Dr. Bana, Heche, Mkosamali na Kafulila LIVE ON STAR TV

Binafsi naona ujumbe wa Chadema umefika sababu ujumbe ni nini: Chadema wanalalamika juu yakubadilisha Mfumo ambapo source ya tatizo ni Katiba mfumo utakaopelekea kuwa na Tume huru ya Uchaguzi.

Iwapo hiyo Ishu isingeku raised na Wabunge wa Chadema kwakutoka nje hata nyie hapo na huyo Kafulila msingekuwa mnaongelea Ishu ya Katiba,Tanzania nzima saiv watu wanaongelea Katiba.

Mchakato wa Ishu ya Katiba umeanza siku nyingi lakini CCM hawako tayari coz ina wafavour so hi Ishu inatakiwa iwekwe mezani na idaiwe kwa nguvu zote c kuongelea Chini ya meza kwakujikomba komba.
 
Yahaya Muulize Dk. Bana,
Anasema kitendo walichofanya CHADEMA cha kutoka nje si ustaarabu kwa mujibu wake na kinaweza kuchochea ugomvi. Sasa yeye kama yeye angeshauri CHADEMA wangefanya nini ikiwa NEC walikataa pendeko la CHADEMA la kusitisha utangazwaji wa matokeo ya urais ili wahakiki kwanza hata pale kasoro hizi zilipokuwa bayana?
 
Yahaya hiyo hoja ya Dk.Bana kuwa kitendo cha CHADEMA kianweza kuchochea ugomvi na kuhatarisha amani ni kweli kaiongea hata sisis huku tumeisikia
 
John Heche amepinga kauli ya watu wanaosema CHADEMA ni kama NCCR.

Anasema kuwa NCCR ilipata umaarufu wa ghafla 1995 halafu ikapotea ghafla.

Lakini CHADEMA ilianza 1995 ikiwa na wabunge wawili, 2000 wabunge watatu, na 2005 wabunge watano pamoja na halmashauri 3.

Lakini sasa CHADEMA ina wabunge 49 pamoja na wa viti maalum, na madiwani 600 nchi nzima.


Tunaendelea kumnote.
 
Yahya naomba umuulize Mkosamali,
Je anajua harakati za katiba mpya zilianza lini?? Na watu hao chini ya National Committee for Constituonal Reform(NCCR) walikutana mara ya kwanza 1990 walikubaliana nini?? Je walifikia wapi juu ya lalamiko lao??

Maoni:
Mimi naamini njia za kidiplomasia ilishindikana hata Mbatia aliwahi kutishia kuifikisha mahakamani Tume kwa kuwa si huru mwaka jana nadhani.. Hii ya CHADEMA ndio njia mbadala Ndg. yangu Yahya...

Naomba kutoa haja
Eliesikia
 
Yahaya niulizie swali lingine kwa Mkosamali na Kafulila,
Ile kambi ndogo ya upinzani waliyoiunda kwa ushirikiano na CUF na TLP itakuwa na majukumu gani, sababu kwa utaratibu wa sasa kunakuwa na kambi moja tu ya upinzani bungeni
 
Huyo Kilangilo lazima hafahamu tatizo kubwa kabisa tulilonalo ambalo linaweza kuhatarisha Maisha yetu nakugharimu maisha yetu ni hii Tume ya Uchaguzi,Tunawatia Shime Wabunge wetu wasimame Kidete kuhakikisha inapatikana Tume huru ya Uchaguzi.Hivi huyo Shida amesahau watu walivyokesha bila kula kunishinikiza Matokeo yatangazwe bila ivyo anafikiri huyo Mnyika aliempongeza angepatikana!!
 
sure, CHADEMA is gradually growing ikiwa na mizizi ya waanzilishi wake akina Mzee Mtei tofauti na NCCR ambayo iliboom tu kutokana na introduction na Mrema alipotoka CCM na kuhamia NCCR. Mfano Dr. Slaa yupo na alikuwa Mbunge wa CHADEMA tokea 1995 hivyo wanaelewa vizuri mazingira waliyotoka nayo na wanapokwenda.

