Dodoma: Tundu Lissu afuata gari lake lililoshambuliwa ofisini kwa RPC Muroto. Ashangaa hadi sasa hajahojiwa yeye na Dereva wake

BAVICHA Taifa

Senior Member
Jul 25, 2013
117
661
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA

Mgombea Urais wa JMT kwa tiketi ya CHADEMA, Mh. Tundu Lissu, leo ametembelea Ofisi ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma kwa lengo la kuchukua gari lake ambalo limehifadhiwa na Jeshi la Polisi Mkoa huo jaribio la mauaji dhidi ya Mh. Lissu la tarehe 7 September 2017.

Mh. Lissu aliambatana na mgombea mwenza wake Mh. Salum Mwalimu na alipokelewa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, SACP Giles Muroto.

Katika mazungumzo yake na SACP Muroto, Mh. Lissu alisema kwamba ameamua kuja yeye mwenyewe baada ya utaratibu wa kulipata hilo kwa njia zingine kushindikana.

Kwa upande wake, SACP Muroto alimweleza Mh. Lissu kwamba Jeshi la Polisi mkoani hapo linahitaji muda zaidi ili kujiandaa kulikabidhi gari hilo kwake.

Aidha, SACP Muroto alimweleza Mh Lissu kwamba Jeshi la Polisi linamhitaji atoe maelezo kwa Jeshi la Polisi kuhusu kushambuliwa kwake September 2017.

Mh. Lissu alijibu kwamba yeye yuko tayari kutoa maelezo polisi kwa tarehe na muda utakaokuwa muafaka kwa pande zote mbili.

Mh. Lissu alisisitiza mshangao wake kwamba hadi sasa, takriban miaka mitatu tangu kushambuliwa kwake, Jeshi la Polisi halijafanya uchunguzi wowote, ikiwemo kumhoji yeye na dereva wake Adam Bakari Mohamed, licha ya kuahidi kwamba lingefanya tangu Mh. Lissu akiwa hospitalini nchini Kenya.

Imetolewa leo Alhamis, Agosti 27, 2020 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
 
Bora Lissu ameenda polisi, hapo karudisha mpira kwa polisi na atatoa maelezo kwa muda sahihi kwake, polisi wasiendelee kusema Lissu anawakwepa kutoa maelezo, na baada ya hayo maelezo ya Lissu polisi itabidi waueleze umma wa watanzania uchunguzi wa shambulio dhidi ya Lissu umefikia wapi.
 
thetallest, Sasa hapo kuna kiki gan mkuu? Yeye kaenda polisi ili wamuhoji ambapo polisi walisema hatoi ushirikiano yeye kaleta ushirikiano wewe unasema anataka kiki

Ulipaswa kumpongeza mkuu kwa ushirikiano wake wa polisi maana wale polisi iliyowaita wasiojulikana sasa inabidi wajulikane maana ushirikiano kwa pande zote mbili sasa unapatikana
 
Bora Lissu ameenda polisi, hapo karudisha mpira kwa polisi na atatoa maelezo kwa muda sahihi kwake, polisi wasiendelee kusema Lissu anawakwepa kutoa maelezo, na baada ya hayo maelezo ya Lissu polisi itabidi waueleze umma wa watanzania uchunguzi wa shambulio dhidi ya Lissu umefikia wapi.
Jamaa Ana akili kubwa sana

Sent from my MRD-LX1F using JamiiForums mobile app
 
Bora Lissu ameenda polisi, hapo karudisha mpira kwa polisi na atatoa maelezo kwa muda sahihi kwake, polisi wasiendelee kusema Lissu anawakwepa kutoa maelezo, na baada ya hayo maelezo ya Lissu polisi itabidi waueleze umma wa watanzania uchunguzi wa shambulio dhidi ya Lissu umefikia wapi.
Nashangaa hawajamkamata!! Mbona wanakuwa wema sana kwa Lissu tangu arudi.
 
Hahahah huyu mgonjwa amekuwa kitukp kweli sasa kajipeleka ana shangaa hawajamuhoji wakati hakuwepo na alisha sema kuwa wao ndio walimshambulia sasa sijui anataka wamuhoji nini wakati majibu anayo mkononi hahahaha mgonjwa bwana
 
Bora Lissu ameenda polisi, hapo karudisha mpira kwa polisi na atatoa maelezo kwa muda sahihi kwake, polisi wasiendelee kusema Lissu anawakwepa kutoa maelezo, na baada ya hayo maelezo ya Lissu polisi itabidi waueleze umma wa watanzania uchunguzi wa shambulio dhidi ya Lissu umefikia wapi.
Hakuna uchunguzi ni maigizo
 
Hahahah huyu mgonjwa amekuwa kitukp kweli sasa kajipeleka ana shangaa hawajamuhoji wakati hakuwepo na alisha sema kuwa wao ndio walimshambulia sasa sijui anataka wamuhoji nini wakati majibu anayo mkononi hahahaha mgonjwa bwana

Hapo anaendelea kuprove ujinga wa vyombo vyetu. Ukumbuke S*lo alishasema kuwa kwa kuwa kaja watampata as if walikuwa wanamtafuta tangu kaja yupo muda gani nchini. Hawajawahi kumtafuta wala kutaka maelezo yake.
 
Hahahah huyu mgonjwa amekuwa kitukp kweli sasa kajipeleka ana shangaa hawajamuhoji wakati hakuwepo na alisha sema kuwa wao ndio walimshambulia sasa sijui anataka wamuhoji nini wakati majibu anayo mkononi hahahaha mgonjwa bwana
Alitaka kuwapa majibu physically na kuandika statement kwenye counterbook ya polisi..... polisi wamegwaya!

Tundu Lissu kawashika MATAGA kunako!!
 
60 Reactions
Reply
Back
Top Bottom