Dr Benson Bana apendekeza kamati ya Prof Kabudi ipitie upya mikataba ya ubinafsishaji kampuni ya sigara ( TCC) na NBC

NBC ikiguswa nahakika Mkapa hachomoki na Nyumba za Serikali ikifika zamu yake Mkapa na Jiwe hawachomokiiiii.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
If anything huyu Kabudi na mwenzake Magufuli wanatakiwa waambiwe enough

Hakuna tatizo kutaka kuona mikataba inabadilishwa lakini sio kuja na madai yasiyo na uhalisia kama ilivyokuwa kwenye madini au kutaka kubadilisha strategies za watu ulizozikuta.

Yaani wakati namsikiliza huyu Kabudi leo I almost puked kwenye mapendekezo yake jinsi shirika litakavyoendeshwa, sijashangaa kabisa kumuona na mkurugenzi wa airtel alivyokuwa akipiga mayowe wakati Kabudi anaongea the guy is a disaster na Magufuli nae keshatimua uzalishaji wa ndani vya kutosha kiasi kwamba inabidi aambiwe mjomba huku sio kwako endelea na miundombinu.
 
Eti leo mtu huyo huyo anafanya sherehe ya kupewa hisa tisa kwenye mali ambayo ni ya kwake kwa 100% hii si ajabu tu bali ni aibu pia!!

What? Mimi sijaelewa unachozungumzia! Baada ya kusoma uzi huu ambao kwa bahati mbaya haunitoshelezi nilidhani Prof.amegundua udanganyifu na kampuni inarudidhwa kwa mmiliki halali! Wewe unazungumzia hisa 9%?
 
What? Mimi sijaelewa unachozungumzia! Baada ya kusoma uzi huu ambao kwa bahati mbaya haunitoshelezi nilidhani Prof.amegundua udanganyifu na kampuni inarudidhwa kwa mmiliki halali! Wewe unazungumzia hisa 9%?
Yeah! Eti wakati kampuni iliyokuwa mali yetu kwa asilimia mia tulikuwa na share ya asilimia 40 pekee ila sasa tumeongeza share hadi asilimia 49 na tukapata gawio la faida la asilimia 25 tu!! Siyo kosa lako kutokuelewa bali kweli haieleweki!
 
basi na kamati hiyohiyo ipitie mikataba ya uuzwaji wa zile nyumba za serikali uliofanyika enzi za mh Ben mkapa
Sumaye na Mkapa hawatopona, maana Sumaye alikiri mwenyewe akihojiwa kuwa yeye na Mkapa ndiyo waliuza na Magufuli hahusika.

 
Kwa huo wa Airtel wakati unafanywa nchi haikua na Mawaziri na Mwenyekiti wao wa baraza?

Nani amekamatwa koo kwa huo mkataba wa Airtel au in kurudia kwa kutamka tu kama walivyokua wanatamka wapinzani miaka yote kuwa pale kuna ufisa ,Kuna ubadhirifu n.k?

Tunataka wahusika wakuu walioruhusu ufisadi ukafanyika wachunguze kwanza ili kutenda haki.

Siku hizi tunadili na sijui bodi sijui meneja wakati kuna mawaziri waliokua wamehusika na mafudu mengi wanadunda tu na Mwanasheria wao mkuu wakati huo.
Waliohusika ni wale wale na Chama Kile kile kinachounga mkono kila kinachofanywa na serikali hata kama kinalitia hasara taifa.
Bunge lililopitisha lilikua linaongozwa na Chama kile kile.
Bana sio shujaa mana ni yule yule kazi yake ni kupima upepo na kufuata kama bendera wakati ufisadi unatendeka Bana alikuwepo na Kabudi lakini hawakupiga kelele kuwaunga mkono akina Kafulila,Zito,Lisu, Mnyika ,Mdee na wengine.
Wakati huo Bana alikua anasimama na serikali na Tafiti zake za kuifariji serikali na Chama cha Mapinduzi.
Kwa hiyo hata yeye huyo Bana ni upande wa hao waliodhulumu Taifa hili mana wakati ufisadi unafanyika alikuwepo.

Haki ikitendeka magereza yatajaa watu waliovaaa T-shirt za rangi ya kijani.
.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom