Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,105
- 35,046
Miongoni mwa watu walioteuliwa leo na Rais Samia Suluhu kuwa majaji wa mahakama kuu, jina la DPP Biswalo Maganga lipo pia.
Hili jambo limetushtua sana wadau wa mambo ya sheria, kuna kitu tunakiona hakiko sawa na kinakwenda kutuharibia zaidi mhimili wetu wa sheria. Nitaweka sababu za msingi sana kwanini Biswalo Maganga hastahili kuwa jaji.
1. Kabla ya mtu kupendekezwa kuwa jaji, ni lazima vetting ifanyike kisheria. Hili ni jambo la kisheria na linapaswa kufanyika kwa haki, uwazi na weledi. Biswalo Maganga hakufanyiwa vetting na tume utumishi wa mahakama popote pale.
2. Kabla ya mtu kuteuliwa kuwa jaji ni lazima jina lake lipendekezwe na tume ya mahakama. DPP Biswalo Maganga hakupendekezwa popote.
3. Nafasi iliyokuwa nayo kama DPP haiwezi kumruhusu kufanyiwa vetting au kupendekezwa kuwa jaji na vyombo vya mahakama. Ni sawa na kufanya 'vetting na kupendekeza' Rais Samia awe spika wa bunge wakati huo akiwa bado Rais!
4. Haiwezekani kwa mtu kutoka kwenye nafasi ya DPP na moja kwa moja kuteuliwa kuwa Jaji, kimahakama inatia ukakasi mkubwa. Yaani jana DPP alikuwa ana file kesi za jinai dhidi ya watu fulani halafu leo anakuwa jaji wa mahakama hiyo hiyo kusikiliza kesi na kuhukumu kesi hizo hizo!.
5. Tabia, sifa, mwenendo na vitendo vingi alivyovifanya Biswalo Maganga akiwa kama DPP dhidi ya utendaji wa mahakama havistahili hata chembe kuweza kufikiriwa kuwa hata hakimu wa mahakama yoyote ya kutoa haki hapa duniani. (Mganga aliweza kuamuru mtu yoyote afikishwe mahakamani hata kama hakuna mashtaka dhidi yake ama aachiwe huru hata kama hati ya mashtaka hairuhusu hilo kufanyika). Rais angeweza kumtunuku Biswalo Mganga chochote kile kwenye mhimili wake wa serikali (ikiwa alikuwa anamhitaji) lakini sio kumsukumizia kwenye mhimili wa mahakama. Huko ni kuwatukana wanasheria wa mahakama kuu.
Kwa wale wasio na uelewa wa mambo ya kisheria na mfumo wa uteuzi wa majaji hapa Tanzania, kikatiba uteuzi wa majaji ni jambo linapaswa kuzingatia weredi, mchakato mpana na muda mrefu. Sio jambo ghafla, fadhila au mapendekezo binafsi ya Rais aliyepo madarakani.
Hili jambo limetushtua sana wadau wa mambo ya sheria, kuna kitu tunakiona hakiko sawa na kinakwenda kutuharibia zaidi mhimili wetu wa sheria. Nitaweka sababu za msingi sana kwanini Biswalo Maganga hastahili kuwa jaji.
1. Kabla ya mtu kupendekezwa kuwa jaji, ni lazima vetting ifanyike kisheria. Hili ni jambo la kisheria na linapaswa kufanyika kwa haki, uwazi na weledi. Biswalo Maganga hakufanyiwa vetting na tume utumishi wa mahakama popote pale.
2. Kabla ya mtu kuteuliwa kuwa jaji ni lazima jina lake lipendekezwe na tume ya mahakama. DPP Biswalo Maganga hakupendekezwa popote.
3. Nafasi iliyokuwa nayo kama DPP haiwezi kumruhusu kufanyiwa vetting au kupendekezwa kuwa jaji na vyombo vya mahakama. Ni sawa na kufanya 'vetting na kupendekeza' Rais Samia awe spika wa bunge wakati huo akiwa bado Rais!
4. Haiwezekani kwa mtu kutoka kwenye nafasi ya DPP na moja kwa moja kuteuliwa kuwa Jaji, kimahakama inatia ukakasi mkubwa. Yaani jana DPP alikuwa ana file kesi za jinai dhidi ya watu fulani halafu leo anakuwa jaji wa mahakama hiyo hiyo kusikiliza kesi na kuhukumu kesi hizo hizo!.
5. Tabia, sifa, mwenendo na vitendo vingi alivyovifanya Biswalo Maganga akiwa kama DPP dhidi ya utendaji wa mahakama havistahili hata chembe kuweza kufikiriwa kuwa hata hakimu wa mahakama yoyote ya kutoa haki hapa duniani. (Mganga aliweza kuamuru mtu yoyote afikishwe mahakamani hata kama hakuna mashtaka dhidi yake ama aachiwe huru hata kama hati ya mashtaka hairuhusu hilo kufanyika). Rais angeweza kumtunuku Biswalo Mganga chochote kile kwenye mhimili wake wa serikali (ikiwa alikuwa anamhitaji) lakini sio kumsukumizia kwenye mhimili wa mahakama. Huko ni kuwatukana wanasheria wa mahakama kuu.
Kwa wale wasio na uelewa wa mambo ya kisheria na mfumo wa uteuzi wa majaji hapa Tanzania, kikatiba uteuzi wa majaji ni jambo linapaswa kuzingatia weredi, mchakato mpana na muda mrefu. Sio jambo ghafla, fadhila au mapendekezo binafsi ya Rais aliyepo madarakani.