‪DPP atumie madaraka yake kisheria ipasavyo, asisubiri maelekezo ya wanasiasa ili afanye kazi‬

Sio tuu mimi na wewe hatuwezi kumbana DPP, bali hakuna yoyote mwenye uwezo wa kumbana, hata rais hawezi!.
Mzee MMKJJ, yote uliyosema kuhusu DPP ni kweli, lakini pia kwa mujibu ya sheria iliyounda ofisi ya DPP, havunji sheria yoyote kwa kutofanya uchunguzi wowote kwa vile hayo ndio mamlaka yake ambayo kisheria, anayatumia at his discretion as he pleases at his pleasure na sheria inamlinda.
Kwa maoni yangu, tatizo sio DPP, tatizo ni mamlaka ya ajabu yaliyochini ya DPP.
Niliwahi kuchangia mahali nikaainisha sheria yetu iliyounda ofisi ya DPP, amepewa mamlaka makubwa yac ajabu, na hayo aliyoyaainisha MMKJJ ni dibaji tuu, nguvu haswa za DPP ni pamoja na 'power to declare nolle proseque' yaani hakuna kesi ya kujibu. DPP huyu anauwezo wa kuingilia kesi yoyote ya jinai, ikiwa mahakama yoyote na ikiwa katika hatua yoyote kabla ya hukumu, kuisimamisha, kingilia, ama kuifuta bila kulazimika kutoa sababu zozote wala maelezo yoyote.
Sheria ya DPP inamtaka kutimiza wajibu wake bila shinikizo lolote kutoka popote na hata akiletewa kesi yoyote ni discretion yake aprosecute ama asiprosecute na hakuna chombo chochote ndani ya JMT chenye mamlaka ya kumuuliza lolote DPP, hata rais hana mamlaka hayo, sembuse MMKJJ?.

Naungana na WoS sisi mwisho wetu ni kupiga tuu kelele, japo za mlango, siku moja moja mwenye nyumba atakosa usingizi kwa sababu nyingine na atazisikia hizi kelele za mlango na ama ataamka na kuubana mlango, ama atautia kizuizi ili usiendelee kupiga kelele.

Enzi za Mwalimu kulikuwa na sheria ya 'Presidential Preventive Detention Orders' iliyompa rais mamlaka ya kumuweka mtu yoyote kizuizini kwa kipindi chochote bila kutoa sababu yoyote. Mwalimu Nyerere aliitumia kipindi chote cha utawala wake. Kipindi cha Mwinyi, wanasheria wa chuo kikuu wakiongozwa na Shivji na Mgongo Fimbo, waliichalenge sheria hii kwa 'court review' na mahakama ikatamka its a bad law, hivyo ikamlazimisha rais, kila akisaini 'preventive detention order' lazima atoe sababu. kuna detention moja ya Mwinyi ilipigwa chini na mtuhumiwa kuachiwa huru.

Kama wanasheria wetu, waliweza kufanya hivi dhidi ya mamlaka ya rais, wanashindwa nini kwenye mamlaka ya DPP?.
Kwa mawazo yangu, 'Tatizo sio Feleshi as DPP, ni mamlaka yake makubwa mno anayatumia atakavyo bila kuvunja sheria. Tazizo ni the institutional of the DPP.

watu wengi wanachanganya sheria ya Prevention and Detention ambayo bado ipo na sheria ya Emergency Powers za Rais. Sheria ya Prevention and Detention haimpi nguvu Rais kwa kiasi hicho ila ya Emergency Powers. Sijui kuhusu specific cases lakini ninafahamu sheria ambayo imewahi kutumiwa vibaya ni hiyo ya emergency powers ambayo ilidaiwa kutumika kwenye suala hili la EPA pia..

Unaweza kunisaidia review ya hiyo kesi ya kina Shivji juu ya Prevention and Detention?
 
Nadhani, watu wakisoma wataelewa wanapomtwisha JK lawama za watu kufikishwa mahakamani wanakosea. Wakumkomalia ni DPP. Huyu jamaa ndiyo kikwazo kikubwa cha mapambano haya kwani kama angekuwa anafanya kazi yake kama alivyoapa na kwa mujibu wa sheria leo hii tusingekuwa tunazungumza mambo mengine ambayo tunazungumza. Aidha afanye kazi yake au aamue kukaa pembeni aingie mtu mwingine mwenye ujasiri wa kufanya kazi hiyo.

