DPP Biswalo Maganga kuwa Jaji, Rais Samia umekosea sana

Miongoni mwa watu walioteuliwa leo na Rais Samia Suluhu kuwa majaji wa mahakama kuu, jina la DPP Biswalo Maganga lipo pia.

Hili jambo limetushtua sana wadau wa mambo ya sheria, kuna kitu tunakiona hakiko sawa na kinakwenda kutuharibia zaidi mhimili wetu wa sheria. Nitaweka sababu za msingi sana kwanini Biswalo Maganga hastahili kuwa jaji...
Watanzania mna bahati mbaya kwa kuwa hamjui mnacho taka. Nakubaliana na yote uliyoandika kasoro pale unapomkosoa Rais Samia SSH kumteua kuwa Jaji.

Pima kati ya mawili lipi ni jema. Biswalo kubakia DPP ambaye maamuzi yake ya kimashtaka yeye hawi challenged na mamlaka nyingine yeyote, au kuwa Jaji wa Mahakama Kuu anaweza kuwa challenged na Mahakama ya Rufaa?

Kumtoa DPP ni suala la kikatiba/ kisheria kama ilivyo kumtoa CAG. Rais ana mamlaka ya kuwateua, lakini kuwatoa ofsini ni mchakato mrefu.

Je mnataka Rais avunjje Katiba Kama Mwendazake alivyofanya kwa kutoa Prof Assad aliyekuwa CAG?

Tumepata Rais msikivu na anayependa kufuata Katiba, asiyependa kuonea watu bado haturidhiki?
Hebu tujifunze kwa yaliyotupata baada ya kumponda JK, tukapata dude la kutisha
 
Nakumbuka wakati wa Magufuli aliwahi kusema Biswalo alipendekezwa kua jaji ila yeye akakataa kwani ni mtu ambae anawapeleka mafisadi jela.

Kama sasa hajapendekezwa labda mama ametumia mapendekezo ya awali. Hilo la kwanza.

La pili, kwani mapendekezo hua yanatumwa kwa nani ili tujue kama hakupendekezwa ama alipendekezwa?


Dah hii kavu sana
 
Pendekezo la jana kuwa na sifa za kuwa jaji halina maana linaweza kutumika leo kuwa jaji. Kwanini? Sifa za mtu hubadilika kutokana na nafasi aliyonayo, nyakati tuliyopo na mwenendo wake.
Wewe ni mjuvi wa mambo lakini umeamua kutumia ujuzi wako ndivyo sivyo. Mbona umesahau kuwa wakati wa Mwendazake karibu maamuzi yote iwe Mahakamani, Bungeni, Polisi au yalikuwa yanafanywa na yeye au watendaji walikuwa wanaogopa kuamua kinyume.

Hata kama ungekuwa wewe Zanzibar-ASP ndiye DPP wakati wa Mwendazake ungefanya hivyo hivyo
 
Hiyo ndio njia pekee ya kumtoa pale jamaa....Mama katumia fimbo ya kisiasa kumchapa kama alivyomchapa Bashiru.... unampromote kumtoa usiyempenda huko umakompeleka unakwenda kumtelekeza kimyakimya.... Mama sasa yuko huru kufanya uteuzi wa DPP....
Ndio awe jaji si angemteua awe hata DAS huko Namtumbo
 
  • Thanks
Reactions: y-n
Watanzania mna bahati mbaya kwa kuwa hamjui mnacho taka. Nakubaliana na yote uliyoandika kasoro pale unapomkosoa Rais Samia SSH kumteua kuwa Jaji.

Pima kati ya mawili lipi ni jema. Biswalo kubakia DPP ambaye maamuzi yake ya kimashtaka yeye hawi challenged na mamlaka nyingine yeyote, au kuwa Jaji wa Mahakama Kuu anaweza kuwa challenged na Mahakama ya Rufaa?

Kumtoa DPP ni suala la kikatiba/ kisheria kama ilivyo kumtoa CAG. Rais ana mamlaka ya kuwateua, lakini kuwatoa ofsini ni mchakato mrefu.

Je mnataka Rais avunjje Katiba Kama Mwendazake alivyofanya kwa kutoa Prof Assad aliyekuwa CAG?

Tumepata Rais msikivu na anayependa kufuata Katiba, asiyependa kuonea watu bado haturidhiki?
Hebu tujifunze kwa yaliyotupata baada ya kumponda JK, tukapata dude la kutisha
Rubbish
 
Kwa taarifa tu

Jaji Kiongozi wa sasa Dr Feleshi aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu mwaka 2014 akitokea NAFASI ya DPP

KATIBA INAMPA MAMLAKA RAIS YA KUTENDA ALIYOTENDA BAADA YA KUSHAURIANA NA JOPO HUSIKA
Kwa kuongezea hapa, kisheria DPP ana hadhi sawa na judge wa Mahakama mkuu.
 
