BEYOND_LIMIT
Member
- Feb 10, 2017
- 88
- 109
Kutoakana na mji wa Dodoma kuwekwa rasmi kuwa makao makuu imepelekea wakazi wa mji huo kuchukuliwa mashamba yao na serikali kwa fidia ambayo kiuhalisia inanuka dhuluma (kwa mtazamo wangu). Hii inatokana na namna fidia hyo inavyolipwa kwa watu wenye maeneo hayo ambayo mengi yao yalikuwa mashamba (katika eneo la kisasa karibu na chuo cha UDOM ambako inasemekana ni ukanda ambao utajengwa soko kuu, kiwanja cha mpira na stendi ya mabasi, kifupi ni sehemu ambayo iakuwa na fursa nyingi). Kwanin ninasema imejaa dhulma, ni kwa sababu zifuatazo:
Naomba mawazo/kufahamu sharia inasemaje kuhusu jambo hili kwa yeyote mwenye uelewa wa mambo haya.
- Hakuna uwiano ulio wazi wa fidia ya mashamba hayo;
- Wahusika hawataki viongozi (walio teuliwa kwa upande wa wenye mashamba) wakae na wananchi kufanya vikao kujadili hatima ya mashamba yao kwa madai kwamba hitimisho limeshafikiwa.
- Kuvunjwa kwa uongozi wa wawakilishi wa wenye mashamba bila kuhusisha wahusika (wenye mashamba)
Naomba mawazo/kufahamu sharia inasemaje kuhusu jambo hili kwa yeyote mwenye uelewa wa mambo haya.