Do we really need TAKUKURU?

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Posted Date: 10/16/2007

Wapinzani waeleza sababu za kuikataa Takukuru

Kizitto Noya na Salim Said
Mwananchi

UMOJA wa Vyama vya CUF, TLP, Chadema na NCCR Mageuzi, vimeueleza sababu za kutotaka tuhuma za ufisadi kuchunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuwa ni kuokana na kushindwa kwake kutoa ripoti inayoridhisha katika mikataba Richmond na Dowans iliyoikabili serikali.

Katika tamko la vyama hivyo lililotolewa jana jijini Dar es Salaam, umoja huo umesema kuwa hautofanya makosa kukubali taasisi hiyo kuchunguza tuhuma nzito za ufisadi wa viongozi wa serikali kwa kuwa wanaamini kuwa haitatenda haki.

Akisoma tamko hilo katika mkutano uliofanyika kwenye ofisi za Chama cha Tanzania Labour (TLP), Mwenyekiti wa chama hicho, Augostine Mrema, alisema kuwa kitendo cha taasisi hiyo kuisafisha serikali na kashfa ya mikataba hiyo ya Richmond ni doa kwake lisiloweza kusahaulika kirahisi na mwanaharakati yeyote.

Ikiwa Kampuni ya Richmond ambayo serikali ilifanya usimamizi wa kawaida kuhakikisha tatizo la umeme lililoikumba nchi yetu wakati huo linapatiwa ufumbuzi haikuzalisha umeme, Kwa nini serikali haikuwajibika kwa kusimamia mikataba iliyozaa matunda?� alihoji Mrema.

Alisema umoja wa upinzani hauna imani na Takukuru katika kushughulikia wala rushwa na mafisadi ambao ni viongozi wavyeo vya juu serikalini kwa kuwa haiwezi kutenda haki.

Alisema ingawa taasisi hiyo iliisafisha serikali dhidi ya rushwa katika mikataba ya Richmond na Dowans, taarifa za hivi karibuni kutoka Mamlaka ya Kusimamia Manunuzi nchini (PPRA) zinasema kuwa kulikuwa na mkono wa rushwa iliyofanywa na vigogo wa seriakali katika kutoa zabuni na kuidhinisha mikataba hiyo.

Mrema alidai kuwa serikali ilijua kuwa takukuru itailinda katika uchunguzi wake na ndiyo maana iliamua kupinga hoja ya wabunge waliotaka kujadili suala hilo bungeni na kulipeleka kwenye taasisi hiyo.

Wabunge kadhaa walitaka kujadili suala la kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond Development Corporation (sasa Dowans) bungeni ili kujua endapo ulitawaliwa na rushwa lakini serikail iligoma na kuamua kulipeleka suala hilo Takukuru.

Hata hivyo wabunge hao hawakuweza kutimiza azma yao hiyo baada ya kushindwa kutimiza kanuni ya 45 ya Bunge ya kuwasilisha hoja binafsi inayotaka mbunge kutoa hoja hiyo kimaandishi siku mbili za kazi kabla ya mkutano husika wa Bunge.

Richmond iliingia mkataba na Tanesco wa kuzalisha megawati 100 za umeme kwa kutumia gesi asilia, lakini ilikuwa ikikumbwa na matatizo katika utekelezaji wa mkataba huo hadi ilipouzwa kwa kampuni ya Dowans. Mradi huo uligharimu dola za Marekani 172,500,000 (sawa na Sh225 bilioni).

Katika kuchunguzi wake Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) iliisafisha Kampuni ya Richmod Development Company dhidi ya tuhuma za rushwa zilizokuwa zikiikabili katika uingiaji wa mkataba wa kukodisha mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura kwa TANESCO.

Mkurugenzi wa Takukuru, Edward Hosea, alisema baada ya uchunguzi wa taasisi hiyo kuwa hakuna ushahidi wowote uliopatikana kuthibitisha rushwa au upokeaji wa kamisheni kwa watendaji wa serikali.

Alisema uchunguzi wa Takukuru umebaini kuwa Richmond Development Company, LCC ambayo ni kampuni mama ya kampuni ya Richmond Development Company (T) Limited inayomilikiwa na Naeem Gire mwenye uraia wa Tanzania na Mohamed Gire raia wa Marekani, ilifanikiwa kushinda zabuni iliyotangazwa na TANESCO baada ya kuyashinda makampuni mengine manane yaliyojitokeza.
 
