Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Mbunge wa Ubungo (Chadema) Saed Kubenea amepelekwa katika Zahanati ya Bunge baada ya kujihisi vibaya.
Katibu wa wabunge wa Chadema, David Silinde amesema leo Jumatano kuwa, Kubenea amefika mbele ya Kamati ya Haki, Maadili ya Madaraka ya Bunge na amewaeleza kwamba hali yake si nzuri.
Kutokana na hilo, amesema amepelekwa kwenye Zahanati hiyo na hali yake itakapoimarika atahojiwa na Kamati.
Mbunge huyo ambaye alipelekwa Dodoma kwa ndege leo asubuhi, jana Jumanne alisema alikuwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay wilayani Kinondoni akisubiri utaratibu wa safari hiyo ya kwenda kuhojiwa kama Spika wa Bunge Job Ndugai alivyoagiza.
NB:
Hivi kamati hii kwanini wasifanye kama Mahakama walivyo fanya kwa Yusuf Manji kwenda pale Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete JKCI kumsomea mashtaka pale alipo.
Kutolewa hospitali Agakhan Dar, matokeo yake huko anapokelewa anaishia kulazwa kwenye Zahanati.
Chanzo: Mwananchi
Katibu wa wabunge wa Chadema, David Silinde amesema leo Jumatano kuwa, Kubenea amefika mbele ya Kamati ya Haki, Maadili ya Madaraka ya Bunge na amewaeleza kwamba hali yake si nzuri.
Kutokana na hilo, amesema amepelekwa kwenye Zahanati hiyo na hali yake itakapoimarika atahojiwa na Kamati.
Mbunge huyo ambaye alipelekwa Dodoma kwa ndege leo asubuhi, jana Jumanne alisema alikuwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay wilayani Kinondoni akisubiri utaratibu wa safari hiyo ya kwenda kuhojiwa kama Spika wa Bunge Job Ndugai alivyoagiza.
NB:
Hivi kamati hii kwanini wasifanye kama Mahakama walivyo fanya kwa Yusuf Manji kwenda pale Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete JKCI kumsomea mashtaka pale alipo.
Kutolewa hospitali Agakhan Dar, matokeo yake huko anapokelewa anaishia kulazwa kwenye Zahanati.
Chanzo: Mwananchi