Dr. Chitage: Mashine moja ya CT scan ni sawa na bei ya Toyata shangingi moja!

Unachoshindwa kuelewa ni kuwa nchi hii iliuliwa kifo kibaya sana, toka tulikuwa wasafirishaji wa kwanza wa mazao ya kilimo katika Afrika mpaka kuwa maskini wa kwanza katika Afrika, kwa miaka 24 tuliyafanya hayo tu, ya kuibomoa bomoa nchi. Leo hii tunaona yanayofanyika, leo Tanzania ya Kikwete tuna miradi ya barabara kuliko nchi yoyote ya Afrika Mashariki na kati na pengine ni Afrika nzima. Leo Tanzania hii iliyokuwa hohehahe tuna CT scan na MRI za bure.

Leo Tanzania hii iliyokuwa maskini wa mwisho duniani tuna akiba ya chakula. Leo Tanzania hii hii tuliokuwa tunaletewa msaada mpaka unga wa uji (wa manjano) leo tuna uwezo wa kuuza mahindi nje ya nchi.

Nakuhisi ni mtoto mdogo sana na hujui tulipotoka na ndio maana huwezi kuthamini leo tuko wapi.

kubomoa rahisi kuliko kujenga. Nyumba inayobomolewa kwa siku moja inachukuwa mwaka kuijenga. Sasa fikiri nchi iliyobomolewa kwa miaka 24 itakuchukuwa miaka mingapi kuijenga? ukipata jibu ukubali kuwa, Kikwete anafanya miujiza kwa jinsi anavyotuletea maendeleao ya haraka haraka na ya rekodi katika kila nyanja. Ukweli ubaki kuwa ukweli na tuwache uongo.

Wengi roho zinzwauma kwanini leo huyu aweze waliposhindwa tunaifkiri kuwa ni watakatifu. Hakuna zaidi ya hilo, ni roho za kichawi tu.

Tuongelee afya kabla ya Kikwete na leo. Takwimu tu zinawasuta.

zomba, unaongea vizuri kuliko Wassira!

Ninavyojua mimi huko nyuma tulikuwa na ATC na ilikuwa na ndege zinaenda nchi za nje, elimu ilikuwa bure, bure, bure kabisa, huduma za afya zilikuwa bure, 90% ya watanzania walikuwa wanajuwa kusoma na kuandika, tulikuwa na viwanda ya kubangua korosho, tulikuwa na Tanganyika Packers, General Tyre, National Milling, Ranchi za taifa, Mwatex, Mutex, Machine Tools, Tanneries, usafiri wa reli na kubwa zaidi hatukuwa na mashimo makubwa kama yale ya Bulyanhulu, au Nyamongo

Pili, kama nchi tulijua tunasimama wapi kwenye ulingo wa kimataifa. Mambo ya kukodisha bendera hayakuwepo na mtu alipojaribu kuleta kiburi na mipaka ya nchi yetu tulimtandika vilivyo - kaulize wajukuu wa Idd Amin. Sasa hivi wazamiaji wanakuja hadi Dodoma hakuna mtu wa kuwazuia, Kibondo watu wanachwapa kila siku na watu toka nchi jirani (fedheha).

Tatu, kwenye red: Sijui mwenzetu wewe unapata data toka wapi ila kaa ukijua kwa sasa Tanzania ni ya tatu duniani kwa kupata misaada!
 
By Matern Kayera and Sharifa Kalokola
Looking at the high tech buildings and equipment at Muhimbili National Hospital, it is hard to believe
...

Tafuteni ukweli utawaweka huru, huu ni wakati wa nani? soma zaidi: Muhimbili
zomba sasa itimimisho lako nini au wewe unaona ni sawa serikali kuendelea ku-invest pesa nyingi za walipa kodi kwa kununua magari ya kifahari au ifikie wakati hata watumie Land Cruiser (hard top) gari za bei nafuu lakini unapita nalo popote katika mazingira ya nchi yetu na pesa zingine zielekezwe katika maendeleo ya taifa letu.
Na ifike mahali tujadili ubora na uozo wa taifa letu bila kuonyesha mapenzi yetu ya moja kwa moja aidha ki-udini ama ki itikadi za vyama.
 