Date: 9/22/2008

Takukuru yachunguza sita BoT

*SASA YAFANYA UCHUNGUZI WA RUSHWA

Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi


BAADA ya uongozi wa Benki Kuu (BoT) kuchukua hatua za kinidhamu, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) inawachunguza vigogo sita wa benki hiyo, kutokana na tuhuma za rushwa katika fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Uchunguzi huo wa Takukuru umekuja wakati tayari ikiwa imefanya uchunguzi wa watoto 16 wa vigogo, ndani ya BoT na uchunguzi wa gharama za ujenzi wa majengo pacha (Twin Tower) ya ghorofa 18.

Taarifa kutoka ndani ya BoT zinasema baada ya jopo la kamati ya nidhamu ya benki hiyo kumaliza kazi kwa kuadhibu vigogo sita, wakiwemo wakurugenzi, Takukuru imejiingiza kuchunguza makosa ya jinai ya rushwa.

Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, alipoulizwa suala hilo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, alisema hiyo ni kazi ya Takukuru kwani mwisho wa kazi ya benki ni kutoa adhabu za kinidhamu.

Lakini Profesa Ndulu akabainisha kuwa BoT imetoa taarifa ambazo Takukuru imekuwa ikihitaji kuhusu maafisa wa EPA.

"Sisi (BoT) hutuhusiki na jinai, kazi yetu ni kuchukua hatua za kinidhamu, hayo mambo ya jinai si yetu, lakini Takukuru tumekuwa tukiwapa taarifa wanazohitaji," alisema kwa kifupi Profesa Ndulu na kuongeza:

"Hata katika uchunguzi wa ajira za baadhi ya watumishi wanaodaiwa kughushi, sisi tulichukua hatua zetu na wao za kwao za jinai, sasa ni vema ukawatafuta wenyewe."

Hata hivyo, kifungu cha 37 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya Takukuru ya mwaka 2007, inazuia taasisi hiyo kuzungumzia uchunguzi unaoendelea.

Habari hizo kutoka BoT zilifafanua zaidi kwamba, Takukuru inawachunguza maafisa hao kuona kama wamenufaika na fedha za EPA.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, vigogo hao iwapo watabainika kunufaika na fedha hizo huenda wakakabiliwa na makosa ya jinai ya rushwa.

"Lengo kubwa ni kuona kama wamenufaika kwa namna moja au nyingine, sasa kama wamenufaika wanaweza kukabiliwa na mashitaka ya jinai," alisema mtu mmoja kutoka BoT.

Chanzo kingine kutoka BoT kilieleza kwamba maafisa hao ambao wametajwa katika Ripoti ya Ukaguzi ya Ersnt & Young, wanachunguzwa kwa jinai huku rufaa zao za adhabu za kinidhamu zikiwa katika hatua ya mwisho.

Rufaa nne kutoka kwa vigogo hao sita, akiwemo mkurugenzi mmoja ambaye mkataba wake wa kustaafu ulikwisha mwezi Machi, zinasikilizwa na mwenyekiti wa rufaa, ambaye kwa sheria ya BoT ni Gavana.

Chanzo hicho kilifafanua zaidi kwamba, vigogo hao sita kwa sasa wako kwenye wakati mgumu kutokana na kwamba, walitajwa katika ripoti ya ukaguzi wa kitaalamu.

"Kinachowapa hofu ni kwamba, kwanza tayari wametajwa katika ripoti ya ukaguzi wa Ernst & Young, ndiyo maana hata BoT ilipowachukulia hatua za kinidhamu, ilipitia ripoti hiyo na kisha yenyewe kufanya uchunguzi wa kina na kujiridhisha kwamba kwa namna moja au nyingine walihusika," kilisema chanzo hicho na kuongeza:

"BoT haikukurupuka hata kidogo... yule gavana (Profesa Ndulu), ni mtu makini sana... wafanyakazi wengi wanampenda, hapendi majungu, ndiyo maana nakwambia hawa jamaa hadi kuadhibiwa ujue kumefanyika uchunguzi wa kweli."