Ukweli ni Huu... Kingine kama Kuna mtu yeyote anategemea mabadiliko kutoka kwa kiongozi ambae anatokana na CCM basi huyo mtu ni kichaa.
IMG-20201201-WA0004.jpg
 
Msiwe na hofu hata kidogo. Hapo kasogezewa karoti ili tukate kichwa. Ni suala la muda tuuu
 
Kuondokana na haya madudu yote, Katiba Mpya ndiyo suluhisho pekee kwa sasa.
 
Hawaja elewa kwamba hapakuwa na njia nyingine ya kumtoa hapo bila kumpsndisha cheo
Na sio yeye tuu katolewa, bali hata naibu wake.
Kumtoa ni tiba zaidi kwa Taifa kuliko kumuacha
mama aha lengo zuri tu kufuta kesi zote zinazoonekana kuonea watu, mfano uamsho,Ruge,n.k. na kutengua uteuzi wake na kumwacha mtaani isingekuwa busara. Mwacheni mama apange serikali yake tuingie kazini kuchapa kazi kwa maslahi mapana ya nchi yetu
 
  • Thanks
Reactions: y-n
Samia alivyoingia madakani mlishangilia na kuona mmpepata mkombozi atawatoa kwenye kero za jiwe. Nashangaa now nyuzi za kumkosoa zimetaradadi.
Poleni.
 
Teuzi zake za wasiwasi zimekuwa kielelezo cha utawala wake, kuanzia yule mkurugenzi wa TPDC aliemteua na baadae kutengua uteuzi wake within 24 hrs mpaka leo bado anayumba tu.

Sijui washauri wake huwa wanamshauri vitu gani, she is too soft hearted, hataki kutumbua yeye anakutoa hapa anakuweka pale hata kama hufai kulingana na historia yako, na ni Rais mwenyewe aliesema anamteua mtu kutokana na historia yake, sijui kwa Maganga katumia historia ipi.
Hata jpm alitengua ukurugenzi tpdc na kupelekwa mahakamani.
Kesi ilifutwa na jpm kumteua tena kurudi tpdc,
 
Hakuna ushaidi kabisa kwamba

Kisheria na mfumo wa uteuzi wa majaji hapa Tanzania, kikatiba uteuzi wa majaji ni jambo lilalozingatia weledi, mchakato mpana na la muda mrefu. HAKUNA ushahidi kwamba Sio jambo la ghafla, fadhila au mapendekezo binafsi ya Rais aliyepo madarakani.

Na mfano ni pale Jiwe aliwahi kumteua mtu jaji kwa sababu ameandika hukumu kwa kiswahili
 
Ndio maana kuna umuhimu wa kupata katiba mpya kuondoa huu mkanganyiko ambao unaharibu kabisa mfumo wa kutoa haki.
Kwa taarifa tu

Jaji Kiongozi wa sasa Dr Feleshi aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu mwaka 2014 akitokea NAFASI ya DPP

KATIBA INAMPA MAMLAKA RAIS YA KUTENDA ALIYOTENDA BAADA YA KUSHAURIANA NA JOPO HUSIKA
 
Yeye anaweza kuziondia au pia anaweza kutunga sheria zake kinyume ya zile za jiwe
Mambo mengine nadhani mnamuonea tu.

Hili ni moja ya janga alilolitengeneza Magu. Na hatukusaidia chochote.

Watu wake wengi aliwatungia sheria za kuwalinda ili wavuruge atakavyo. Spika, Waziri Mkuu, DPP

Hata Rais Samia yawezekana hamtaki ila kaona hiyo ndio njia yenye afadhali.

Soma hizo sheria akizotunga Jiwe

View attachment 1781254

View attachment 1781255
 
Tutakuwa nchi ya hovyo sana kama tutaendelea kuishi kwa katiba hii chakavu.
Katiba yetu raha sana, ni kama tunatawaliwa kifalme vile kama Kwazulu land au E-swati kwa Mswati.... Na kwa bahati mbaya/ nzuri suala la katiba halikuwepo kwenye Ilani ya Chama cha Mama, Wacha majoka yarukwe tu.
 
Unaelewa kweli maana ya mahakama??
Hata hao watu kidogo atakaowaonea akiwa jaji hawapaswi hata wao kuonewa.Mahakama inapaswa kuwa sehemu ya mwisho ya kimbilio kwa wanaotafuta haki zao sasa kama kuna watu inajulikana wazi hawatatenda haki na bado wanapewa nafasi ya maamuzi ni kuchangikwa haswa kwa watu na mfumo mzima.
Kuna baadhi ya mambo tunatakiwa kuyafikiria kwa upana,sio haraka haraka za kukurupuka,kuteuliwa kuwa jaji kutoka dpp ni kama kuwa demoted in a right sense,kuwa jaji ni wa mahakama moja tu, na kama mtu ni muonevu ataonea watu kidogo tu, tafauti na kuwa dpp,dpp ni wa nchi nzima Akiwa muonevu system nzima ya kiserikali itakuwa ya kiuonevu,kumuondoa dpp lazima umpe keki isiyokatalika,sababu analindwa na sheria lazima ajiuzulu mwenyewe.
 
Back
Top Bottom