Last edited by a moderator:
Nani alioziharibu?

Kuna mashine za kupima virusi vya vvu zilipelekwa Tumbi hospital, na zikamiminiwa maji ili ziharibike eti kwa sababu kwanini kachaguliwa fulani ndio akafundishwe hizo mashine. Uliza hili Tumbi, linajulikana.

Sasa kama vifaa vinaletwa na haohao wanafanyiana roho mbaya mpaka kuviharibu eti kwa sababu mtu hakuchaguliwa yeye kusomeshwa hizo mashine, halafu mulaumu Kikwete. Wacheni hizo.

Kikwete kwenye sekta ya Afya kafanya kuliko yeyote wa kabla yake na takwimu za kungezeka kwa life span yetu kwa miaka 5 kwa kipindi chake tu kinathibitisha hilo. Wacheni kuwa wanafik.

Huyu daktari kaja hapa anadanganya na nyinyi mnakubali tu, hamchukui hata dakika moja kuuthamini ukweli.

Nimewaletea data hapo za mashine za CT scan, zinaonesha kwa uchahe kama hauna $ 1,000,000/= (million moja) huwezi kupata CT scan ikafanya kazi ipasavyo, labda uinunuwe uje kuiweka urembo.

Mimi nipo apollo hospital hapa hyderabad, india namuuguza b mkubwa wangu, kaka kukosekana kwa Ct scan mashine ni aibu kwa serikali maana hapa nilipo kila block Ct scan yake, na apollo ni hospital binafsi sasa serikali inayokusanya kodi kibao itashindwa nini kununua hizo mashine. Hospitali za wenzetu ni Health cities, I mean unakuta hospital kubwa mara 5 ya muhimbili na kuna blocks za kutosha, vipimo, drs na nesi kama utitiri hadi unajiuliza hawa watu wanalipwaje mbona wapo wengi sana. Yaani tumekosa imani kabisa na serikali ya ****** kiasi kwamba ni bora ndugu tuchangishane kutibia watu.
 
Nikiangalia maelezo na utetezi wa pande zote mbili, ninachoweza kujifunza ni kuwa wote wako sahihi. Kwa upande mmoja akina Zomba na Macos wako sahihi kuwa serikali imefanya mengi lakini uwezo wa kufanya mengi zaidi upo, tatizo la serikali ni kutochagua vipaumbele kwa hali, mahali na wakati ufaao. Kulikuwa na haja gani ya "kusherehekea" uhuru na kununua mashangingi kwa kutumia mamilioni ya shilingi huku tukiwa shida kama tulizonazo?

Kwa upande wa pili, ule msemo wa mjenga nchi na mvunja nchi ni mwananchi. Wananchi (kwa hapa madaktari na wengineo), wanafanya uharibifu wa makusudi wa mali za umma kwa sababu ya maslahi binafsi au chuki. Dakatari anaharibu kifaa au hatoai huduma ipasavyo kwa sababu akimpeleka mgonjwa hospitali binafsi kule anapatiwa "mshiko". Mwalimu hasomeshi ipasavyo akiwa shuleni anawaagiza watoto waende kwenye twisheni yake, dereva anang'ola kipuli cha gari na kukiuza bila kujali kuwa gari hilo ni la umma na linawatumikia wananchi wenzake. Mtengeneza barabara anauza kokoto, nondo na saruji na kuiacha barabara baada ya mwaka mmoja imekufa...na mifano mingi tu. Halafu watu hawa hawa wanamlaumu Kikwete. Aibu gani!

Watanzania wenzangu, tuache kulalamika hata kwa yale ambayo sisi wenyewe tumeyasababisha. Kama ingekuwa kulalamika tu kunatatua shida zetu, nchi hii ingekwisha fika mbali kwa kulalamika. Viongozi, tuache mara moja kufikiria matumbo yetu na anasa zetu wakati tunaowaongoza wanakufa kwa umasikini wa kutupwa. Tusichape usingizi kudhani kuwa mabadiliko yatashuka toka mbinguni au kubadilisha uongozi au chama ndio suluhisho pekee. Tubadilishe nafsi zetu.
 