Chanzo hicho kiliongeza kwamba, mkurugenzi wa sita ambaye ameingizwa katika orodha hiyo alikuwa amestaafu Machi lakini naye ameingizwa katika orodha na anachunguzwa, kwani wakati ufisadi ukitokea mwaka 2005/06, alikuwepo.

"Sasa hapa ndipo utajua hawa watu wana wakati mgumu, huyu mkurugenzi alimaliza mkataba wake mwezi Machi, lakini ameingizwa katika orodha kwani wakati wizi ukitokea alikuwepo katika madaraka," kilifafanua chanzo kingine.

Tuhuma za ufisadi katika akaunti ya EPA ziliibuliwa katika ukaguzi wa hesabu za mwaka 2005/06 uliofanywa na Ersnt&Young, baada ya ule wa Kampuni ya Deloitte&Touche ya Afrika Kusini kusitishwa.

Baada ya Deloitte&Touche kubaini ufisadi uliofanywa na Kampuni ya Kagoda, ghafla ilisitishiwa mkataba, hali iliyozidisha maswali ambayo yaliibua mjadala mzito bungeni hadi serikali kuagiza uchunguzi ufanywe na Ersnt& Young, ambayo iliibua kashfa hiyo ya wizi wa zaidi ya Sh133 bilioni.

Baada ya kubaini ufisadi huo, Januari mwaka huu Rais Jakaya Kikwete, aliagiza hatua zichukuliwe kwa wahusika ndani ya BoT kwa mujibu wa taratibu za benki.

Kufuatia agizo hilo, kwa mara ya kwanza Gavana Profesa Ndulu, mwezi Januari alifanya mabadiliko makubwa ya wakurugenzi ambayo yalifuatiwa na kung'olewa vigogo hao sita wa sasa.

Katika mabadiliko ya Januari, Profesa Ndulu alibadili wakurugenzi kutoka idara mbalimbali isipokuwa Uchumi, Fedha na Masoko.

Katika mabadiliko hayo, gavana huyo ambaye amekuwa akiangaliwa kama mwenye kuweza kuleta mabadiliko ndani ya BoT kutokana na uzoefu wake wa kufanya kazi Benki ya Dunia (WB), alisafisha wakurugenzi wa Idara za Makao Makuu na matawi yote ya benki hiyo, isipokuwa Mwanza.

Matawi ya BoT nchini ukiacha Mwanza ni pamoja na Zanzibar, Mbeya na Arusha ambayo yamekuwa yakiongozwa na wakurugenzi.

Idara zilizokumbwa na mabadiliko hayo ni Utawala na Utumishi, Fedha, Benki, Idara inayoshughulikia Deni la Taifa na inayoshughulikia Zabuni.
 
Kikwete aiwakia TAKUKURU
  • Ataka mafisadi vigogo sasa wakamatwe
  • Awaambia wasio na ujasiri waondoke
  • Aiagiza ikomeshe rushwa uchaguzi 2010

PCB.jpg

Rais Jakaya Kikwete (katikati), akisikiliza maelezo kuhusu jengo jipya la makao makuu ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kutoka kwa Mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo, Dk. Edward Hosea (kulia), jijini Dar es Salaam jana.

Rais Jakaya Kikwete, amewataka watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kuwa na ujasiri wa kuwakamata wala rushwa wakubwa na kwamba ambaye anajiona hawezi ni heri akauze juisi.

Pia, ameitaka taasisi hiyo kujipanga kukabiliana na vitendo vya rushwa kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa jengo la Makao Makuu ya Taasisi hiyo lililopo Upanga jijini Dar es Salaam jana, Rais Kikwete aliitaka isimwonee haya kigogo yeyote mla rushwa na kusisitiza kuwa kamwe serikali haitaiingilia katika utendaji wake.

Alisema rushwa kwenye uchaguzi ni kubwa na inasababisha wapatikane viongozi wasio waadilifu ambao baada ya kupata madaraka, hutafuta namna ya kurejesha fedha walizotoa badala ya kuwatumikia wananchi.

Pia alisema Takukuru inapaswa kuwapeleka mahakamani watuhumiwa baada ya kujiridhisha na ushahidi walioupata, lakini wasifanye hivyo kwa kushinikizwa na baadhi ya watu.