Whatever the case, Kikwete ulimately ndiye atakayebeba lawama kwa mambo yote makubwa yatakayoenda mrama.

Kikwete anapewa nguvu sana kikatiba, na hata DPP anayemteua ni yeye rais kwa hiyo hata kama rais hana mamlaka formally (which I doubt) ana mamlaka politically, kwa hiyo katika principles za "noblesse oblige", hii power aliyonayo Kikwete inakuja na responsibility. The buck stops with Kikwete, ndiyo maana kila siku watu wanamsema yeye, yeye ndiye rais, DPP si rais.

Kama DPP hafanyi kazi si aondolelwe tu? Mimi nina mashaka DPP amepewa mipaka asivuke, na huenda anacheki na Ikulu.
 
Last edited:
Pasco.. na wengine.. ninachosema ni kuwa DPP amekuwa kimya kwa sababu the pressure is not on him. Watu bado wanataka tumbane JK wakati hana uwezo wala nguvu ya kisheria ya kuendesha mashtaka au kumshtaki mtu. Nguvu hizo ziko kwa DPP.

Nilikuwa miongoni mwa watu waliopinga kabisa kwa DPP kuwa sehemu ya tume inayoundwa na Rais kuchunguza EPA.. kwangu DPP ndiye alitakiwa aunde tume hiyo au kusimamia uchunguzi huo. Watu walipofurahia kuwa hatimaye tume imeundwa hawakujua wanafurahia nini.

Ndiyo maana nasema hata kule Bungeni, Wabunge wamlilie DPP kwenye Meremeta, Mwananchi, Deep Green na wengine.. kuililia "serikalii" tu haitoshi.

We have to put the pressure where it matters! Kusema JK JK JK might be politically popular lakini kiukweli ni kuwa kwenye uwanja wa sheria ni DPP ndiye tunatakiwa kumbana. Kwanini?

a. Kwa sababu ndiye mwenye wajibu wote wa kisheria kwenye mambo ya mashtaka
b. Rais au mtu mwingine yoyote hawezi kumtimua au kuingilia uchunguzi wake.
c. Ana uwezo wa kuteua mtu mwingine kuendesha uchunguzi kwa niaba yake hata Mwanasheria binafsi!

So, kisiasa tunaweza kufanya sawa kupiga kelele kwa Rais lakini itabakia kuwa ni siasa tu; tukitaka kweli sheria ifuate mkondo wa kumbana ni DPP.
Bado niko na wewe kwenye hili, ila nimekwenda zaidi kwa kusema kuwa sio Feleshi, ni mamlaka yaliyo chini yake kwa kutoyafanya hayo yote, pia ni miongoni mwa kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa sheria

a. Kwa sababu ndiye mwenye wajibu wote wa kisheria kwenye mambo ya mashtaka, pia ana manlaka ya kotoendesha mashitaka yoyote bila sababu yoyote na bila kuulizwa na yoyote.
b. Rais au mtu mwingine yoyote hawezi kumtimua au kuingilia uchunguzi wake. pia ana manlaka ya kusimamisha uchunguzi wowote katika hatua yoyote bila kuulizwa na yoyote.
c. Ana uwezo wa kuteua mtu mwingine kuendesha uchunguzi kwa niaba yake hata Mwanasheria binafsi! pia ana uwezo wa kutoteu yoyote, ama kuzuia uchunguzi wowote kuendeshwa na yeyote bila kuulizwa sababu yoyote.
Pamoja na sheria kuruhusu Private Prosecution' bado ni DPP ndiye anayetoa kibali che kuendeshwa kwa uchunguzi huo, akiwa na mamlaka ya kutotoa kibali chote bila kutoa sababu yoyote.
Bado nasimama na sheria inayompa DPP mamlaka aliyonayo.
To be honest, hata kama mimi ndiye ningekuwa DPP, najua RA ndiye Kagoda na ni rafiki na Rais na mfadhili mkuu wa CCM, kama sheria inaniruhusu nisimprosecute na siulizwi popote na yeyote, sitamprosecute!.
 
