DODOMA: Zahanati hufungwa hadi wiki mbili kila wakati mganga anaposafiri

FikraPevu

JF-Expert Member
Jan 2, 2010
303
236


GRACE Machidya, mkazi wa Kijiji cha Malolo katika Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, anahangaika kutafuta usafiri wa bodaboda ili impeleke katika zahanati ya Al Jazeera iliyoko Ruaha Mbuyuni wilayani Kilolo katika Mkoa wa Iringa, umbali wa takriban kilometa 25 kutoka kijijini hapo, kumwahisha mwanaye wa miaka miwili aliye mgonjwa.

Mwanaye huyo ana homa kali na pia anaharisha na msaada ambao alitarajia kuupata katika zahanati ya Kijiji cha Malolo hapo baada ya kukuta imefungwa kwa siku ya tatu sasa kutokana na ofisa afya kusafiri.


“Ningejua ningekwenda tu moja kwa moja, kwa sababu tumezowea kutibiwa nje ya kijiji, zahanati gani kila siku imefungwa hakuna huduma?” anasema kwa masikitiko.

Lakini anaieleza FikraPevu | JamiiForums' News Site kwamba, hata kama zahanati hiyo ingekuwa wazi, huenda mwanaye asingeweza kupata huduma kwa sababu hata dawa za malaria tu, ugonjwa unaoua watoto wengi nchini Tanzania, ni shida kupatikana.

Hawezi kutumia usafiri wa gari kwa sababu huduma hiyo haipo, hivyo njia pekee ni kutafuta bodaboda ambayo ataikodi kwa Shs. 10,000 ili imfikishe huko zahanati.

"Hii ni mara ya pili nakuja hapa, mara ya kwanza nilikuja wiki tatu zilizopita, zahanati ilikuwa imefungwa ambapo niliambiwa ofisa afya alikuwa amefuata dawa wilayani, mjini Mpwapwa, sikupata huduma nikalazimika kwenda Ruaha Mbuyuni. Leo nimeambiwa kwamba amepeleka ripoti ya utendaji huko Halmashauri,” anasema.

Hata hivyo, anasema ni gharama kubwa kwenda Ruaha, kwani si kila mtu atakayekuwa na uwezo wa kukodi bodaboda kwa Shs. 20,000 kwa maana ya kwenda na kurudi, achilia mbali uhakika na usalama wa usafiri huo ulivyo, hasa unapokuwa na mgonjwa mahtuti.

Ikiwa mpakani kabisa mwa mikoa ya Dodoma, Iringa na Morogoro, zahanati hiyo ya Malolo ndiyo pekee kwa wananchi wa kijiji hicho chenye wakazi 2,600 kutoka katika vitongoji sita, na iko umbali wa kilometa 155 kutoka Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa, ambapo siyo tu usafiri hakuna kutoka hapo, bali njia yenyewe imejaa makorongo pamoja na mawe yakiambatana na milima.

FikraPevu ilishuhudia zahanati hiyo ikiwa imefungwa, ambapo baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Malolo walisema, hiyo ilikuwa siku ya tatu tangu ofisa afya, Elias Mlwande, aliposafiri.

“Hapa ni kawaida, wakati mwingine inaweza kufungwa hadi wiki mbili, tumeshazowea kwenda kutibiwa huko Morogoro na Iringa ambako ni karibu na kuna usafiri na huduma za uhakika kuliko hapa kijijini au kwenda Mpwapwa,” anasema Julius Mapalilo, mkazi wa kijiji hicho.

Mapalilo anasema, wakati mwingine hulazimika kuvuka mto kwenda Kijiji cha Malolo ya wilayani Kilosa ama kwenda zahanati ya Al Jazeera Ruaha Mbuyuni au Hospitali ya Misheni ya Mtandika wilayani Kilolo mkoani Iringa.

“Siyo ajabu, tunakwenda pia Hospitali ya Misheni Ilula au Hospitali ya Mtakatifu Kizito ya Mikumi, ambayo ni ya misheni pia. Huko kuna huduma nzuri na usafiri ni wa uhakika,” anaongeza Mapalilo.

Uchunguzi wa FikraPevu umebaini pia kwamba, ni vigumu kufanya kazi katika kijiji hicho kutokana na changamoto ya miundombinu, hususan usafiri, licha ya kwamba kama kuna mgonjwa mahututi gari la wagonjwa linaweza kuitwa kutoka Mpwapwa.

Hakuna maduka ya dawa ya binafsi kijijini hapo na mtu pekee anayehudumu kwenye zahanati ni ofisa afya, ambaye kwa sasa ni Bwana Mlwande.

Bosco Paulo Mwaluga, Kaimu Ofisa Mtendaji wa Kata ambaye pia ndiye mtendaji wa Kijiji cha Malolo, anasema zahanati hiyo haina mtumishi mwingine zaidi ya ofisa afya.

"Tunajua kwamba mazingira ni magumu ya kufanyia kazi. Licha ya miundombinu ya mawasiliano ukiwemo usafiri, lakini pia kuna uhaba mkubwa wa dawa," anasema Mwaluga, ambaye anathibitisha kwamba ofisa afya huyo ana siku ya tatu tangu alipoondoka kwenda Halmashauri Mpwapwa kupeleka ripoti ya kila mwezi.

