ya siku chache tu mvutano ulianza kati ya vyama hivyo.
Baadhi ya wafuasi wa chama cha Tshisekedi walianza kususia ushirikiano huu, huku wakiwashutumu wafuasi wa chama cha kabila kumzuia rais mpya kutekeleza ahadi zake.
Hivi karibuni , katibu mkuu wa UN na kiongozi wa Umoja wa Afrika walieleza wasiwasi wao juu ya mvutano wa kisiasa wa pande zote mbili.