Dotto Bulendu, kipindi chako cha “Jicho letu ndani ya habari” kinapoteza maana kwa kumshirikisha Pascal Mayalla

nguruka wa kig0ma

JF-Expert Member
Jan 16, 2020
2,946
2,929
Niende moja kwa moja kwenye mada.

Wakati kinaanza kipindi chako tajwa hapo juu, mimi binafsi nilikipenda sana. Siyo mimi tu, niliona sehemu nyingi nilizotembelea watu wenye akili kubwa, uelewa mpana na wenye heshima wakiamka asubuhi mapema kukusikiliza ukiendesha kipindi, na kusikiliza hoja kinzani kutoka kwa washiriki uliowaalika.

Kipindi chako kilifanana na Malumbano ya hoja kilichokuwa kikirushwa na ITV kila Alhamisi na kuvutia watu wengi, ambacho kwa sasa kimepoteza maana na kukimbiwa na watu wenye weledi kukisikiliza hata kwenda kujumuika.

Nakumbuka, watu walitoka mikoani kwenda kujumuika, na makundi kukusanyika kwenye runinga maeneo mbalimbali. KWASASA KIMEPOTEZA MAANA YA KULUMBANA ILI KUTENGENEZA HOJA YA PAMOJA.

Naamini Serikali iliyopita ilikuwa inachukua vitu kwenye kipindi kile. Kipindi kile kilikuwa kama bunge, kasoro kusoma bajeti tu.

Jicho letu ndani ya habari kilikusanya watu kila Jumamosi, kusikiliza wataalam wa habari na wanasheria wakifukua madini, na wanasiasa kipigana vijembe. KIPINDI KILINOGA.

Nasikitika kusema, baada ya kutishwa na watawala ukaanza kualika watu wa upande mmoja, au watu kama Pascal Mayalla UMEKIHARIBU KIPINDI NA SASA KINAPENDWA NA UPANDE MMOJA TU, NA WASIO NA UWEZO WA KUPAMBANUA MAMBO.

Kumshirikisha Mayalla kwenye jicho letu ndani ya habari, umekiua kipindi. Mayalla anapotosha sana umma kwa kigezo cha u-nguli wa habari na kuijua sheria. Na kwakuwa watanzania wengi ni mbumbumbu, wanapotezwa.

Wenye akili na walioamka toka ujingani hawaangalii na kusikiliza jicho letu ndani ya habari siku hizi.

Mbona ulionekana ulionekana kuvaa ujasiri huko siku za nyuma, ujasiri umeupeleka wapi? Hata thread zako unazoandika humu huwa na ujasiri na nguvu kubwa, UMEUPELEKA WAPI UJASIRI?
DOTTO JITAFAKARI UPYA.

Karibuni,



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani Chadema bwana mpo km watoto wadogo

Mnataka Chadema ipambwe wakati sacos imejiozea imechokwa?

Chadema kufa kabla ya Uchaguzi Mkuu ni aibu kubwa
Siyo wote wasioramba viatu ni cdm.
Ivi una muda wa kuwa na mkeo kweli, au umehamia rumumba na mkeo atahudumiwa?
Maana hakuna thread inayokupi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pascal Mayalla amepotosha kitu gani bwashee?

Unapomtuhumu mtu weka na ushahidi badala ya blah...blah!
Katiba inasemaje juu ya kukoma kwa ubunge kwa mbuge aliyevuliwa ubunge na chama chake?
Au spika yupo juu ya katiba?

Ninachojua mamlaka ya kiongozi yeyote inatokana na katiba, Mayalla anasema inapotokea marumbano basi kwa mamlaka aliyopewa Rais, spika nk, anawezatoa maamuzi ya mwisho.

Hii inaonesha hata nje ya katiba au kanuni.
Huoni hapo anapotosha?
Au na wewe ni walewale wa bahi sokoni?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katiba inasemaje juu ya kukoma kwa ubunge kwa mbuge aliyevuliwa ubunge na chama chake?
Au spika yupo juu ya katiba?