Bado niko na wewe kwenye hili, ila nimekwenda zaidi kwa kusema kuwa sio Feleshi, ni mamlaka yaliyo chini yake kwa kutoyafanya hayo yote, pia ni miongoni mwa kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa sheria

a. Kwa sababu ndiye mwenye wajibu wote wa kisheria kwenye mambo ya mashtaka, pia ana manlaka ya kotoendesha mashitaka yoyote bila sababu yoyote na bila kuulizwa na yoyote.
b. Rais au mtu mwingine yoyote hawezi kumtimua au kuingilia uchunguzi wake. pia ana manlaka ya kusimamisha uchunguzi wowote katika hatua yoyote bila kuulizwa na yoyote.
c. Ana uwezo wa kuteua mtu mwingine kuendesha uchunguzi kwa niaba yake hata Mwanasheria binafsi! pia ana uwezo wa kutoteu yoyote, ama kuzuia uchunguzi wowote kuendeshwa na yeyote bila kuulizwa sababu yoyote.
Pamoja na sheria kuruhusu Private Prosecution' bado ni DPP ndiye anayetoa kibali che kuendeshwa kwa uchunguzi huo, akiwa na mamlaka ya kutotoa kibali chote bila kutoa sababu yoyote.
Bado nasimama na sheria inayompa DPP mamlaka aliyonayo.
To be honest, hata kama mimi ndiye ningekuwa DPP, najua RA ndiye Kagoda na ni rafiki na Rais na mfadhili mkuu wa CCM, kama sheria inaniruhusu nisimprosecute na siulizwi popote na yeyote, sitamprosecute!.

DPP anateuliwa na nani? DPP anaweza kuondolewa na nani? DPP serves at whose pleasure?

Where does the DPP get his cues and priority?

Ukichunguza utaona DPP kawekwa pale kikaragosi tu, na kama rais anataka DPP afuatilie jambo fulani atafuatilia tu, kama rais hataki DPP ni vigumu kufuatilia.

It is as if the system is set up to fool people into thinking "The president's hands are tied, this issue rests with the office of the DPP"

While the president is the one with the political capacity to give directions all along.
 
Whatever the case, Kikwete ulimately ndiye atakayebeba lawama kwa mambo yote makubwa yatakayoenda mrama.

Kikwete anapewa nguvu sana kikatiba, na hata DPP anayemteua ni yeye rais kwa hiyo hata kama rais hana mamlaka formally (which I doubt) ana mamlaka politically, kwa hiyo katika principles za "noblesse oblige", hii power aliyonayo Kikwete inakuja na responsibility. The buck stops with Kikwete, ndiyo maana kila siku watu wanamsema yeye, yeye ndiye rais, DPP si rais.

Kama DPP hafanyi kazi si aondolelwe tu? Mimi nina mashaka DPP amepewa mipaka asivuke, na huenda anacheki na Ikulu.

Huwezi kumuondoa na hawezi kuondolewa kirahisi! la maana kama tunataka kweli ni kumtaka DPP ajiuzulu ili Rais amteue mtu mwingine (hilo linawezekana). Tukianza kumpigia kelele DPP ajiuzulu au afanye kazi yake tutaona.... lakini kumpigia kelele JK ni nzuri kisiasa.
 
DPP anateuliwa na nani? DPP anaweza kuondolewa na nani? DPP serves at whose pleasure?
Anateuliwa na rais, hawezi kuondolewa mpaka ithibitishwe is of 'unsound mind'. He saves at his own pleasure although also for 'who pays the piper, may call the tune'
 
Anateuliwa na rais, hawezi kuondolewa mpaka ithibitishwe is of 'unsound mind'. He saves at his own pleasure although also for 'who pays the piper, may call the tune'

Hawezi "kustaafishwa kwa manufaa ya umma" au "kupangiwa kazi nyingine"?

Unataka kuniambia kama kweli Kikwete anataka kumuondoa DPP anashindwa?
 
Hawezi "kustaafishwa kwa manufaa ya umma" au "kupangiwa kazi nyingine"?