Mwaluga anasema, amekuwa akipokea taarifa ya bwana mganga kila anapotuma orodha ya dawa na vifaa tiba vinavyohitajika kutoka ofisi ya afya ya wilaya, lakini mara nyingi dawa hizo huchelewa na wakati mwingine si zote zinazoombwa ambazo hupelekwa.

"Hili ni tatizo sugu hasa kwa watoto ambao, kwa mujibu wa ripoti ya ofisa afya, ndio wanaongoza kwenye orodha ya wagonjwa,” anasema ofisa mtendaji huyo.

Anaeleza kwamba, kutokana na uhaba wa watumishi wa afya, zahanati hiyo hufungwa hata kwa wiki mbili ikitokea bwana mganga anahudhuria mafunzo au hata akipatwa na dharura binafsi.


Kusoma zaidi, tembelea => Dodoma: Zahanati hufungwa hadi wiki mbili kila wakati mganga anaposafiri
 
MBONA KAMA GHARAMA YA NAULI NI KUBWA MNO KWANINI WASIJE DOM MJINI TU NAULI ELFU.4 TOKA MPWAPWA
 
MBONA KAMA GHARAMA YA NAULI NI KUBWA MNO KWANINI WASIJE DOM MJINI TU NAULI ELFU.4 TOKA MPWAPWA
Wazo lako zuri ila kutoka malolo hadi mpwapwa hakuna gari wala njia nzuri,kwa hiyo changamoto iko palepale
 
Wazo lako zuri ila kutoka malolo hadi mpwapwa hakuna gari wala njia nzuri,kwa hiyo changamoto iko palepale
kwa hilo sawa mkuu.ila katika wilayazenye chamgamoto ya miundominu mibovu kwa mfano barabara basi nahisi MPWAPWA INAONGOZA!
 
kwa hilo sawa mkuu.ila katika wilayazenye chamgamoto ya miundominu mibovu kwa mfano barabara basi nahisi MPWAPWA INAONGOZA!
Ni kweli unachosema mpwapwa jiografia yake haisapoti local infrastructures kwa hyo serikali inabidi ijitahidi kujenga barabara kuunganisha vijiji wilayani mpwapwa na maeneo ya karibu kama ruaha,kilosa,kidete na lumuma.
 
Maajabu katika majimbo ya wilaya zilizotajwa hapo yote yanaongozwa na ccm. Je wabunge was ccm hawawajibiki?
 
50+ bado tupo kwenye kushugulikia changamoto za maji, umeme, barabara, elimu na chakula.

Basi tujifunze kwa wenzetu miaka mingine 50 tuwe mbali
Hizi ni nchi ambazo zimepiga hatua japo mpk kua hapo changamoto zilifanya wakawa hapo, tena hawako dunia ya kwanza
Libya(maji) wkt wa Gaddafi (RIP)
Egypt (kilimo )
Afya na elimu (Cuba)
 
upload_2017-2-24_8-0-32.png


Huenda ni taarifa ya muda mrefu au mwandishi hakupata taarifa sahihi au ameamua kwa makusudi kuupotosha umma. Eneo hili lina usafiri wa mini buses kwenda pande zote (Ruaha Mbuyuni na Mpwapwa pia), isipokuwa gari hizi hazianzii eneo hilo, zinapita kutokea pande zote; si eneo rafiki kwa dharura lakini usafiri upo majira ya asubuhi kwenda Ruaha Mbuyuni na Iringa, na mchana usafiri upo wa kueleka upande wa Mpwapwa.
 
View attachment 473974

Huenda ni taarifa ya muda mrefu au mwandishi hakupata taarifa sahihi au ameamua kwa makusudi kuupotosha umma. Eneo hili lina usafiri wa mini buses kwenda pande zote (Ruaha Mbuyuni na Mpwapwa pia), isipokuwa gari hizi hazianzii eneo hilo, zinapita kutokea pande zote; si eneo rafiki kwa dharura lakini usafiri upo majira ya asubuhi kwenda Ruaha Mbuyuni na Iringa, na mchana usafiri upo wa kueleka upande wa Mpwapwa.
Suala la ugonjwa mara nyingi huwa dharura hasa kwa watoto!
 
Serikali haitaki kununua dawa wala kuajiri watumishi mpaka ndege zote zifke, AJABU YA TANZANIA, Kuna sayari zngne 7 zmegunduliwa bora kwenda kuishi huko maana hapa dunian na hasa Tz viongoz hovyo bt wanajar matumbo yao tu na kusahau mahtaj ya wananchi, tutafka tu tuendako!
 
Naamini viongozi wa eneo hilo wameliona hilo tatizo lakini wanajua wakisema kweli wanakuwa ni jipu
Huduma ya afya bado ni changamoto
 
Tunaomba muelewe, tunajenga kiwanja cha ndege cha kimataifa jijini CHATO, ofisi kubwa ya TRA kushinda iliyoko DSM au Mwanza. Tutawarudia miradi ikiisha, kwanza sikusema ntaleta magonjwa. Mwafwaaaa...
 
Haya ndiyo maisha halisi ya Watanzania maeneo mengi sana lakini tumekalia kujadili mambo yasiyokuwa na uhalisia kabisa.....

Tunasikitisha zaidi ya namna utakavyoweza kufikiria....
 
Back
Top Bottom