"Mkimpeleka mtu mahakamani, muwe na uhakika, siyo mnampeleka leo wiki ijayo mnafuta mashitaka dhidi yake, hapo mnakuwa tayari mmemfedhehesha na hakuna kitu cha fedheha kama mtu kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za rushwa," alisema.


Aliitaka taasisi hiyo ijipange vizuri ili kuhakikisha inashinda kesi zote hasa kubwa inazopeleka mahakamani na kwamba hali hiyo ndiyo itaipa heshima kubwa na serikali kwa ujumla.

"Najua kuna watu wana watu wao ambao wangependa waone wanafikishwa mahakamani na bila hao watu kukamatwa, hawajisikii raha, lakini ninyi msifanye kazi kwa shinikizo la mtu, chunguzeni mkijiridhisha, kamateni na kumpeleka mahakamani mhusika," alisema.


Aidha, Rais Kikwete alisema amekuwa akipokea ujumbe mwingi kutoka kwa watu wanaolalamikia vitendo vya rushwa na kuzituma kwa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk. Edward Hosea, ili zifanyiwe kazi.

Alisema kila taarifa ya rushwa inayotolewa na wananchi, lazima ifanyiwe kazi ili kupunguza malalamiko ya mara kwa mara kuhusu vitendo vya ulaji rushwa.

"Naomba muelekeze darubini yenu katika rushwa kwenye manunuzi maana huko kuna malalamiko mengi sana, tenda zikitolewa kunakuwa na malalamiko fulani hivyo elekezeni nguvu kule ili mtu anayepata tenda awe amepata kwa sifa stahiki na si kwa sababu anajuana na mtu ama katoa rushwa," alisema.


Aliongeza kuwa fedha nyingi za umma zimekuwa zikiliwa, lakini hakuna kinachofanyika mara baada ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kutoa ripoti yake.

Alisema umefika wakati wa ripoti ya CAG ikionyesha kuna fedha za umma zimeliwa, basi ipelekwe Takukuru ili uchunguzi ufanyike na wale wote waliohusika na kadhia hiyo wakamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria.

"CAG akigundua fedha zimeliwa anaandika ripoti analeta kwangu na mimi nasaini nawasilisha bungeni, kule wabunge wanaijadili na mjadala unafungwa hakuna hatua wanazochokuliwa wahusika sasa hii haisadii, lazima uchunguzi ufanyike na waliokula wakamatwe," alisema.

"Ripoti ikifika kule bungeni wabunge wanamshambulia waziri weee, tena wanachagua mawaziri wa kuwashambulia na kama huna uhusiano mzuri nao wanasema huyu atatukoma ukiwa na uhusiano mzuri unanusurika," alisema na kuongeza kuwa kama kuna tatizo linakuwa la serikali nzima na si la waziri mmoja.


Alisema anaelewa ugumu wa kuwakamata wala rushwa hasa wakubwa ambao hutoa vitisho kwa watumishi wa taasisi hiyo, lakini alisema mtumishi jasiri na mahiri, hawezi kuogopa vitisho hivyo na atapambana na mtu wa aina hiyo.

Alisema anaelewa kuwa kazi hiyo ni ngumu na ya hatari, lakini kwa kuwa watumishi hao waliomba wenyewe ni vyema wakawa wakakamavu la sivyo wakafanye kazi zingine watakazoona wanaweza.

"Hata mtu unayemjua unalazimika kumkamata maana lazima ipo siku katika kamatakamata utakutana naye tu, ujasiri, umahiri ni sifa za msingi za kufanya kazi hii ya kupambana na wala rushwa," alisisitiza.

Akizungumza na Nipashe baada ya shughuli hiyo, Mkurugenzi wa Takukuru, Dk. Hosea, alisema uchunguzi wa kesi za vigogo unaendelea na wananchi wasubiri matokeo hivi karibuni.

Alisema ofisi yake inategemea zaidi ushirikiano kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) katika kutengeneza mashitaka ya watuhumiwa hivyo suala hilo linachukua muda.

Alisema uchunguzi umefikia hatua nzuri na matokeo yanaweza kuonekana muda si mrefu.

"Kama alivyosema Rais, hapa lazima tuchunguze tujiridhishe ili tusimwonee mtu, kwa hiyo acheni uchunguzi ufanyike na wenye tuhuma watafikishwa mahakamani," alisema Dk. Hosea, ambaye Mei, mwaka huu alisema mwezi huu kesi zote kubwa za ufisadi zinazowahusisha vigogo zitafikishwa mahakamani.