Unataka kuniambia kama kweli Kikwete anataka kumuondoa DPP anashindwa?
just read between the lines, jamaa anamfanyia kazi nzuri sana JK. ndie mastermind viini macho vyote vinavyoendelea mahakamani.
 
just read between the lines, jamaa anamfanyia kazi nzuri sana JK. ndie mastermind viini macho vyote vinavyoendelea mahakamani.


Which is precisely my point, kumlaumu DPP ni kumaumu puppet wakati unamuachia puppet master mwenyewe JK (ambaye naye ni puppet wa mafisadi in turn) aende Scot free.
 
Which is precisely my point, kumlaumu DPP ni kumaumu puppet wakati unamuachia puppet master mwenyewe JK (ambaye naye ni puppet wa mafisadi) aende Scit free.
thats the name of the game and we all dance to the music
 

Kama DPP hafanyi kazi si aondolelwe tu?

Hawezi kumuondoa, wala hana utaratibu wa kumpa dira ya kazi.

DPP ilibidi awe Mwanasheria Mkuu ambae anaingia kwenye cabinet ambayo ndio moja ya bully pulpit ya uongozi wa nchi ku set the national agenda, kama vile kupambana na ufisadi na utawala wa sheria kwa ujumla. Katikati ya Rais na DPP kuna Mwanasheria Mkuu, kuna Waziri wa Sheria, ambao ni cabinet members, lakini sio mhusika wenyewe, DPP, hivyo uwezo wa Rais juu ya kumkoromea DPP uko mbali sana, kama upo.

Tatizo ni mfumo wa sheria. DPP ilibidi awe Mwanasheria Mkuu, member wa cabinet, au Rais aweze kum fire DPP.
 
Pasco.. na wengine.. ninachosema ni kuwa DPP amekuwa kimya kwa sababu the pressure is not on him. Watu bado wanataka tumbane JK wakati hana uwezo wala nguvu ya kisheria ya kuendesha mashtaka au kumshtaki mtu. Nguvu hizo ziko kwa DPP.

Nilikuwa miongoni mwa watu waliopinga kabisa kwa DPP kuwa sehemu ya tume inayoundwa na Rais kuchunguza EPA.. kwangu DPP ndiye alitakiwa aunde tume hiyo au kusimamia uchunguzi huo. Watu walipofurahia kuwa hatimaye tume imeundwa hawakujua wanafurahia nini.

Ndiyo maana nasema hata kule Bungeni, Wabunge wamlilie DPP kwenye Meremeta, Mwananchi, Deep Green na wengine.. kuililia "serikalii" tu haitoshi.

We have to put the pressure where it matters! Kusema JK JK JK might be politically popular lakini kiukweli ni kuwa kwenye uwanja wa sheria ni DPP ndiye tunatakiwa kumbana. Kwanini?

a. Kwa sababu ndiye mwenye wajibu wote wa kisheria kwenye mambo ya mashtaka
b. Rais au mtu mwingine yoyote hawezi kumtimua au kuingilia uchunguzi wake.
c. Ana uwezo wa kuteua mtu mwingine kuendesha uchunguzi kwa niaba yake hata Mwanasheria binafsi!

So, kisiasa tunaweza kufanya sawa kupiga kelele kwa Rais lakini itabakia kuwa ni siasa tu; tukitaka kweli sheria ifuate mkondo wa kumbana ni DPP.

Pamoja na kuwa mimi si mwanasheria lakini bado nina maswali machache,

a)Nani au ni mamlaka ipi yenye uwezo wa kumsimamisha kazi DPP pale itakapoonekana dhairi kuwa hana uwezo nayo? Mathlani amepata matatizo ya akili, amekuwa mlevi kupindukia n.k. Haiwezekani kuwa hamna namna ya kumtoa maana hata majaji kuna utaratibu. Jopo la majaji wenzake n.k.

b) utumishi wa DPP ni wa muda gani? Ana specific term au hadi afikie umri wa kustaafu au kama Supreme Justices wa Marekani, atakapoamua mwenyewe?

c) Rais ana uhuru gani katika uteuzi wa DPP? Nini vigezo anavyopaswa kufuata kisheria?

