Dodoma: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa awaambia Mawaziri kuwa CCM itakwenda na mtu mmoja pekee ambaye ni Samia Suluhu Hassan

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,552
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema mwaka 2025 Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitampeleka kwa wananchi mtu mmoja, Rais Samia Suluhu Hassan hivyo mawaziri watambue hilo.

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Oktoba 29, 2021 katika ukumbi wa St Gasper jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa mawaziri na naibu mawaziri.

Majaliwa amewataka mawaziri na naibu wao kuwa wasemaji wakubwa wa mafanikio ya Serikali ili itakapofika 2025, Samia Suluhu Hassan (Rais) apite na kusema kidogo tu.

"Wambieni wananchi kuhusu mazuri yanayofanywa na Serikali hii, tambueni msimamo na mtazamo wa Rais ili mkawe wasemaje zaidi yeye akija awe na maneno machache ya kueleza," amesema.

Waziri Mkuu amewataka mawaziri na naibu wao kufanya kazi kwa mashirikiano na kuheshimu kauli za viongozi wakuu kwani siyo kila agizo lazima waandikiwe barua ndipo watekeleze.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu amewataka viongozi hao kuwa mfano kwa mienendo yao wakianzia na mavazi, kauli na kutojiinga katika mambo yatakayowafanya wajadiliwe.
 
EFF0680E-1D47-4E4A-BA4B-3D8CD245B67D.jpeg
 
  • Kicheko
Reactions: BAK
Hawa viumbe wanakera sana! Yaani kwao madaraka na utawala ndiyo vipaumbele vyao. Siku zote wanawazia matumbo yao tu na kutembelea Ma V8, huku wakiwaweka kwenye foleni walalahoi ili wapite kwa mbwembwe, na wakichagizwa na vile ving'ora vya policcm.
 
Back
Top Bottom