Kuna ajali mbaya imetokea usiku huu maeneo ya Mbande, Dodoma
=====
Watu saba waliokuwa wakisafiri katika gari STL 6250 mali ya CAG wamekufa papo hapo na wengine watatu kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na gari SU 41173 mali ya NSSF, katika eneo la Mbande Chalinze Mkoani Dodoma leo.
Taarifa za awali zinasema kuwa waliokufa katika ajali mkoani Dodoma leo katika gari la Ofisi ya CAG ni dereva wa ofisi hiyo na wengine 6 ni ndugu wa Naibu CAG waliokuwa wakitoka katika msiba huko Chato mkoani Geita.
Dereva wa CAG aliyefariki ametambulika kwa jina la Uson Kitanda Mjita. Alikuwa akitokea Dodoma kwenda Dar huku gari la NSSF lilikuwa likitokea Dar kwenda Dodoma. Majeruhi wote ni wa gari la NSSF. Maiti zipo Hospitali ya Kongwa.
Chanzo cha ajali ni Lori Reiland lenye tela lililoharibikia njiani. Dereva wa CAG aliligonga Lori hilo kwa nyuma na kupoteza uelekeo ndipo akagongana na gari la NSSF.
=====
Watu saba waliokuwa wakisafiri katika gari STL 6250 mali ya CAG wamekufa papo hapo na wengine watatu kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na gari SU 41173 mali ya NSSF, katika eneo la Mbande Chalinze Mkoani Dodoma leo.
Taarifa za awali zinasema kuwa waliokufa katika ajali mkoani Dodoma leo katika gari la Ofisi ya CAG ni dereva wa ofisi hiyo na wengine 6 ni ndugu wa Naibu CAG waliokuwa wakitoka katika msiba huko Chato mkoani Geita.
Dereva wa CAG aliyefariki ametambulika kwa jina la Uson Kitanda Mjita. Alikuwa akitokea Dodoma kwenda Dar huku gari la NSSF lilikuwa likitokea Dar kwenda Dodoma. Majeruhi wote ni wa gari la NSSF. Maiti zipo Hospitali ya Kongwa.
Chanzo cha ajali ni Lori Reiland lenye tela lililoharibikia njiani. Dereva wa CAG aliligonga Lori hilo kwa nyuma na kupoteza uelekeo ndipo akagongana na gari la NSSF.