Mimi bado napinga wazo la kusema kuwa Rais hana nguvu yeyote juu ya DPP. Rais alipomteua ni lazima alipima loyalty yake kwa serikali yake. Si rahisi ( mahali popote) kuchagua mtu kaika sehemu nyeti kama hii ambae utajua kuwa hautakuwa na influence nae, directly au indirectly. Indirectly, kwamba hawezi kufanya kitu ambacho anajua wazi kuwa kitahatarisha stability ya utawala wako. Hasa kama sheria inampa mamlaka ya kufanya hivyo, kutokufanya kitu. Kusema kuwa ati tukimuandama DPP bila kumuandama aliyemweka kutaweza kumfanya achukue hatua kama hiyo ni kujidanganya. Hivi unataka tuamini kuwa ni uzembe tu ndio unaomfanya akae kimya?

Kwa kumwandama aliyemteua na kugeuzi ishu nzima kuwa political kiasi cha kufanya kurejea kwao kwenye madaraka kuwa mashakani ndio njia pekee wananchi waliyokuwa nayo. Rais akitamka hadharani kuwa haoni kwa nini DPP hawafungulii mashtaka wahusika kama anaona wana kesi ya kujibu, DPP hatakuwa na sehemu ya kujificha. Nguvu ya wananchi ni kwa wale tunaowapigia kura na si kwa hao watendaji. Tatizo la argument yako kwangu mimi ni hapo unapodai kuwa kumuandama Rais ni kupoteza wakati maana hana nguvu zozote kisheria. Ningekuunga mkono kama ungetukumbusha kuwa wakati anaandamwa Rais,asisahauliwe DPP. Naamini kuwa watanzania wanaweza kula big G wakati wanatembea!

Amandla.......
 
Baada ya mjadala wote huu, je kuna mtu anamfahamu vizuri huyu DPP atumwagie ili tupate fursa ya kuchangia kwa upana zaidi.
 
Baada ya mjadala wote huu, je kuna mtu anamfahamu vizuri huyu DPP atumwagie ili tupate fursa ya kuchangia kwa upana zaidi.


anafahamika kuwa ni msomi aliyebobea ambaye alipoteuliwa watu walisifia kuwa ni kiongozi kijana n.k n.k matokeo yake ni haya ya ukuti ukuti wa ufisadi! Tukisema tunaambiwa "tuna chuki binafsi"
 
Kwani DPP, hawezi kushtakiwa na umma au mtu binafsi kama ushahidi upo kuwa anakiuka miiko yake ya kazi? kama anaenda kinyume na maslahi ya nchi?
 
Kwani DPP, hawezi kushtakiwa na umma au mtu binafsi kama ushahidi upo kuwa anakiuka miiko yake ya kazi? kama anaenda kinyume na maslahi ya nchi?

Naamini kama Bar inaweza kumfutia leseni yake kama amekiuka miiko ya kazi yake anapoteza sifa ya kuwa wakili siyo?
 
anafahamika kuwa ni msomi aliyebobea ambaye alipoteuliwa watu walisifia kuwa ni kiongozi kijana n.k n.k matokeo yake ni haya ya ukuti ukuti wa ufisadi! Tukisema tunaambiwa "tuna chuki binafsi"

Lakini kwa kumbukumbu zilizopo, hadi anateuliwa kuwa DPP hakuwahi kufika hata daraja la Principal State Attorney au nimekosea mimi. Mwenye kujua zaidi atusaidie.
 
Lakini kwa kumbukumbu zilizopo, hadi anateuliwa kuwa DPP hakuwahi kufika hata daraja la Principal State Attorney au nimekosea mimi. Mwenye kujua zaidi atusaidie.

Daraja la kuwa Principal halikuwa muhimu bali iliangaliwa kwa kigezo cha je atasikiliza mruzi wa bwana???
 
Hakika umebainisha ukweli mtupu.
Lakin kwa uzoefu wangu wa Tanzania labda anatishwa na viongozi wakuu wa Serikali ikiwa pamoja na vyombo va usalama kutekeleza wajibu wake aliopewa kikatiba.
 
Back
Top Bottom