beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa rai kwa Vijana kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo kupitia sekta mbalimbali zikiwemo Kilimo, Maliasili, Utalii, Ujenzi, Uchukuzi, Mawasiliano, Nishati, Madini, Viwanda na Biashara.
Amesema hayo leo akiwa katika Kongamano la Tano la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Jijini Dodoma na kuongeza, "Haya maeneo niliyotaja yanapatikana kwa urahisi Nchini".
Pia ametoa wito kwa Wadau wa Maendeleo hususan Asasi za Kiraia kuongeza jitihada katika kuwezesha Wananchi Kiuchumi ili kuongezea chachu ya kushiriki shughuli za Uchumi.