Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,001
- 112,637
Chini hapo ni video za mkusanyiko wa watu waliokuwa wanaapia kuwa Donald Trump kamwe hatoweza kuja kuwa rais wa Marekani.
Nami nakiri kuwa nilikuwa mmoja wa hao watu licha ya kwamba uchaguzi wa mwaka huu ulikuwa ni uchaguzi wa mabadiliko [change election] ambao hutokea mara nyingi kila baada ya miaka 8 ambapo rais wa chama kimoja anakuwepo madarakani kwa muda wote huo wa mihula miwili.
Hivyo, kwa kufuata utamaduni huo wa chaguzi za kisiasa, mwaka huu ulipaswa kuwa ni mwaka wa chama cha Republican kushinda uchaguzi mkuu. Lakini kwa vile ambavyo mgombea wa chama hicho alivyokuwa akijinadi, maoni ya watu wengi yalikuwa kwamba hawezi kabisa kushinda.
Ila uzuri wa mambo ni kwamba kura na maoni ya watu yanayojalisha na kuhesabika ni ya wale ya watu waendao kupiga kura siku ya uchaguzi.
Kura za maoni na maoni ya wataalamu [mimi nawaita wajuaji] hayajalishi na wala hayahesabiki kabisa.
Na ndicho haswa kilichotokea siku ya tarehe 8 mwezi Novemba, mwaka 2016 ambapo Bw. Trump, licha ya watu wengi kuona kuwa hawezi kumshinda Bi. Clinton, alijishangaza hata yeye mwenyewe kwa kuibuka kidedea katika uchaguzi mkuu huo wa taifa bora kabisa kuwa kutokea katika uhai wa mwanadamu.
Ingawa sikuwa namuunga mkono, lakini nilifurahi sana. Kilichonifurahisha kuhusu huo ushindi wake ni kitendo chake cha kuwatia kidole cha kati wale wote waliokuwa wanamdharau, kumkebehi, kumkejeli, na hata kumzushia mambo lukuki.
Nilifurahi mno kwa sababu karibu dunia nzima, vyombo karibu vyote vya habari, hususan vile vya ndani vya Marekani, vilionyesha upendeleo wa wazi kabisa dhidi yake. Yaani viliamua kuitupilia mbali kabisa miiko yote ya uandishi wa habari na kuamua kumuunga mkono yule bibi na kumpinga Trump.
Ila licha ya vigingi vyote hivyo, jamaa akaibuka juu.
Shikamoo Bw. Donald J. Trump.
Nguruvi3 El Jefe The Boss
Nami nakiri kuwa nilikuwa mmoja wa hao watu licha ya kwamba uchaguzi wa mwaka huu ulikuwa ni uchaguzi wa mabadiliko [change election] ambao hutokea mara nyingi kila baada ya miaka 8 ambapo rais wa chama kimoja anakuwepo madarakani kwa muda wote huo wa mihula miwili.
Hivyo, kwa kufuata utamaduni huo wa chaguzi za kisiasa, mwaka huu ulipaswa kuwa ni mwaka wa chama cha Republican kushinda uchaguzi mkuu. Lakini kwa vile ambavyo mgombea wa chama hicho alivyokuwa akijinadi, maoni ya watu wengi yalikuwa kwamba hawezi kabisa kushinda.
Ila uzuri wa mambo ni kwamba kura na maoni ya watu yanayojalisha na kuhesabika ni ya wale ya watu waendao kupiga kura siku ya uchaguzi.
Kura za maoni na maoni ya wataalamu [mimi nawaita wajuaji] hayajalishi na wala hayahesabiki kabisa.
Na ndicho haswa kilichotokea siku ya tarehe 8 mwezi Novemba, mwaka 2016 ambapo Bw. Trump, licha ya watu wengi kuona kuwa hawezi kumshinda Bi. Clinton, alijishangaza hata yeye mwenyewe kwa kuibuka kidedea katika uchaguzi mkuu huo wa taifa bora kabisa kuwa kutokea katika uhai wa mwanadamu.
Ingawa sikuwa namuunga mkono, lakini nilifurahi sana. Kilichonifurahisha kuhusu huo ushindi wake ni kitendo chake cha kuwatia kidole cha kati wale wote waliokuwa wanamdharau, kumkebehi, kumkejeli, na hata kumzushia mambo lukuki.
Nilifurahi mno kwa sababu karibu dunia nzima, vyombo karibu vyote vya habari, hususan vile vya ndani vya Marekani, vilionyesha upendeleo wa wazi kabisa dhidi yake. Yaani viliamua kuitupilia mbali kabisa miiko yote ya uandishi wa habari na kuamua kumuunga mkono yule bibi na kumpinga Trump.
Ila licha ya vigingi vyote hivyo, jamaa akaibuka juu.
Shikamoo Bw. Donald J. Trump.
Nguruvi3 El Jefe The Boss