Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,807
- 11,969
MKURUGENZI wa Mashitaka nchini (DPP), amewasilisha hati katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya kwamba anamuondolea mashitaka mfanyabiashara Mustapha Kambangwa ambaye alikuwa anakabiliwa na mashitaka yake manne yakiwemo kuisababishia Serikali hasara ya sh.bilioni 188.9.
DPP aliwasilisha hati hiyo leo Mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Joseph Luambano na kusema hana nia ya kuendelea kumshitaki.
Baada ya kusema hayo Hakimu Luambano, alisema mshitakiwa anamwachia huru
Awali Wakili wa Serikali Ashura Mnzava, alidai shauri lilipelekwa kwa kutajwa ambapo DPP hana nia ya kuendelea kumshitaki mshitakiwa hivyo anayaondoa mashitaka yote dhidi yake.
Kambangwa alikuwa anakabiliwa na mashitaka manne likiwemo kusababishia Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) hasara ya sh. bilioni 188.9 kwa kupitia mashine ya kielekroniki.
Mshitakiwa Kambangwa alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Desemba 7, mwaka 2018 ambapo alisomewa mashitaka katika kesi ya uhujumu uchumi .
Inadaiwa mshtakiwa anakabiliwa na mashitaka manne aliyoyatenda katika siku tofauti kati ya Juni Mosi , mwaka 2016 na Novemba 2, mwaka 2018
Alidai katika mshitaka ya kwanza, Kambangwa alijifanya kama mtu aliyesajiliwa kuwa mlipa kodi ya ongezeko la thamani (VAT)
Alidai katika tarehe tofauti kati ya Juni Mosi, mwaka 2016 na Novemba 2, mwaka 2018 maeneo ya jiji la Dar es Salaam mshitakiwa alijifanya kuwa amesajiliwa kukusanya kodi ya VAT sh. 188,928,752,166 kwa kujifanya anakusanya fedha hizo kwa niaba ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Katika mashitaka ya pili, alidai Juni Mosi, 2016 na Novemba 2, mwaka 2018 Kambangwa kwa udanganyifu alitumia mashine ya kieletroniki ya EFD yenye namba 03TZ842011315 iliyosajiliwa kwa jina la Kampuni ya Abraham's Group LTD kukwepa kodi ya VAT yenye thamani ya fedha hiyo.
Katika mshitaka ya utakatishaji fedha, tarehe na kipindi hicho, maeneo ya jiji la Dar es Salaam alijipatia au kujimilikisha fedha hizo alizozipata kutokana na makato ya kodi ya VAT ambazo zilipaswa kutolewa kwa Kamishna wa TRA na mshitakiwa huyo alipaswa kujua kuwa fedha hizo bi zao la kosa la ukwepaji kodi.
Ilidaiwa katika tarehe tofauti kati ya Juni Mosi, mwaka 2016 na Novemba 2, mwaka jana maeneo ya Dar es Salaam kwa vitendo vya makusudi vya kukwepa kodi alitumia mashine ya kieletroniki ya EFD na huku akijua kwamba hajasajiliwa kama mlipakodi ya VAT aliisababishia TRA hasara ya sh. 188,928,752,166
Zaidi, soma;
1). Mustapha Kambangwa afikishwa mahakamani kwa mashtaka manne likiwemo la kukwepa kodi na kujipatia Sh.bilioni 188.9 kupitia mashine ya kieletroniki (EFD
DPP aliwasilisha hati hiyo leo Mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Joseph Luambano na kusema hana nia ya kuendelea kumshitaki.
Baada ya kusema hayo Hakimu Luambano, alisema mshitakiwa anamwachia huru
Awali Wakili wa Serikali Ashura Mnzava, alidai shauri lilipelekwa kwa kutajwa ambapo DPP hana nia ya kuendelea kumshitaki mshitakiwa hivyo anayaondoa mashitaka yote dhidi yake.
Kambangwa alikuwa anakabiliwa na mashitaka manne likiwemo kusababishia Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) hasara ya sh. bilioni 188.9 kwa kupitia mashine ya kielekroniki.
Mshitakiwa Kambangwa alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Desemba 7, mwaka 2018 ambapo alisomewa mashitaka katika kesi ya uhujumu uchumi .
Inadaiwa mshtakiwa anakabiliwa na mashitaka manne aliyoyatenda katika siku tofauti kati ya Juni Mosi , mwaka 2016 na Novemba 2, mwaka 2018
Alidai katika mshitaka ya kwanza, Kambangwa alijifanya kama mtu aliyesajiliwa kuwa mlipa kodi ya ongezeko la thamani (VAT)
Alidai katika tarehe tofauti kati ya Juni Mosi, mwaka 2016 na Novemba 2, mwaka 2018 maeneo ya jiji la Dar es Salaam mshitakiwa alijifanya kuwa amesajiliwa kukusanya kodi ya VAT sh. 188,928,752,166 kwa kujifanya anakusanya fedha hizo kwa niaba ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Katika mashitaka ya pili, alidai Juni Mosi, 2016 na Novemba 2, mwaka 2018 Kambangwa kwa udanganyifu alitumia mashine ya kieletroniki ya EFD yenye namba 03TZ842011315 iliyosajiliwa kwa jina la Kampuni ya Abraham's Group LTD kukwepa kodi ya VAT yenye thamani ya fedha hiyo.
Katika mshitaka ya utakatishaji fedha, tarehe na kipindi hicho, maeneo ya jiji la Dar es Salaam alijipatia au kujimilikisha fedha hizo alizozipata kutokana na makato ya kodi ya VAT ambazo zilipaswa kutolewa kwa Kamishna wa TRA na mshitakiwa huyo alipaswa kujua kuwa fedha hizo bi zao la kosa la ukwepaji kodi.
Ilidaiwa katika tarehe tofauti kati ya Juni Mosi, mwaka 2016 na Novemba 2, mwaka jana maeneo ya Dar es Salaam kwa vitendo vya makusudi vya kukwepa kodi alitumia mashine ya kieletroniki ya EFD na huku akijua kwamba hajasajiliwa kama mlipakodi ya VAT aliisababishia TRA hasara ya sh. 188,928,752,166
Zaidi, soma;
1). Mustapha Kambangwa afikishwa mahakamani kwa mashtaka manne likiwemo la kukwepa kodi na kujipatia Sh.bilioni 188.9 kupitia mashine ya kieletroniki (EFD