Dkt. Tulia: Kama wasingeenda Mahakamani ningetangaza nafasi kuwa wazi

Wa kukemea uovu hayupo genge la kifisadi linalolindwa na dola limeng'ang'ana kutunyonya kama luba!kazi ipo kiukweli nchi yetu haina viongozi.
Nchi hii umma usipotoka usingizini tutaendelea kuibiwa mpaka Basi, mahakama na bunge vinatumika kusafisha ufisadi wa kulipa watu wasio na vyama bungeni.Dhambi hii itaendelea kuumiza taifa letu daima
 
Tulia ukilala unasali kwa roho na kweli? Hujajifunza tu ya Job? Cheo ni dhamana na WAKATI SI MILELE!
Yuko wapi Job leo hii
Yuko wapi Sabaya
Yuko wapi Bashite....
Yako wapi mafirauni yote yaliyotamba kwa nyakati zao?
Kwa hali mbaya ya uchumi wa maskini wa nchi hii halafu Kuna watu wamekalia ofisi za umma bila kujali Kodi zetu zinavyoliwa kitapeli nadhani Karma italipa kama ilivyolipa Kwa wengine.

Tulia ni msaka Mali na umaarufu TU Hana uzalendo wowote.

Chadema imemaliza kazi yake kilichobaki ni kuionyesha umma jinsi wezi wa nchi hii wanavyolindwa na kulindana huku wabunge wakipiga makofi.

Natamani atokee Mbunge mmoja wa CCM msema kweli aseme bungeni kuwa pale Kuna Wabunge wasio na Chama wapo Kwa Sheria ipi? na Je bunge linapewa Ubunge na mahakama ?

Ndio maana mtu alishinda kesi ya uchaguzi kwenye Jimbo hapewi Ubunge na mahakama Bali uchaguzi una rudiwa ili apatikane Mbunge Mwingine Kikatiba.
Wale wamevuliwa uanachama hawana sifa Tena Kikatiba. Hilo halihitaji hukumu ya mahakama.

Ubunge sio haki ya kina Halima Mdee Bali ni Haki ya Chama chao Kwa mujibu wa Katiba yetu.
Hivyo wakishafukuzwa uanachama basi Chama kimechukua haki yake.

Mkiambiwa tuwe na Katiba mpya inayotambua mgombea binafsi manasema Katiba haileti chakula mezani wakati Kuna watu wanakula mamilioni Kwa kujifanya wanatetea maslahi yao Kikatiba.
 
Na vipi ikionekana wamefukuzwa kiharamu? Je watalipwa marupurupu yao yote ikiwemo mafuta ya gari kwa muda waliokuwa nje?
Watafungua kesi ya kukidai Chama kiwalipe fidia na kuwadhalilisha.

Hao Wabunge wanamuwakikisha nani?

Hivi viti Maalumu vifutwe kabisa kwenye katiba mpya ni kuhujumu TU fedha za umma Kwa mambo yasiyo na tija. Kila mtu apigiwe kura ndipo aingie bungeni. Bunge liwe linalinda maslahi ya umma sio maslahi yao kama ilivyo Sasa.Serikali na bunge na Sasa mahakama vipo Kwa maslahi ya waliopo Huko kwenye nafasi za Juu sio vinginevyo . Tumepigwa paaaaa na kitu kizito.
 
Huyu Spika ametoa hoja dhaifu sana, ameridhalilisha bunge na wasome wa sheria.
Ngoja nifafanue hili.
1. Spika anasema aliambiwa na wakina Mdee kuwa wamedhamiria kufungua kesi hivyo akaamua awasubiri kwanza wafungue kesi!
Mbunge aliyevuliwa uanachama wake anaweza kwenda mahakamani baada ya siku, wiki, mwezi, mwaka nk. Spika atajuaje mhusika atakwenda mahakamani lini ili asichukue maamuzi kwanza? Kwa mfano wakina mdee wangesema watafungua kesi mwakani, je spika angesubiri muda wote huo?