Ninachojua mamlaka ya kiongozi yeyote inatokana na katiba, Mayalla anasema inapotokea marumbano basi kwa mamlaka aliyopewa Rais, spika nk, anawezatoa maamuzi ya mwisho.

Hii inaonesha hata nje ya katiba au kanuni.
Huoni hapo anapotosha?
Au na wewe ni walewale wa bahi sokoni?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mayala ili kutetea uvunjaji wa haki, anabumba vifungu vipya vya kupingana na katiba. Exclusive powers nje ya katiba ya NCHI? Hiyo njaa yake ndio yammaliza.
 
Wivu utakuua mzee,sema husikii kikizumzwa unachopenda kukisikia,zaidi ya yote hongera pascal mayalla kwa nyuzi humu jf na uchambuzi mujarabu huko star tv.
 
Kwa utawala huu no ngumu sana kuwa vocal against the rulers, mimi nawaelewa hawa jamaa, japo wapo wachache bado wana audacity ya kuongea kwa unyoofu.
 
Mkuu uko Sawa kabisa, Watu tunataka Challenges za maana,

Hoja hoja kweli, sio blahblah, Haya mavyama tukiyaendekeza ndio tunalea majambazi pia

Vyama vichemke ndani Kwa ndani, vyenyewe Kwa vyenyewe, mtu Kwa mtu bila kulindana na bila kuleana, Tunataka Taifa lenye uwiano Sawa, siasa Safi ndani ya Vyama hata nje,

Paschal, hatutaki Vioja tunataka hoja ambazo zitakuwa na manufaa ya nchi yetu, na Kwa pande zote
 
Kwa taarifa yako Mayalla kaongeza watazamaji wengi sana kufuatilia hicho kipindi, zamani wageni wengi walikuwa waandishi na wahariri tu.

Lakini sasa viongozi Wakuu wa serikali wengi wanaaalikwa japo majibu yao yanakuwa ya kisiasa zaidi.

Sema wafuasi wa Chadema hampendagi Changamoto, mmezoea kusifiwa tu.

Hamna tofauti na serikali ya Magufuli.

Mayalla acha kuficha ujumbe kwenye maandiishi wengi hawakuelewi kabisa.

Niliona hata siku unahojiana na Mwakyembe, uliikosoa Wizara nzima tena kwa kutaja majina kabisa. hadi Mwakyembe akasema uwe unawasiliana nae moja kwa moja.
 
Umemtafsiri paskali yeye huwa menzani yake inalala pande zote sio ya wafuasi watiifu au ya fatuma karume,kigogo,mange haioni mazuri hata wewe pia umeathiriwa na fikra za kuwa postive tu!
 
Pascal Mayalla amepotosha kitu gani bwashee?

Unapomtuhumu mtu weka na ushahidi badala ya blah...blah!
Pasco Mayalla yupo kutetea kila ujinga wa hii serikali. Kwa sasa ana njaa mnoo. Ile kampuni yake ya PPR inaelekea kufa kifo cha Mende, kwa sasa Mayala anaitafuta nafasi ya Grayson Msigwa kwa hali na mali.

Kama uamini wewe subiri.
 
Pasco Mayalla yupo kutetea kila ujinga wa hii serikali. Kwa sasa ana njaa mnoo. Ile kampuni yake ya PPR inaelekea kufa kifo cha Mende, kwa sasa Mayala anaitafuta nafasi ya Grayson Msigwa kwa hali na mali.

Kama uamini wewe subiri.

Japo Mayalla anaonekana mjivuni wa kujua lakini anamzidi Greyson Msigwa kwa Mbali kabisa, Msigwa anapwaya tuseme ukweli ikulu imekosa kichwa cha maana kwa sasa kwenye habari. Hata hivo Paschal inabidi uandishi wako humu JF uwe wenye umakini, nadhifu na mnyoofu, uache mzamzaha sio wote wataelewa mizaha wengi hawana upeo wa kupembua mzaha.
 
Back
Top Bottom