MWENYEKITI wa Chama cha United Peoples' Democratic (UPDP), Fahmi Dovutwa, ametoa kauli yenye ukakasi kwa Rais Jakaya Kikwete, akimshauri ajiuzulu urais. Dovutwa alisema, Rais Kikwete hana sababu za kuendelea kubaki tena madarakani, kwa madai kuwa ameshindwa kumaliza tatizo la rushwa nchini.
"Mh. Kikwete wewe ni rais wa nchi, unavyolia rushwa imejaa ndani ya CCM, wakati wewe ndiye mwenyekiti wa chama hicho tawala, unashangaza watu," alisema.
Dovutwa ambaye aliwahi kugombea urais mwaka 2010, aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na Mtanzania, kuhusu uchaguzi wa CCM kutawaliwa na rushwa.
Mwanasiasa huyo ambaye alimuunga mkono Rais Kikwete katika uchaguzi huo, alisema amelazimika kusitisha ‘uswahiba' na Rais Kikwete, kwa madai kuwa amepoteza sifa.
Dovutwa alisema, hivi karibuni Rais Kikwete aliwashangaza Watanzania wengi, pale alipoibuka na kulalamika kukithiri kwa rushwa ndani ya chama chake.
"Mh. Kikwete wewe ni rais wa nchi, unavyolia rushwa imejaa ndani ya CCM, wakati wewe ndiye mwenyekiti wa chama hicho tawala, unashangaza watu," alisema.
Dovutwa ambaye aliwahi kugombea urais mwaka 2010, aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na Mtanzania, kuhusu uchaguzi wa CCM kutawaliwa na rushwa.
Mwanasiasa huyo ambaye alimuunga mkono Rais Kikwete katika uchaguzi huo, alisema amelazimika kusitisha ‘uswahiba' na Rais Kikwete, kwa madai kuwa amepoteza sifa.
Dovutwa alisema, hivi karibuni Rais Kikwete aliwashangaza Watanzania wengi, pale alipoibuka na kulalamika kukithiri kwa rushwa ndani ya chama chake.