2. Kipindi chote kifupi ambacho wakina mdee wamevuliwa uanachama na baraza kuu la CHADEMA kabla ya kufungua kesi, kwanini waliendelea na status za kibunge ikiwemo kuingia bungeni?

3. Spika alijuaje aina ya kesi inayokwenda kufunguliwa na akina Mdee kabla ya kesi husika kutajwa mahakamani?

4. Spika aliwezaje kuzifanyia kazi taarifa za kusikia sikia za kina mdee kutaka kufungua kesi na hapo hapo akashindwa kuzifanyia kazi taarifa za kusikia sikia (ambazo zilitangulia) kuhusu kuvuliwa uanachama wa CHADEMA?

5. Kwanini Spika alipopokea barua inayohusu kuvuliwa uanachama wa akina Mdee (siku ya ijumaa asubuhi) hakuifanyia kazi papo hapo ikiwemo kutangaza kupoteza ubunge badala yake akasubiri mpaka wafungue kesi?
Nafikiri hii Hali ya watu wa Chache kulindana na kulihujumu Taifa itashamiri sana mana hata kule Hazina watakwapua halafu serikali ikitaka kuwasimamisha kazi au kuwafukuza watakimbilia mahakamani na kuomba mahakama izuie wasiachie ofisi na waendelee kukalia ofisi mpaka mahakama itoe hukumu.
Hivi Mhimili wa Serikali unaweza kufanyiwa ujinga huo na mtu waliyemtoa ofisini Kwa kukosa sifa.?
Tulia ni Mkuu wa Mhimili wa ajabu kuwahi kutokea.
 
Crap!

Utendaji wa bunge unategemea uwepo wa wabunge wa viti maalum - kweli ukiwa mnafiki, ni rahisi kukubali kuwa mjinga. Watu wanatetea ujinga.

Natural justice principle ni kwamba, taasisi yoyote ambayo wewe umo, ikikuondolea haki au manufaa yoyote yale, iwe kwa haki, kimakosa au kukuonea, utaendela kuitumikia hukumu hiyo mpaka ama fhombo cha juu zaidi ndani ya taasisi yako au mahakama itakavyobatilisha uamyzi wa taasisi hiyo.

Huu upuuzi wa Tulia na wajinga wengine waliomo humu, eti ukishakatia rufaa maamuzi ya taasisi yako mahakamani, basi unaendelea na haki za awali, ni uwendawazimu wa hali ya juu. Kama shwria zingekuwa zinafanya kazi kwa namna hiyo, tysingekuwa na wafungwa. Kwa maana mtu akihukumiwa kifungo, anakata rufaa, kisha anakuwa huru kusubiria maamyzi ya rufaa. Na hayo maamuzi yakitoka, unakata rufaa tena, hukumu inasimama, unaendelea kuwa huru.
Na wale wezi kule halimashauri wakishaiba pesa au wakituhumiwa kula pesa za Halmashauri na kusimamishwa au kufukuzwa kazi basi nao watakimbilia mahakamani kupinga kuachia ofisi hivyo wataendelea kukalia ofisi wakisubiri hukumu ya mahakama. Ni khatari sana kama Mhimili unaotunga Sheria unajidhalilisha Kwa kiwango hicho Tena ukiwa inaongozwa na Daktari wa Sheria.

Kumbe na wale waliotumbuliwa Kwa vyeti feki wangekimbilia mahakamani wangeendelea kufanya kazi na kulipwa mshahara mpaka mahakama itoe hukumu?
 
Mnasumbuka bure wale 19 hawatoki Bungeni.
Kesi itazungushwa hadi msahau.

Tutaongeaje na Wahisani juu ya Democrasia kwenye medani za Kimataifa ?
Hao 19 ndio chambo ya kuonesha Demokrasia yetu kimataifa.