Jengo jipya la taasisi hiyo lililojengwa kwa mkopo kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) limegharimu Sh. bilioni 4.1.


Chanzo: :: IPPMEDIA
 
mimi hapa ndo napopate kiwewe..yaani JK anawapiga mkwara Takukuru meaning haelewi kinachoeldelea au
 
Sasa wa kuwashangaa wanaongezeka pia, namshangaa huyu Bwana Hosea, badala ya kumfahamisha Raisi wazi wazi kuwa anakosa ushirikiano wa DPP anakuja kuwaambia waandishi??? Kama hakumfahamisha Raisi hilo angalau faragha anastahili kutimuliwa, hafai hafai! Na kama JK hatamtimua baada ya matamshi hayo (kama hakumlalamikia kabla) yote ni feki! itakuwa kama Walienda kufungua kihoteli chao cha siri humo ndani ya Takukuru!!!
 
Iwapo kutoa na kupokea rushwa ni kosa la jinai, mbona TAKUKURU inawaandama WANASIASA peke yao, waliotuhumiwa kutoa rushwa wakati wa mchakato wa kura za maoni (hususan CCM)? Wanasiasa hao wasingetoa rushwa kama wapiga kura wasingekuwa wanapokea. Kahaba hasimami mtaani, usiku kucha, akijiuza, pasipokuwa na wateja. Hivyo, mtoa rushwa hatoi pasi na kuwapo na mpokeaji.

TAKUKURU iwakamate pia na kuwashtaki mahakamani waliopokea. Wasiseme hawawajui, kwani walijuaje nani ametoa mpaka wakamkamata na kumpeleka mahakamani? Huwezi kuwa na ushahidi wa upande mmoja, na kusema fulani ametoa rushwa, kwa hiyo ashtakiwe. Ametoa rushwa, sawa, lakini nani aliyepokea? Ushahidi kamili ni kuwapo kwa waliopokea, ambao nao wanatakiwa kushtakiwa PAMOJA na waliotoa, KWA PAMOJA, si vinginevyo.

Ama sivyo huu ni UNAFIKI, sawa na kelele nyingi zinazotoka kwenye DEBE TUPU!

TAKUKURU fanyeni kazi yenu kwa umakini! Hizi ni porojo!

./Mwana wa Haki
 
nadhani ni namna y a kuwaengua DAMU MPYA.....ARI ZAID.....UPEPO MWINGINE NDAI YA CHAMA CHA KIJANI...!
 
Hakuna kesi ya mtoa rushwa pekee. Huo ni unafiki na kinyume cha sheria! Washtakiwe wote kwa pamoja! Anayetoa na anayepokea! Vinginevyo, hawana mantiki ya kisheria...

In jurisprudence, the burden of proof always lies with the PROSECUTION! I cannot be accused of murder without the body of the murdered person!
 
Hakuna kesi ya mtoa rushwa pekee. Huo ni unafiki na kinyume cha sheria! Washtakiwe wote kwa pamoja! Anayetoa na anayepokea! Vinginevyo, hawana mantiki ya kisheria...

In jurisprudence, the burden of proof always lies with the PROSECUTION! I cannot be accused of murder without the body of the murdered person!

Mara nyingi wanadai kuwa ule ni mtego kuwa yule mtu kaenda kutonya so anatumika kama mtego.
Cha msingi wantakiwa kuzuia so wanatatiwa kukataza wanachi kupokea so na mtoaji hata toa.So ukisema wote wapelekwe mahakani hiyo bomba hasa kwa wapinzani maana inaweza kutokea mtu pandikizi akasema fulani kanipa rushwa so ajue kuwa kama yeye alipokea wote vibogo 20 wakati wakuingia jela na 20 wakati wakutoka wakonyeshe wenzi wao.
 
Kumbe taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inafanya kazi zake kwa ushirikiano na Chama cha Mapinduzi badala ya kuwa chombo huru, imefahamika.

Taarifa kutoka Mwanza zinasema Takukuru imefikia hatua ya kutoa ushauri wa moja kwa moja kwa CCM juu ya nani ateuliwe kugombea ubunge na nani aenguliwe.

Mfano halisi ni barua ya Christopher Mariba, Mkuu wa Takukuru mkoa wa Mwanza, kwenda kwa Katibu Mkuu wa CCM mkoa, Rajab Kundya.

Katika barua hiyo, mkuu wa Takukuru anapendekeza nani ateuliwe kuwa mgombea, kwa mujibu wa uchunguzi wao kwa kuzingatia Sheria ya Gharama za Uchaguzi iliyotungwa na kuanza kutumika mwaka huu.

Kwa barua yenye Kumb. Na. PCCB/MZ/8/13/VOL.XXII/99 ya tarehe 9 Agosti mwaka huu, Takukuru inapendekeza Titus Kamani (Mlegeya), aliiyeshinda kura za maoni jimboni Busega, asiteuliwe kugombea kwa madai kuwa alivunja sheria ya gharama za uchaguzi. Kamani alikuwa akichuana na Dk. Raphael Chegeni, Dadius Swea na Nyangi Tindo.

Katika barua hiyo, Mariba anapendekeza jina la Kamani litupwe na nafasi yake ichukuliwe na mmoja wa washindani wengine.

Taskukuru inaripoti katika barua yake, "Katika siku yenyewe ya upigaji kura, Agosti mosi, 2010, vitendo kama ugawaji wa pikipiki, kununua kadi za wapiga kura na kuwanywesha pombe wapiga kura vilikithiri," inasema Takukuru.

"Intelijensia tulizonazo zinatosha kabisa kufungua jalada rasmi la uchunguzi dhidi ya Kamani na hatimaye kufungua hatua za kisheriam dhidi yake," inaeleza Takukuru.

Mariba amezitaja tuhuma dhidi ya Kamani kuwa ni kuandaa kundi la vijana wahuni ambao alihakikishawamelewa muda wote na kazi yao kubwa ni kuzomea na kuleta fujo.

Madai mengine dhidi ya kamani ni kwamba alitumia gari la serikali Na. DFP 440 Land Rover 110 PickUp mali ya idara ya Wanyama Pori katika shughuli za uchaguzi.

Akifafanua, Mariba alisema gari hilo lilitumika kusombea wapiga kura na mawakala kutoka kituo kimoja hadi kingine kinyume cah sheria…………

………Naye Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza, Rajab Kundya, amekiri kuwa alipokea mapendekezo ya Takukuru lakini walibaini kuwa hayakuwa sahihi na ndioyo maana hawakuyatekeleza.

"Sisi tulichukulia barua ile ya Takukuru kama mapendekezo au ushauri kwetu. Hata hivyo, tulifanya uchunguzi binafsi na kugundua baadaye kuwa hawakuwa sahihi," emesema Kundya.

Akihojiwa kwa simu kutoka Mwanza Kundya hakutaka kueleza CCM ina vyombo gani vya kufanya uchunguzi vyenye uwezo kuzidi Takukuru yenye dhima ya kufanya kazi za uchunguzi nchini…………….


Habari zaidi ndani ya Mwanahalisi la leo.
 
Asante Mkuu:

Sijawahi kuona mambo ya hovyo na ya kihuni kama haya ya CCM na Takukuru yake. sasa hakuna ubishi kabisa kwamba Takukuru ni project ya CCM -- ila tu watu kama akina Kundya hawajui. Kama Hoseah anajiona yeye na taasisi yake wako huru basi ajiuzulu sasa hivi kutokana na hiyo humiliation kutoka kwa JK kuhusu Mwakalebela.

Taasisi yake imemchunguza, imegundua alitoa hongo kwa wapiga kura na ikamfikisha mahakamani -- lakini sasa mwajiri wa Hosea (JK) anaona yote hayo ni bure tu -- na huenda akamwambia aondoe kesi mahakamani au akitiwa hatiana atamsamehe mara moja na kumtoa gerezani.

Hosea hawezi kujiuzulu kwa na atayameza yote hayo aliyotapikiwa na JK.
 
Asante Mkuu:

Sijawahi kuona mambo ya hovyo na ya kihuni kama haya ya CCM na Takukuru yake. sasa hakuna ubishi kabisa kwamba Takukuru ni project ya CCM -- ila tu watu kama akina Kundya hawajui. Kama Hoseah anajiona yeye na taasisi yake wako huru basi ajiuzulu sasa hivi kutokana na hiyo humiliation kutoka kwa JK kuhusu Mwakalebela.

Taasisi yake imemchunguza, imegundua alitoa hongo kwa wapiga kura na ikamfikisha mahakamani -- lakini sasa mwajiri wa Hosea (JK) anaona yote hayo ni bure tu -- na huenda akamwambia aondoe kesi mahakamani au akitiwa hatiana atamsamehe mara moja na kumtoa gerezani.

Hosea hawezi kujiuzulu kwa na atayameza yote hayo aliyotapikiwa na JK.

Huyu Hosea si alitakiwa ang'oke kutoikana na mapendekezi ya kamati ya Bunge kwa sababu ya kutetea mafisadi? Watanzania hebu tujitutumie mwaka huu tulitimue genge la hawa impostors waliotanda kwenye uongozi. Nakubali tuna matatizo ya fedha, lakini kwa watu wanaotaka kujikomboa, si kazi kubwa.
 
Kwa kuwa Takukuru iliwasafisha mafisadi wa Richmond kwa kufunika ukweli

kwa kuwa Katika Kampeni za kura za maoni ndani ya CCM ilionekana moto , lakini ilinyamaza kimya katika Uchaguzi mkuu na kuacha vitendo vya rushwa vikiendelezwa na mafisadi wa CCM,

Kwa kuwa haikusema tangu awali kwamba Chenge alishasafishwa na SFO , imeibuka tu kipindi Chenge ameijitokeza kugombea Uspika , na kuzua maswali mengi kama kweli hakuna ulipaji kisasi na kukomoana kutokana na Six kuruhusu Mjadala ulihiotimishwa kwa kutaka Mkuu wa TAKUKURU awajibiswe,

Kwa kuwa wanatumia pesa nyingi sana kudili na wala rusha dagaa baadala ya Manyangumi ,


Kwa kuwa Tume hii sio huru ,

Hivyo basi napendekeza ivunjwe na iundwe tume huru ,otherwise bora isiwepo kabisa maana haina manufaa kwa taifa mbali na kupoteza pesa za walipakodi (PAYE JAMANI , mimi nalipa zaidi 500,000/= kila mwezi agrrrrrr.... hasira sana)
 
Walioiweka ndio inawasaidia na kuwalinda. Sasa nani wa kuivunja?

kwenye uchaguzi mkuu ,Mwanza, Arusha , Kawe na Ubungo imethibitisha umma ukiamua matakwa yake yatatekelezwa


tufanye vivyo vyo kwa Takukuru , tunaokatwa PAYE tuna wajibu kuhakisha pesa zetu zinatumika kisawasaw
 
kwenye uchaguzi mkuu ,Mwanza, Arusha , Kawe na Ubungo imethibitisha umma ukiamua matakwa yake yatatekelezwa


tufanye vivyo vyo kwa Takukuru , tunaokatwa PAYE tuna wajibu kuhakisha pesa zetu zinatumika kisawasaw

Kama wameshindwa kumzuia Chenge kuchukua fomu ya kugombea uspika, hawataweza kuvunja takukuru. Takukuru ipo kwa maslahi ya mafisadi.
Mimi na wewe tutafanyaje kuvunja Takukuru? Tupige makelele, ama?
 
Mkuu sio TAKUKURU, NI IDARA ZOTE ZINATUMIKA KISIASA
1) UHAMIAJI- mara huyu sio raia, mara huyu raia, na juzi wamemgongea RA Muhuli wa EXIT wa pale NIA ili ionekane kuwa ametoka nje siku ya tukio akuwepo
2) JWTZ- Kama mlivyomsikia Shimbo+ issue ya Meremeta
3) POLICE- jinsi wanavyoshughulikia watu kutokana na siasa zao ( issue ya Shibuda na yule jamaa wa CCM)
4) TISS-Kama inavyojulikana
5) NEC-Kama inavyojulikana
6)TCA (Mawasiliano)-Hawa jamaa walikuwa hawajuhi zile MSg z kumkashifu Slaa zinatoka wapi
7)TBC, DailyNEws,HLeo-Hivi ni Vyombo vyaq Habari vya Umma lakini vinafanya kazi ya CCM
8)..........
9)..........
 
Back
Top Bottom