Lakini lazima kuwe na angalizo la hawa watu toka CCM or other parts kuingia CHADEMA, waangaliwe vizuri na isiwe kuruhusu kila mtu na kuwa "dodoki" kama alivyosema Nyerere.
 
Eti NCCR ni chama tawala kigoma!! Kafulila's words in STAR TV now. Jamaa kanunuliwa nini!!! Kweli sisiem wameingilia system kila mahali. Poor tanzanian jamani
 
Serikali isisubiri hadi damu imwagike. Wenzetu wa Kenya ilibidi damu imwagike ndipo wakapata katiba mpya. Ya Zanzibar tuliyaona. Kama damu itamwagika Tanzania wakati wa kudai uhalali wa viongozi 2015, kama katiba haikubadilika, basi serikali itabeba lawama zote. Kumbuka watanzania wanapata na wanaendelea kupata elimu ya uraia. Siyo mazezeta kama mnavyofikiria
 
Shukrani Yahya kutushirikisha kwa njia hii.
Dr. Bana, mshauri wa siasa wa mgombea wa CCM wa nafasi ya Rais amesema madai ya Chadema yanazungumzika, na yalianza 1995. Je anakubali kuwa kilichojiri Dodoma kimeliibua suala hilo kwa nguvu mpya?
La pili Yahya, kwa sababu unapata wageni mbalimbali hapo studio, NAOMBA TUFAFANULIWE hayo MAADILI YA KISIASA YA KITANZANIA wakati hatujui kama taifa letu linaelekea kwenye ujamaa au ubepari, ni yepi?
 
Watangazaji wa star tv watangaze wasidhani wana maarifa yoyote zaidi,kukondition mjadala ni upuuzi.kama wana maoni waalikwe kama wazungumzaji siyo watangazaji
 
Yahaya nakushukuru kwa kuwakilisha maswali yaliyotoka kwa wana JF, japo wajibuji walikuwa wanauma uma maneno, ila next time wabane wajibu straight. Sababu kama Mkosamali na Kafulila wanaulizwa yapi ni malengo ya kambi ndogo ya upinzani wao wanajibu eti wako tayari kushirikiana na chama chochote cha upinzani hapo nafikiri hawajatoa jibu sahihi, au wamekwepa swali.
But, nextime kama ulivyohidi tuwekee post mapema, maana ni rahisi kuchangia kupitia mtandao maana sometimes ni tabu sana kupata line ya simu
 
SWALI KWA DR.BANA:
REDET mbona inafanya kazi ya kukuza chama cha CCM? mbona inashndwa kuwa chombo cha kukuza demokrasia nchini? Watu inatoboa saana.

Kama hvyo bas ivunjwe, hawana dira. Tunapenda watu kama Prof. Xavery Lwaitama... Wanatoa elimu nzur kwa umma.
 
Halafu ndugu Yahya kuna wakati mnaonekana kabisa mnafanya kazi ambayo radio uhuru wanatakiwa waifanye,kuna siku mlikuwa mnafanya spining live live....hasa ile siku CHADEMA walipokataa kuhudhuria sherehe za kumwapisha waziri mkuu.Mlipoteza credibility ya kuwa professional Journalists.Thanks kwa kutuhabarisha though!
 
Post maoni na maswali muda huu tutawauliza kwa niaba yenu wanaJF

Poa tunashukuru M, Yahya. Huyo bana ni kweli mshauri wa jey key mambo ya siasa. Kama ni kweli haoini kuna conflict of interest.
 
John Heche amepinga kauli ya watu wanaosema CHADEMA ni kama NCCR.

Anasema kuwa NCCR ilipata umaarufu wa ghafla 1995 halafu ikapotea ghafla.

Lakini CHADEMA ilianza 1995 ikiwa na wabunge wawili, 2000 wabunge watatu, na 2005 wabunge watano pamoja na halmashauri 3.

Lakini sasa CHADEMA ina wabunge 49 pamoja na wa viti maalum, na madiwani 600 nchi nzima.


Tunaendelea kumnote.

Good
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom