Dotto Bulendu: Ni kweli adui mkubwa wa maendeleo ni vyama vya upinzani kiasi kwamba tunatamani kuvifuta?

Abery

Member
Oct 18, 2016
25
59
Ameandika Mwandishi Dotto Bulendu

Kabla hatujaviona vyama vyingi ni kero na vinachelewesha Maendeleo tujiulize kwanza maswali yafuatayo;

1.Ubinafsishaji wa mashirika ya umma kwa bei ya kutupwa kulifanyika kwa sababu ya vyama vingi hivyo tuhakikishe vinakufa?

2.Kufa kwa reli ya kati kulisababishwa na vyama vingi hivyo inabidi tuhakikishe tunavifuta?

3.Kuuzwa kwa bei ya hasara kwa benki ya NBC kulitokana na vyama vingi hivyo tuhakikishe vinakufa ili tuirejeshe benki yetu?

4.Kuuzwa kwa hisa za shirika la simu la TTCL kwa bei inayotajwa ya hasara kulitokana na vyama vingi? na hivyo inabidi tuhakikishe vinafutika?

5.Kufa kwa viwanda na mashamba makubwa yaliyoasisiwa tangu wakati wa ukoloni kulisababishwa na vyama vingi vya siasa na hivyo tuhakikishe vinakufa?

5.Shule za Serikali kufanya vibaya na sasa wazazi wenye uwezo hawawapeleki tena watoto wao kwemye shule za serikali kumesababishwa na hivi vyama vingi hivyo tuhakikishe hakuna Diwani wala Mbunge wa upinzani?

6.Mikataba ya hovyo na hasara kwenye sekta ya madini iliyosababisha vifo vya watu huko Nyamongo,Kahama,Nzega n.k kulisababishwa na vyama vingi hivyo tuhakikishe halmashauri zetu,ndani ya bunge hakuna mwakilishi kutoka vyama vya upinzani?

7.Tanzania kufanya vibaya kwenye medani ya michezo kumesababishwa na hivi vyama vingi na hivyo yeyote anayeunga mkono vyama vya upinzania anatakiwa kuitwa siyo mzalendo?

8.Viwanda kutangaza kufunga uzalishaji kutokana na kukosekana kwa sukari kumesababishwa na vyama vingi vya siasa?

9.Tangu mwaka 2015,vijana wengi wahitimu wa vyuo vya kati na vyuo vikuu kukaa mtaani bila ajira kumesababishwa na vyama vingi hivyo tuhakikishe vinakufa ili ajira zifunguke?

10.Nyongeza ya misharaha kwa watumishi wa umma imekuwa inasuasua kutokana na vyama vingi vya siasa?

11.Wafanyakazi hewa serikalini walioisababishia hasara kubwa serikali kwa muda mrefu ni kutokana na vyama vingi na hasa mikutano ya vyama vya siasa?hivyo tufute mikutano yote ya vyama vya upinzani ili kuhakikisha hakuna watumishi hewa?

12.Shirika la ndege ambalo miaka 35 iliyopita lilikuwa na ndege zaidi ya kumi,zikatoweka mpaka kubaki na ndege chini ya tano,kulitokana na hivi vyama vya upinzani?hivyo tuvizike ili shirika la ndege liwe na ndege za kutosha?

13.Watu wakiwemo wabunge na mawaziri waliwahi kujigawia pesa za umma kutoka akaunti ya Escrow na kuisababishia serikali hasara,hiyo ilitokana na Uwepo wa vyama vya upinzania hivyo tuvifute ili Escrow isije jirudia?

14.Kuliibuka tuhuma za Rushwa za EPA na Meremeta,tuhuma hizi zilitokana na vyama vingi?hivyo tuvifute ili tusipate tena tuhuma za Epa na Meremeta?

15.Kuna kiongozi akijua kabisa yeye ni mtumishi wa umma,alijiuzia mgodi wa Kiwira tena kwa bei ya hovyo,alifanya hivyo kwa sababu ya uwepo wa vyama vingi hivyo tuhakikishe hakuna cha diwani wala mbunge wa kutoka upinzani kwenye halmashauri zetu na bungeni?wabaki wa chama kimoja?

16.Kuna waziri aliwahi ingia mkataba na kampuni ga Barrick kwenye mgodi wa Buzwagi ,je huyo waziri aliingia mkataba huo kwa sababu ya hivi vyama vingi?

Najaribu kuwaza tu kwa kina.
 
Taifa la ajabu sana hili mwenyekiti wa ccm na polepole toka mwaka 2015 waingie madarakani wamewekeza nguvu yote kupambama na vyama vya upinzani ambayo ndio ajenda kuu ya chama tawala, upinzan hua moyoni mwa watu sio chama mtaua chadema, cuf au act hamuwezi kuua hisia za watu kutaka mabadiliko movement zitaendelea kwa namna nyingine tena.

Ukiambiwa hii nchi inaongozwa na maprofesa na madokta utashangaa sana mambo yanayofanyika ya ajabu sana ambayo hata lusinde hawezi kuyafanya unaratibu kupiga risasi binadamu mwenzio kisa amekukosoa hatari sna hii.
 
Ukugeuza upande wa pili wa kalamu yako unakuta vyama vya upinzani navyo vinafanya hayohayo nje ya mfumo
Mifano
Zitto mwingamba na kitila walifukuzwa CDM kialali?
2/ hati chafu za CIG zinazopata vyama vya upinzani sio matumizi mabaya ya fedha za umma?
3/ kukaa madarakani kwa viongoz wakuu wa upinzani ni democracy ndani ya vyama?
4/ mali za vyama vya upinzani kwa kias gani vinatenganishwa na mali binafsi za viongozi wakuu wa upinzani?
[HASHTAG]#UTAKUTA[/HASHTAG] MADUDU MENGI YA AJABU ATA MIMI YANANICHOSHA KU MENTION
 
Ukugeuza upande wa pili wa kalamu yako unakuta vyama vya upinzani navyo vinafanya hayohayo nje ya mfumo
Mifano
Zitto mwingamba na kitila walifukuzwa CDM kialali?
2/ hati chafu za CIG zinazopata vyama vya upinzani sio matumizi mabaya ya fedha za umma?
3/ kukaa madarakani kwa viongoz wakuu wa upinzani ni democracy ndani ya vyama?
4/ mali za vyama vya upinzani kwa kias gani vinatenganishwa na mali binafsi za viongozi wakuu wa upinzani?
[HASHTAG]#UTAKUTA[/HASHTAG] MADUDU MENGI YA AJABU ATA MIMI YANANICHOSHA KU MENTION
Uliyoyasema nikweli mkuu.
Wanasiasa wajitathimini, mabadiliko yanahitajika hakika.
 
Tanzania tulipata bahati ya kutengeneza kamba ya kuwafunga na kuwabana waliofanya namba 1 hadi 16 ila KATIBA MPYA lakini wale wale waliokosea ndio wakawa mafundi wa kutengeneza Rasimu ya Katiba inayopendekezwa.

Mfumo wa kufikiria tofauti na wakubwa ni kosa kwa watu wenye low self esteem hapa Tanzania.

Kuwa na viongozi wenye hatia na hofu ndani ni hatari kuliko kupata mlipuko wa volcano.
Kama wewe ni baba wa watoto na unaona hali ya kinachoendelea, utaogopa pale atakapomaliza Chuo Kikuu na kupata shahada ya sheria LLB na kujiunga na CUF na baada ya siku unasikia amepota na ameokotwa akiwa ndani ya mfuko wa sandarusi;

Ndipo utakapolia na kusaga meno wakati ulikuwa na nafasi nzuri ya kuzuia hayo yote
 
Hakika inastajabisha sana nadhan wanaona wanabanwa banwa kufanya udhalimu wao nanjia pekee nikumuondoa anayekufutilia kila unapo taka kukwapua, kuiba kufisad, tukumbuke vyama vinavyoitwa vya upinzan nisawa na taa kwa nyumba mwivi akija hutamani azime taa ndipo apate nafasi nzur zaidi yakuiba kwa nafas, mhimu tusikubali kuzimiwa taa yetu kukawa na giza hakika tukifanya kosa hilo taa itakapo washwa tutakuta kila kitu kishaondolewa
 
Ukugeuza upande wa pili wa kalamu yako unakuta vyama vya upinzani navyo vinafanya hayohayo nje ya mfumo
Mifano
Zitto mwingamba na kitila walifukuzwa CDM kialali?
2/ hati chafu za CIG zinazopata vyama vya upinzani sio matumizi mabaya ya fedha za umma?
3/ kukaa madarakani kwa viongoz wakuu wa upinzani ni democracy ndani ya vyama?
4/ mali za vyama vya upinzani kwa kias gani vinatenganishwa na mali binafsi za viongozi wakuu wa upinzani?
[HASHTAG]#UTAKUTA[/HASHTAG] MADUDU MENGI YA AJABU ATA MIMI YANANICHOSHA KU MENTION
Hata ubongo wako umejaa madudu mengi ndio maana umeyamwaga baadhi hapa ambayo hayalandani na ya mleta hoja! Unashangaza kiukweli hasa kama umri wako unakutambulisha kama kijana lakini unawaza kizee! Msome tena Bulendu uipate mantiki ya hoja yake kisha upime kama kweli kuvifuta vyama vya upinzani, kuua viongozi wa upinzani na kununua viongozi wa upinzani kutaongeza kasi ya ujenzi wa viwanda na kuuboost uchumi au kuna jambo linafichwa ili umma usijue na kuhoji?
 
Na haya mauaji ya viongozi na wanachama wa vyama pinzani na kupotezwa kwa wakosoaji wa utawala wa Sizonje, ni njama za vyama pinzani?
 
Ukugeuza upande wa pili wa kalamu yako unakuta vyama vya upinzani navyo vinafanya hayohayo nje ya mfumo
Mifano
Zitto mwingamba na kitila walifukuzwa CDM kialali?
2/ hati chafu za CIG zinazopata vyama vya upinzani sio matumizi mabaya ya fedha za umma?
3/ kukaa madarakani kwa viongoz wakuu wa upinzani ni democracy ndani ya vyama?
4/ mali za vyama vya upinzani kwa kias gani vinatenganishwa na mali binafsi za viongozi wakuu wa upinzani?
[HASHTAG]#UTAKUTA[/HASHTAG] MADUDU MENGI YA AJABU ATA MIMI YANANICHOSHA KU MENTION
Haya yameathiri vipi maisha ya Watanzania walio na vyama na wasio na vyama kwa ujumla wao!?!?
 
Back
Top Bottom