TANZIA Dodoma: Asia Saidi, Mwenyekiti wa BAWACHA afariki dunia kwa kupigwa na mshale

RPC Dodoma Gilles Muroto amesema tukio la kuuawa kwa M/Kiti wa BAWACHA Kata ya Palanga Asia Said, aliyechomwa na mshale halihusiani na siasa, bali ni kuwa mume wa marehemu alikuwa na ugomvi na mtuhumiwa aliyefanya mauaji hayo baada ya kuingiza mifugo kwenye shamba lake.

1595491360614.png
 
khaa... hebu mwangalie sura, uongo na unafiki haujifichi, yaani hili ni tukio LA kisiasa banaa halihitaji hata elimu kulijua, wafanye kazi kwa haki na sio kuisemea sisiemu!
 
Hakuna watu wajinga km wafugaji, ile tabia yakuona uchi wa ng'ombe masaa yte nadhani inawaathiri hakiri.
 
Bila kuwepo mazingira ya uchaguzi huru na wa haki upo uwezekano mkubwa Tanzania kushuhudia vifo zaidi .Sisemi mimi ,historia ya karibuni(recent election history) Tanganyika na Zanzibar.
 
RPC Dodoma Gilles Muroto amesema tukio la kuuawa kwa M/Kiti wa BAWACHA Kata ya Palanga Asia Said, aliyechomwa na mshale halihusiani na siasa, bali ni kuwa mume wa marehemu alikuwa na ugomvi na mtuhumiwa aliyefanya mauaji hayo baada ya kuingiza mifugo kwenye shamba lake.

hii zee liongo sana, nitakuwa wa mwisho kumuamini!.
huyu hata muuaji angekamatwa kavaa manguo ya kijani pamoja na lebo kamwe hawezi kusema ukweli!.
 
Asia Said Ali (50) Mrangi ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA Kata ya Palanga, Wilaya ya Chemba Mkoani Dodoma, amefariki dunia baada ya kupigwa mshale na Mtu aliyefahamika kwa jina la Haruna Ali Kimata miaka 35.

Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Gilles Muroto ameiambia JamiiForums kwamba, Mtuhumiwa wamemkamata na Mshale uliotumika wameupata ambao ni kidhibiti na akaongezea kwamba, tukio hili halihusiani na Siasa.

Mungu amlaze pema
 
Asia Said Ali (50) Mrangi ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA Kata ya Palanga, Wilaya ya Chemba Mkoani Dodoma, amefariki dunia baada ya kupigwa mshale na Mtu aliyefahamika kwa jina la Haruna Ali Kimata miaka 35.

Marehemu akiwa amekaa na mume wake muda wa saa mbili na nusu Usiku, Waliviziwa na Bwana Haruna Ali Kimeta kwa nia ya Kumpiga Mshale Mume wa Marehemu anayefahamika kwa jina la Iddi Masale miaka 55, lakini Mshale Ukamkosa na kumpata Mke wake Mgongoni ambaye alipoteza maisha Muda mchache baada ya kufikishwa Hospitali ya Kondoa.

Chanzo cha ugomvi, ni kwamba Iddi Masale aliingiza Mifugo kwenye Shamba la Alizeti la Haruna. Siku ya tukio, Mchana Walishinda Wanarumbana na kurushiana maneno Makali.

Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Gilles Muroto ameiambia JamiiForums kwamba, Mtuhumiwa wamemkamata na Mshale uliotumika wameupata ambao ni kidhibiti na akaongezea kwamba, tukio hili halihusiani na Siasa.
*CHADEMA WAUANA KISA VITIMAALUM*

WATIA NIA CHADEMA WAUWANA KURA ZA MAONI WILAYANI CHEMBA, WAMTUHUMU HAJAWAHI KUGAWA-MDE AKIRI.

DEMOKRASIA NI CHANGAMOTO KUBWA NDANI YA CHADEMA.

DEMOKRASIA INANUNULIWA NDANI YA CHADEMA.

DEMOKRASIA INATOA UHAI WANACHAMA CHADEMA.

HAKUNA KIONGOZI YEYOTE ALIYEKEMEA TATIZO SUGU HILO, MWENYEKITI WALA VIONGOZI WENGINE WOTE WAKO BIZE KUTAFUTA TONGE.

DHAMBI YA DEMOKRASIA NI RAHISI KUZAA CHUKI KUTENGENEZA MAKUNDI, UHASAMA HADI KUUWANA NA KUFA KWA CHAMA CHENYEWE.

WANANCHI WA CHEMBA MUWE MAKINI NA FAMILIA ZENU, KURA ZA MAONI CHADEMA ZISIWAACHE YATIMA...... VITIMAALUM NI VYA FARUJOHN.
 
Pole kwa wafiwa.

Jamaa kamponza mkewe na mtuhumiwa kwa kuingiza mifugo kwenye shamba la mwenzake.

Sijui chochote kinachoendelea kwenye hicho kifo, lakini kwa mwenendo wa jeshi la polisi, ni vigumu sana kuamini taarifa yao.
 
Vipi Polisi wanasemaje? Nani amehusika? Je, waliofanya kitendo hicho wameshikwa? Wapi hiyo habari kamili inapatikana?
Jamani ungesoma habari yote hayo maswali yako ungejijibu mwenyewe bila kugusa key nyingi kivile.
🤣 🤣 🤣 🤣
 
Back
Top Bottom