MIMI BABA YENU
JF-Expert Member
- Mar 1, 2019
- 295
- 679
Shirika la Habari la Kimataifa la CNBC Africa tarehe 29 Februari, 2020 limerusha kwa zaidi ya nchi 100 duniani makala inayoeleza mafanikio ya Tanzania katika sekta mbalimbali
Ripoti ya RMB ya mwaka 2020 imeitaja Tanzania imekuwa ya 21 duniani, Afrika imekuwa ya 4 na Afrika Mashariki imekuwa ya Kwanza kwa kiwango cha biashara ndogondogo na uboreshaji wa shughuli za machinga
Haki za binadamu sio siasa, kama nchi tumeendelea kusisitiza na tutaendelea kuzienzi haki zote za binadamu
Ujenzi wa reli ya SGR kwa eneo la Dar-Moro umefikia zaidi ya 75% na Moro-Makutopora umefikia zaidi ya 28% ikijumuisha uwekaji wa nguzo na nyaya za umeme ambapo jumla ya fedha zilizotumika hadi sasa ni Trilioni 2.957
Tenda ya ujenzi wa reli ya SGR kutoka Mwanza-Isaka itatangazwa wakati wowote
Ujenzi wa Chelezo katika ziwa victoria umekamilika na inasubiriwa kujaribiwa kwa uzito uliosanifiwa wa tani 4000 na itaanza kutumika katikati mwa mwezi Machi, 2020
Ujenzi wa MV Victoria katika ziwa Victoria umefikia 89% na ukarabati wa MV Butiama umefikia 86%
Mradi umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) sehemu ya ujenzi wa eneo la kuchepusha maji ya mto limekamilika kwa 100%
Utendaji wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi umezidi kuimarika, jumla ya migogoro ya ardhi 10,000 imetatuliwa
Tunataka utawala bora katika vyama vyote vya michezo, sisi kama Serikali tunafuatilia, moja ya eneo ambalo nitalifuatilia kwa karibu katika sekta ya michezo ni vitendo vya rushwa
Mhe Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza kuwa Serikali ijenge uwanja wa Michezo Dodoma uliokuwa ujengwe na Morocco na tunategemea ujenzi wa uwanja huu uanze mwaka huu baada ya ramani kukamilika
Nampongeza sana Mbwana Samatta kwa mafanikio makubwa katika soka, tutaweka mikakati ya kuwa na vituo vya mafunzo vya michezo ‘academy’ ili kukuza na kuendeleza vipaji nchini
Haitatokea katika dunia hii, Serikali yoyote duniani kwa chochote inachokifanya isikosolewe, hata manabii walipingwa, Serikali ina nia na kila sababu ya kutokulala kuwapigania watanzania, sisi tupo kazini tunapiga kazi ili kupata maendeleo
Imeandaliwa na Idara ya Habari - MAELEZO
Sent using Jamii Forums mobile app
Ripoti ya RMB ya mwaka 2020 imeitaja Tanzania imekuwa ya 21 duniani, Afrika imekuwa ya 4 na Afrika Mashariki imekuwa ya Kwanza kwa kiwango cha biashara ndogondogo na uboreshaji wa shughuli za machinga
Haki za binadamu sio siasa, kama nchi tumeendelea kusisitiza na tutaendelea kuzienzi haki zote za binadamu
Ujenzi wa reli ya SGR kwa eneo la Dar-Moro umefikia zaidi ya 75% na Moro-Makutopora umefikia zaidi ya 28% ikijumuisha uwekaji wa nguzo na nyaya za umeme ambapo jumla ya fedha zilizotumika hadi sasa ni Trilioni 2.957
Tenda ya ujenzi wa reli ya SGR kutoka Mwanza-Isaka itatangazwa wakati wowote
Ujenzi wa Chelezo katika ziwa victoria umekamilika na inasubiriwa kujaribiwa kwa uzito uliosanifiwa wa tani 4000 na itaanza kutumika katikati mwa mwezi Machi, 2020
Ujenzi wa MV Victoria katika ziwa Victoria umefikia 89% na ukarabati wa MV Butiama umefikia 86%
Mradi umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) sehemu ya ujenzi wa eneo la kuchepusha maji ya mto limekamilika kwa 100%
Utendaji wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi umezidi kuimarika, jumla ya migogoro ya ardhi 10,000 imetatuliwa
Tunataka utawala bora katika vyama vyote vya michezo, sisi kama Serikali tunafuatilia, moja ya eneo ambalo nitalifuatilia kwa karibu katika sekta ya michezo ni vitendo vya rushwa
Mhe Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza kuwa Serikali ijenge uwanja wa Michezo Dodoma uliokuwa ujengwe na Morocco na tunategemea ujenzi wa uwanja huu uanze mwaka huu baada ya ramani kukamilika
Nampongeza sana Mbwana Samatta kwa mafanikio makubwa katika soka, tutaweka mikakati ya kuwa na vituo vya mafunzo vya michezo ‘academy’ ili kukuza na kuendeleza vipaji nchini
Haitatokea katika dunia hii, Serikali yoyote duniani kwa chochote inachokifanya isikosolewe, hata manabii walipingwa, Serikali ina nia na kila sababu ya kutokulala kuwapigania watanzania, sisi tupo kazini tunapiga kazi ili kupata maendeleo
Imeandaliwa na Idara ya Habari - MAELEZO
Sent using Jamii Forums mobile app