TANZIA Dodoma: Asia Saidi, Mwenyekiti wa BAWACHA afariki dunia kwa kupigwa na mshale

Duuh! tunakoelekea sio kabisa tukikoseana mtaan tunaanza kuwindana na mishale?

Pole kwa wafiwa
 
Asia Said Ali (50) Mrangi ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA Kata ya Palanga, Wilaya ya Chemba Mkoani Dodoma, amefariki dunia baada ya kupigwa mshale na Mtu aliyefahamika kwa jina la Haruna Ali Kimata miaka 35.

Marehemu akiwa amekaa na mume wake muda wa saa mbili na nusu Usiku, Waliviziwa na Bwana Haruna Ali Kimeta kwa nia ya Kumpiga Mshale Mume wa Marehemu anayefahamika kwa jina la Iddi Masale miaka 55, lakini Mshale Ukamkosa na kumpata Mke wake Mgongoni ambaye alipoteza maisha Muda mchache baada ya kufikishwa Hospitali ya Kondoa.

Chanzo cha ugomvi, ni kwamba Iddi Masale aliingiza Mifugo kwenye Shamba la Alizeti la Haruna. Siku ya tukio, Mchana Walishinda Wanarumbana na kurushiana maneno Makali.

Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Gilles Muroto ameiambia JamiiForums kwamba, Mtuhumiwa wamemkamata na Mshale uliotumika wameupata ambao ni kidhibiti na akaongezea kwamba, tukio hili halihusiani na Siasa.

Vita vikali sana, bahati mbaya Mama watoto imemuangukia yeye ilhali hana kosa.

Nilitamani Huu mshale ungelimpata huyu Bwana Mkubwa Muhusika alietia mifugo shambani kwa mwenzake.

Hawa Wafugaji wanajeuri sana ,
Wamezowea kusababisha Mgomvi ya sampuli hii kila mahali.

Mimi Binafsi Nina shamba mwaka wa 10 huu nashindwa kupata mavuno stahiki kwa vibweka vya wafugaji jinsi walivyo washenzi.

''Natamani na mimi nimiliki Nshale nintafute Ntu wangu anayenitenda kila Mwaka kwenye shamba langu.

Shenzi sana Hawa Wafugaji, sasa Kampoteza Mkewe kwa Ushenzi wake
RIP Mama watoto,
na Mumeo ndio muhusika mkuu,atawajibika kwa kukusababishia Mauti.
Poleni wafiwa.
 
Inawezeka vipi kumuua mtu kwa kumlenga shabaha mtu aliekaa na mwezake?
 
Jamani ungesoma habari yote hayo maswali yako ungejijibu mwenyewe bila kugusa key nyingi kivile.
🤣 🤣 🤣 🤣
Inaonyesha jinsi ambavyo unafikiri kama watu huwa hawasomi. Hiyo heading story imekuwa edited comment yangu ilikuwa na habari ambayo ni nusu nusu. Usiwe unakurupuka next time.
 
Tutaamini vipi kuwa siyo la kisiasa?
Asia Said Ali (50) Mrangi ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA Kata ya Palanga, Wilaya ya Chemba Mkoani Dodoma, amefariki dunia baada ya kupigwa mshale na Mtu aliyefahamika kwa jina la Haruna Ali Kimata miaka 35.

Marehemu akiwa amekaa na mume wake muda wa saa mbili na nusu Usiku, Waliviziwa na Bwana Haruna Ali Kimeta kwa nia ya Kumpiga Mshale Mume wa Marehemu anayefahamika kwa jina la Iddi Masale miaka 55, lakini Mshale Ukamkosa na kumpata Mke wake Mgongoni ambaye alipoteza maisha Muda mchache baada ya kufikishwa Hospitali ya Kondoa.

Chanzo cha ugomvi, ni kwamba Iddi Masale aliingiza Mifugo kwenye Shamba la Alizeti la Haruna. Siku ya tukio, Mchana Walishinda Wanarumbana na kurushiana maneno Makali.

Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Gilles Muroto ameiambia JamiiForums kwamba, Mtuhumiwa wamemkamata na Mshale uliotumika wameupata ambao ni kidhibiti na akaongezea kwamba, tukio hili halihusiani na Siasa.
 
Back
Top Bottom