Mimi nipo apollo hospital hapa hyderabad, india namuuguza b mkubwa wangu, kaka kukosekana kwa Ct scan mashine ni aibu kwa serikali maana hapa nilipo kila block Ct scan yake, na apollo ni hospital binafsi sasa serikali inayokusanya kodi kibao itashindwa nini kununua hizo mashine. Hospitali za wenzetu ni Health cities, I mean unakuta hospital kubwa mara 5 ya muhimbili na kuna blocks za kutosha, vipimo, drs na nesi kama utitiri hadi unajiuliza hawa watu wanalipwaje mbona wapo wengi sana. Yaani tumekosa imani kabisa na serikali ya ****** kiasi kwamba ni bora ndugu tuchangishane kutibia watu.

Naona unashindwa kuelewa kuwa CY scan hata mahospitali binafsi Tanzania zipo. CT scan zilizopo hospitali zinaharibiwa makusudi na hao wataalaam wa CT scan ili watu waende private hospital wao watengeneza fedha zaidi. Hawajali maslahi ya Mtanzania hao ndio watataam wa Tanzania, usisikie wanakuja hapa kudai uongo kuwa wanataka huduma bora kwa Watanzania. Katika madai yao 12 hakuna hata moja linalohusiana na mlalahoi wa Kitanzania. Yote ni yao binafsi hawa ni wanafiki, wazandik na waongo. Hawa kama mimi ni Kikwete, ni kutandika risasi tu, hakuna msamaha.
 
Mkuu FJM unafanya kazi kubwa kujaribu kumuelewesha zomba. Pamoja na hizo juhudi, tafadhali tazama avatar yake na signature yake. Ndipo utatambua kuwa huyu ni kijakazi wa kurugenzi ya mawasiliano ikulu. Anapoteza muda kupotosha mambo.
 
Last edited by a moderator:
Hapo bado hujapata CT scan, wachilia mbali chumba, utaalaam (mafunzo), "consumables".

Huyo dokta alikuwa anaota.


Hata kama ingekuwa inagharimu matrilion, hamna sababu ya kukosa vifaa kama hivi katika nchi hii. Vipaumbele vinakusumbua weye janga la kitaifa, hata ukijitetea kivipi, you have failed.
 
zomba sasa itimimisho lako nini au wewe unaona ni sawa serikali kuendelea ku-invest pesa nyingi za walipa kodi kwa kununua magari ya kifahari au ifikie wakati hata watumie Land Cruiser (hard top) gari za bei nafuu lakini unapita nalo popote katika mazingira ya nchi yetu na pesa zingine zielekezwe katika maendeleo ya taifa letu.
Na ifike mahali tujadili ubora na uozo wa taifa letu bila kuonyesha mapenzi yetu ya moja kwa moja aidha ki-udini ama ki itikadi za vyama.

Hayo yameongelewa na uamuzi umetolewa juzi bungeni rasmi, au hujamsikia Pinda akisema kuanzia sasa gari za Serikali zisizidi cc 3,000.

Lakini tusidangaye kuwa shangingi ni sawa na CT scan. Tena CT scan siyo kama haijanunuliwa, imeletwa na waulize hao madaktari waliopo hospitali kwanini yao haifanyi kazi za private hospital zinafanya kazi? utapata jibu.
 
Kama wewe UAMSHO?

CT scan siyo bei ya shangingi moja ni uongo uliopitwa na wakati. Siku hizi una google tu unapata bei, naona aliyeleta huu uongo alikuwa hajui kama Kikwete kaeneza mitandao ya bei rahisi mpaka vijijini. Siku hizi hatudanganyani, tuna google tu.
 
Huyo Daktari ni muongo wa kutupwa, siku hizi kila kitu kiko wazi, gharama ya CT scan hii hapa:

the compute tomography machine costs depends upon the technology systems
siemens ------------------200000 usd approx
toshiba -------------------180000 usd approx
beckam coulter------------250000 usd approx
sharp------------------------200000 usd approx
ge----------------------------300000 usd approx
phillips ----------------------140000 usd approx



Plus software and technician time. We just got a new siemens definition and its costing 450k (minus software upgrades) so that 200k is really low ball.

