Dogo katusua au utapeli?

UKAWA2

JF-Expert Member
Apr 22, 2014
2,182
1,970
Huyu ni shemeji yangu(mdogo wa mke wangu),alihitimu kidato cha sita na akajiunga na jeshi la kujenga taifa kwa mujibu wa sheria akahitimu mafunzo mwaka jana.
Mwanzonimwa wiki hii alipigia simu na mtu aliyejitambulisha kuwa ni mkuu wake wa kikosi alipofanyia mafunzo na akamjulisha kuwa kuna nafasi za kazi za kujiunga na JWTZ lakini zipo katika kambi nyingine(Hapa sitazitaja hizo kambi) na akampa namba ya simu ya mtu aliyeko huko kwenye kambi yenye hizo nafasi.

Baada ya kumpigia,huyo mtu alimwambia kuwa ni kweli na yeye ni miongoni mwa waliobahataika kupata hiyo nafasi na anatakiwa kufika kambini hapo haraka ili kuchukua vifaa vya mafunzo na kuelekea katika mafunzo ambayo tena yatakuwa yanafanyikia kambi nyingine(Kumbuka mpaka hapo zimeshafika kambi tatu ukianzia na pale simu ya mwanzo ilipotoka).

Mashaka yakaanza pale alipomwabia kuwa anatakiwa kwenda na shilingi 350,000/=kwa ajili ya gharama ya vifaa vya mafunzo.
Je,kwa wajuzi wa haya mambo,hapo kuna kazi kweli au ndo jama na wao wantekeleza kauli mbiu ya HAPA KAZI TU?
 
Mwambie apige simu kwa amiri jeshi mkuu haraka iwezekanavyo ili kuepuka kupigwa changa la macho. Ajira za jeshi huwa watu hawaambiwi waende na pesa kwa ajili kununulia vifaa.
 
Huyu ni shemeji yangu(mdogo wa mke wangu),alihitimu kidato cha sita na akajiunga na jeshi la kujenga taifa kwa mujibu wa sheria akahitimu mafunzo mwaka jana.
Mwanzonimwa wiki hii alipigia simu na mtu aliyejitambulisha kuwa ni mkuu wake wa kikosi alipofanyia mafunzo na akamjulisha kuwa kuna nafasi za kazi za kujiunga na JWTZ lakini zipo katika kambi nyingine(Hapa sitazitaja hizo kambi) na akampa namba ya simu ya mtu aliyeko huko kwenye kambi yenye hizo nafasi.

Baada ya kumpigia,huyo mtu alimwambia kuwa ni kweli na yeye ni miongoni mwa waliobahataika kupata hiyo nafasi na anatakiwa kufika kambini hapo haraka ili kuchukua vifaa vya mafunzo na kuelekea katika mafunzo ambayo tena yatakuwa yanafanyikia kambi nyingine(Kumbuka mpaka hapo zimeshafika kambi tatu ukianzia na pale simu ya mwanzo ilipotoka).

Mashaka yakaanza pale alipomwabia kuwa anatakiwa kwenda na shilingi 350,000/=kwa ajili ya gharama ya vifaa vya mafunzo.
Je,kwa wajuzi wa haya mambo,hapo kuna kazi kweli au ndo jama na wao wantekeleza kauli mbiu ya HAPA KAZI TU?
Matapeli Bongo hawaishi na kila siku wanakuja na mbinu mpya.
 
Halafu tuwe serious jeshi gani linahitaji hela kujiunga??

Kinyume chake iwe njia isiyo halali

Matapeli
 
Nimepitia mimi huko baada ya kumaliza kidato cha sita mujibu wa sheria,makao makuu ya jeshi hutuma watu wao kwenda katika hizo kambi kuwafanyisha usaili wa kujiunga na jwtz kwa wale waliosoma masomo ya sayansi tu kabla ya kumaliza kozi! wakisha maliza kozi na kurudi nyumbani hupigiwa simu kwa wale waliofanya usaili,kutoka makao makuu ya jeshi na huwambiwa sehemu gani waende kukutana kwa wotewaliofanya usaili na taratibu nyingine zinaendelea.lakini hakuna pesa yeyote inayotumika zaidi ya ile utakayojigharamia kutoka mkoa unaoishi kwenda sehemu husika.pia hakuna fedha kwa ajili ya vifaa vya mafunzo,vifaa hutolewa bure kikosini.ila muulize vizuri ilikuwaje hadi akapigiwa simu na kupewa maelekezo hayo,aliongea na huyo mkuu wa kikosi akiwa bado hajamaliza kozi kwamb anavutiwa kujiunga na jwtz au?
 
Ukiitwa jeshini unaenda wewe kama wewe ukifika kambini kuanzia maradhi usafiri chakula vitendea kazi ni juu yao. Hao ni matapeli
 
Yani ndugu asijaribu kutuma fedha Mimi walinipigia jamaa wakajitambulisha kuwa Ni wakuu wa kikosi kutokea kambi ya Dodoma na walitaka kiasi cha fedha kwa kweli baada ya kufuatilia walikuwa matapeli kuweni makini
 
Back
Top Bottom