Dr Bashiru: Suala la Umoja ndani ya CCM ni la lazima siyo hiyari, asiyetaka Umoja tutamfukuza mara moja

Sina popote ninapomzuia yoyote kujadili chama chochote, kiwe cdm au hata chama cha walemavu. Hili ni jukwaa huru, yoyote anaweza kujadili chochote, na ukipotosha tutakuambia acha kupotosha na utapata dozi stahiki.

Kwakweli sikukuu imeenda vizuri japo ukata uko palepale. Mwaka tunaungoja huenda hali ikawa afadhali kuliko mwaka huu. Nashukuru kwa salamu ya sikukuu!

Wacha Kamba mkuu wewe uwe na ukata, wacha waseme wengine maana darubini yangu imeona chupa za wine hapo kibao.
 
Wacha Kamba mkuu wewe uwe na ukata, wacha waseme wengine maana darubini yangu imeona chupa za wine hapo kibao.

Situmii vileo. Hali ya ukata ni jambo la kweli wala siongopi.
 
Bashiru ajifunze Siasa toka kwa Dr Jakaya Mrisho Kikwete

Heka heka zote za Lowassa aliweza kwenda nazo mwanzo mwisho bila ya kufukuza wala kusimamisha Uanachama hata mmoja

Siasa za Darasani na za Field ni kama mbingu na Ardhi
Nimeipenda hiyo sentensi ya mwisho.

Ndio maana Kibajaji na Dr Msukuma wanatamba bungeni!
 
Katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru amesema swala la umoja ndani ya chama ni la lazima na mwanachama yoyote atakayekuwa na viashiria vya kutotaka umoja atafukuzwa chamani mara moja.

Ili kuwagundua wabinafsi Dr Bashiru amesema chama kitafuatilia mienendo ya wanachama wake na ikibainika unataka kutugawa Tutakutimua mara moja.

Dr Bashiru ameyasema hayo mjini Bukoba akiwa kwenye ziara ya kuimarisha chama.

Source Star tv habari!
SAWA Tu!
KAMA:
Ni wanachamia wa chama kimoja
Nchi ya chama kimoja
Mnaongozwa na mtu mmoja
Mnaabudu dini moja
Mnaimba wimbo mmoja
Mnavaa rangi moja
Mnafanya kazi moja
Mnasoma kitabu kimoja
Mnakula sahani moja
Hicho lenu moja
Sikio lenu moja
Mdomo wenu mmoja
Kichwa kimoja!

Hakika ni WAMOJA!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru amesema swala la umoja ndani ya chama ni la lazima na mwanachama yoyote atakayekuwa na viashiria vya kutotaka umoja atafukuzwa chamani mara moja.

Ili kuwagundua wabinafsi Dr Bashiru amesema chama kitafuatilia mienendo ya wanachama wake na ikibainika unataka kutugawa Tutakutimua mara moja.

Dr Bashiru ameyasema hayo mjini Bukoba akiwa kwenye ziara ya kuimarisha chama.

Source Star tv habari!
Arejee ziara ya akina kinana, walinyenyekea japo kinafiki, waliomba msamaha kwa watanzania kwamba wawasamehe kwa ya kijinga waliyoyafanya ili kujenga umoja na ilisaidia kiasi fulani.
Huyu nguja tuone hatma ya technic zake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru amesema swala la umoja ndani ya chama ni la lazima na mwanachama yoyote atakayekuwa na viashiria vya kutotaka umoja atafukuzwa chamani mara moja.

Ili kuwagundua wabinafsi Dr Bashiru amesema chama kitafuatilia mienendo ya wanachama wake na ikibainika unataka kutugawa Tutakutimua mara moja.

Dr Bashiru ameyasema hayo mjini Bukoba akiwa kwenye ziara ya kuimarisha chama.

Source Star tv habari!
Sauti yenye mamlaka "hii ndio CCM niliyokua naiota" either you're with us or against us, mambo ya fitina fitina kujiona wewe Ni Bora kuliko wengine piga chini.

Membe, Kinana na wa Baba J aka Ubatizo wa moto Le Caputain wajiandae kisaikolojia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru amesema swala la umoja ndani ya chama ni la lazima na mwanachama yoyote atakayekuwa na viashiria vya kutotaka umoja atafukuzwa chamani mara moja.

Ili kuwagundua wabinafsi Dr Bashiru amesema chama kitafuatilia mienendo ya wanachama wake na ikibainika unataka kutugawa Tutakutimua mara moja.

Dr Bashiru ameyasema hayo mjini Bukoba akiwa kwenye ziara ya kuimarisha chama.

Source Star tv habari!
Udikteta umehamia chamani? Mi nilidhani Katibu Dr. Slaa tu ndiye alikuwa anafukuza wasiotakiwa chamani kumbe hata Dr. Bashiru naye ni wale wale. Hawa PhD wanakuwaga na shida gani? Au fukuza fukuza ni sehemu ya thesis yao?
 
Back
Top Bottom