There is also the cost of the Tomography room where the unit sits in. It consists of specialty HVAC system that provide perfect humidity and temp.control. Also specail independent electrical circuits to power the equipment, and RAM (radio absorbent)materials for the walls. The cost of a CT room can varry from $250,000- $750,000.
Unakurupuka tu kucopy and paste. Uwe unasoma kabla ya kupaste. Usije ukapaste SMS za MKE wako akikupa mitusi kwa uzoba wako. Si lazima kila post uchangie Kama huna ujualo.
 
Mkuu wao hawana shida wakiumwa wanatibiwa India,South Africa na kwingineko wangekuwa wanatibiwa hapa mwanzo mwisho wangenunua2
 
CT scan siyo bei ya shangingi moja ni uongo uliopitwa na wakati. Siku hizi una google tu unapata bei, naona aliyeleta huu uongo alikuwa hajui kama Kikwete kaeneza mitandao ya bei rahisi mpaka vijijini. Siku hizi hatudanganyani, tuna google tu.
Nasikia kwenye mahakama za kadhi hongo za pilau na juice ya miwa zitakuwa nyingi sana kwajinsi mnavyopenda huo mlo kwi! Kwi! Kwi! Kwi!
 
CT scan siyo bei ya shangingi moja ni uongo uliopitwa na wakati. Siku hizi una google tu unapata bei, naona aliyeleta huu uongo alikuwa hajui kama Kikwete kaeneza mitandao ya bei rahisi mpaka vijijini. Siku hizi hatudanganyani, tuna google tu.
Google jinsi ya kujiua ili utupunguzie janga katika hili Taifa. You are such a douche bag..Pathetic.
 
Sikushangai maana hata waswahili husema ktk msafara wa mamba hata kenge wapo.Watanzania wenzangu hata kwenye mapambano yoyote ya kudai haki wasaliti hawakosekani kama hawa kina Zomba.
Tatizo la serikali hii inashindwa kupanga vipaumbele na badala yake wameegemea kwenye anasa na ubinafsi na ndio maana hata maendeleo yaliyopo hayalingani na maliasili tulizonazo.Hakuna anaebisha kuwa kuna mambo mazuri wamefanya ila hayalingani kabisa na maliasili tulizonazo na hasa ukizingatia sasa tuna miaka 50 ya uhuru.
Hata hivyo ukiona mtu anatetea serikali za aina hii ujue kuna namna moja anavyofaidika na uwepo wa serikali hiyo.
 
huyo daktari ni muongo wa kutupwa, siku hizi kila kitu kiko wazi, gharama ya ct scan hii hapa:

The compute tomography machine costs depends upon the technology systems
siemens ------------------200000 usd approx
toshiba -------------------180000 usd approx
beckam coulter------------250000 usd approx
sharp------------------------200000 usd approx
ge----------------------------300000 usd approx
phillips ----------------------140000 usd approx



plus software and technician time. We just got a new siemens definition and its costing 450k (minus software upgrades) so that 200k is really low ball.

There is also the cost of the tomography room where the unit sits in. It consists of specialty hvac system that provide perfect humidity and temp.control. Also specail independent electrical circuits to power the equipment, and ram (radio absorbent)materials for the walls. The cost of a ct room can varry from $250,000- $750,000.

limbwata
wewe zombe unahitaji maombi maana hakuna unachoona ni sawa na mwanaume aliyelishwa
 
Mheshimiwa mbowe anakwenda nayo sita pale mkutanoni, mbona hatuulizi faida na hasara yake? kadanganya umma kuwa amelirudisha la Serikali, tukabainishiwa kuwa njia ya mnafiki ni fupi kalichukuwa tena.

Na huyu daktari na taaluma yake yote bado anasema uongo. Hapo hujaweka gharama za "consumables", hapo hujaweka gharama za wataalaam wa CT scan, kuwafundisha kuitumia na kuwafundisha mdaktari kujuwa kusoma report za CT Scan.

Msiwe mnadanganywa kijinga na kuwa eti ni daktari tu anaetetea maslahi yake kwa kuuwa wananchi.

Mbona hamsemi kuwa wamepelkwa vijana nje kusomea kufanya opereshen za moyo? mbona hamsemi kuwa kimefunguliwa kituo cha kufundisha madaktari wa moyo? mbona hamsemi kuwa wamepelekwa vijana kusomea magonjwa ya mishipa midogo? mbina hamsemi kuwa kwa sasa tunaweza kufanya opereshen za moyo hapa Tanzania. Na pia mseme kuwa hayo ypte ni wakati wa Kikwete, na pia mseme kuwa mashine za CT scan ziliopo kwa sasa ni wakati wa Kikwete ndio zipo. Mbona hayo yote mnakaa kimya? yalikuwepo kabla ya Kikwete? wacheni unafik, kuweni wakweli.
Una mapenzi ya mke kwa mumewe.Hadithi ndefu ila hoja dhaifu.
Ukweli ni kuwa hali ya vifaa katika hospitali zetu ni mbaya kupita maelezo.Hata kama madaktari wakiwa kazini vifo havitaepukika
 
Naona unashindwa kuelewa kuwa CY scan hata mahospitali binafsi Tanzania zipo. CT scan zilizopo hospitali zinaharibiwa makusudi na hao wataalaam wa CT scan ili watu waende private hospital wao watengeneza fedha zaidi. Hawajali maslahi ya Mtanzania hao ndio watataam wa Tanzania, usisikie wanakuja hapa kudai uongo kuwa wanataka huduma bora kwa Watanzania. Katika madai yao 12 hakuna hata moja linalohusiana na mlalahoi wa Kitanzania. Yote ni yao binafsi hawa ni wanafiki, wazandik na waongo. Hawa kama mimi ni Kikwete, ni kutandika risasi tu, hakuna msamaha.
Wewe ni gamba ambao hamuoni hata
haya kwa huu unyama
 
Sijamuelewa Zomba,anataka tuwe na CT scan au anataka tuendelee kununua mashangingi ambayo mwaka 2010 moja likuwa siyo chini ya $100,000 ukiweka na ushuru na blablah.Mwaka jana mbeya imepoteza mwanafunzi aliyemaliza kidato cha nne kwa kukosa CTscan,kama tunaweza kuhamisha pesa kwenda Uswis kwa nini tuzinunue vifaa muhimu vya hospitali?Tusiangalie jana ilikuwaje,bali leo tunafanyaje?
Viongozi wa Serikali yetu inatakiwa kuwa wakali na walaji pesa za watanzania.Hivi kama wakiondoa sitting allowance za wabunge kwa miezi hii mitatu tutaserve kiasi gani ili tuweze kuboresha hospitali zetu?
Hivi ni haki mbunge tuliyemtuma kutetea maslahi yatu yupo kwa ajili ya maslahi yake zaidi?
Mie nadhani tuangelie hili kwa mapana zaidi tukalijadili badala ya kulaumu madaktari,kuwatukana na hata kuwatesa bila sababu.Tuone ni kwanini tusiwe na huduma bora za afya na siyo bora huduma?
Kwa nini keki ya taifa tuzigawane kwa haki?
Wanasema hivi ukila na kipofu usimshike mkono............
 
Mkuu FJM unafanya kazi kubwa kujaribu kumuelewesha zomba. Pamoja na hizo juhudi, tafadhali tazama avatar yake na signature yake. Ndipo utatambua kuwa huyu ni kijakazi wa kurugenzi ya mawasiliano ikulu. Anapoteza muda kupotosha mambo.

Mwenzako kakubali juu huko kuwa niko sahihi, wewe jee? bado huamini kuwa CT scan ni zaidi maradufu na aliyeleta hii mada kasema uongo, kama ni mleta basi muongo kama ni huyo dokta basi ni muongo. Wewe bado unaamini gharama ya CT scan ni sawa na VX?
 
Back
Top Bottom