Alaf nauliza.
Hivi Chadema hawawachangishi tena ile ruzuku za kunenepesha mfuko wa Chama zile milioni mbili kwa kila Mbunge?

Maana 19 X 200,0000/=
= 38,000,000/= kwa mwezi
Kwa mwaka 38m X 12.
= 456,000,000/=
Pesa yote hii kweli Mbowe anaisusa ?

Hivi ungekuwa wewe Mwanachadema Kindakindaki.
CCM wamekupa ubunge wa bure ule kuku mjengoni miaka mitano.
Ungegoma kweli, sababu tu wanachama hawataki. ?

Na njaa yote hii
Sijui kama kuna Mtanzania angeiacha hiyo fulsa, sijui.
Aisee Sasa hapo wanaoumia ni Chadema au ni Taifa Zima kukosa watu waadilifu. Hivi unafikiri hata CCM ikiwatumia watu wanaoghushi itakua imepata watu wanaofaa kulitumikia Taifa? Au ndio tuamini kuwa CCM ni Chama Cha wezi na mafisadi ndio maana inapigania maslahi HARAMU ya kina Mdee.

Ni upumbavu Gani wa kuliingiza Taifa kwenye Upuuzi wa kuombaomba Huko Ulaya halafu pesa za misaada hiyo hiyo iliwe na kundi la watu 19 Kisha Taifa liingie kwenye madeni .

Kwa Miaka 5 Akina Mdee watakua wamekula almost pesa zote zinazoombwa kukuza Demokrasia. Na matokeo yake hazijakuza hiyo Demokrasia na badala yake zimetumika kuvuruga Demokrasia na kujenga chuki kwenye jamii na kuliachia Taifa madeni na kujenga misingi ya wizi kwenye Taifa. Hii ni akili kweli. Si Bora nchi zinazotawaliwa kinazi au kiidiamini!!

Yani tunakopa na Misaada halafu pesa zikija zinaliwa na kakundi kadogo Kwa watu waliokalia nafasi kinyume na taratibu halafu wananchi wanakamuliwa kwenye tozo na Bei kubwa ,halafu wanasiasa wajinga wanashangilia ? CCM itaanguka wakati mbaya sana bila kutarajia ! Inawaona watu kama ni wajinga sana bila kujua kuwa ,wajinga Kuna siku watakua na maisha magumu sana na watabadilika na kugundua kuwa ujinga wao ndio tatizo.
 
Tunachouliza watanzania, hivi hilo Bunge lina double standards, Katika maamuzi yake?

Iweje wabunge wa CUF walipovuliwa uanachama wao, papo hapo, wakafukuzwa na ubunge wao, kwa kuwa Bunge lilieleza wazi kuwa haliwezi kuendelea na wabunge wasiotokana na chama chochote cha siasa!

Hivi inakuwaje sasa kwa Hawa wabunge wa Chadema, Spika aendelee kuwakumbatia Hadi pale mhimili wa Mahakama utapotoa hukumu??
wale wa CUF walikwenda mahakamani kabla ya nafasi zao za ubunge kufutwa?
 
Viongozi wa chadema Wana utoto flan sometimes wanapenda kuonewa huruma kwenye mitandao kama hivi!

Wao walisema kabisa hawapeleki wabunge wenyewe walijua wanakomoa serikali, katika haya Maisha ya kiafrica uwez kubishana na serikali never,

Ndio maana unaambiwa serikali ina mkono mrefu
Afrika ndio maana hakuna Nabii Wala Mtume aliyepewa kitabu. Tunatumia vitabu vya manabii na wakombozi wa mataifa mengine. Mungu alijua waafrika ni wabinafsi sana na wanajali maisha yao TU.

Kama Yesu angekua na mawazo kama haya angeendelea TU kula Bata Mbinguni sio kuja kuwakomboa wanadamu .

Nchi za Wenzetu zimefukia zilipo Kwa sababu Kuna watu walisimama na kupigania Misingi IMARA na ya Haki Kwa watu wao bila kujali uhai wao au maslahi yao. Afrika tumekosa watu wa aina hiyo. Mungu anasimama na watu Jasiri na wasio na woga.

Hata akina Mdee wakishinda Bado Watakua sio wanachama wa Chadema na kule bungeni watakaa kinyume na Katiba ya nchi Iko siku nchi hii watatokea watawala wazalendo Sio genge la wapigaji na wasaka madaraka watawakamata na kuwatia ndani wahuni waliofilisi nchi hii yenye rasilimali nyingi.
Kuna kiwango Cha dhulma kikifikia Mungu anaweka mtu wa kulipa kisasa ndivyo asili ilivyo Wala Haina ubishi.
Na kama unabisha jaribu kufuatilia utaona kama Kuna sehemu akatokea mfano mtu ameshika Bunduki au panga halafu akapiga watu risasi hadharani na kuua watu wasio na hatia hovyohovyo ,ghafla watu wanabadilika na kuingiwa na ujasiri wanamkabili bila kujali kuwa watakufa au la na wanamfuata muuaji mpaka wanamkamata na Bunduki yake hata kama imeisha risasi na kupiga Kwa kiwango Cha juu sana na hata kumuua. Asili inatabia ya kulipa kisasi kwenye mambo ya dhulma. Ndio maana watanzania tunatakiwa kubadilika na kuwasomea albadiri na Dua mbaya viongozi wanaoiba Mali za umma na sio kuwaombea. Tukiwaombea Mungu anawasamehe na wanaendelea kuiba na kuona wizi ni ufahari na wanauhalalisha na kuwa na kiburi.
 
Chama akitaki

I think wakina sugu na msigwa wangekuwa wanaweza kujibadili kuwa wanawake I'm sure na wao wangeenda tu

Miaka yote mnaibiwa Kura, miaka yote uchaguzi sio huru mbona mlikuwa mnaenda? This time Kwa vile hakuna mwanaume kashinda ndio mnasusa
Acheni kuchoche chuki kwenye Taifa.

Hiyo Miaka yote uliwahi kuona Polisi wanaingia mpaka kwenye vyumba vya Kupiga kura na kubeba masanduku.
2020 Polisi wengi walijitokeza hadharani na kusema kuwa wao ni CCM na wengine mpaka kuchukua Fomu za kugombea Ubunge ili hali katiba inakataza.Ingekuaje kama wangine wangegombea kupitia Vyama vya upinzani?
Watu waliporwa fomu za uchaguzi mchana kweupe?
Watu wanaenguliwa nchi nzima.
Mawakala wanazuiliwa kuingia nchi nzima.
Watu walikatazwa kujumlisha kura zao . Watu walikatazwa kutumia simu.
Mitandao ilizimwa nchi nzima. Halafu unalinganisha na chaguzi nyingine.
Yaani unalinganisha uporaji wa ""Panya Road "" na wizi wa "" Tuma kwenye Namba hii""

Wizi wa Kura ulikuwepo lakini sio kama ule wa Panya Road wa 2020. Watu wakikata mapanga na kuuawa kila mahali. Mpaka Mgombea wa Chadema ananyima Kibali Cha kuruka na Helkopta halafu unahalalisha ushetani huo kweli.
Maisha ni mapito TU hakuna haja ya kufanya mabaya Kwa wengine ili hali kila mtu anataka kutendewa haki.

Ukitaka kujua Maisha ni mapito waangalie wale waliokua ni Vijana awamu zilizopita wakiwa na nguvu za kufanya uhuni wote wanaotaka ,Leo ni wazee wanatembea Kwa kudemadema. Wengine Wamebaki na kiburi TU lakini hawana furaha.

Haki huinua Taifa. Sio kauli ya kupuuzia maana ni kauli ya kinabii.
 
Chama kilisema wazi uchaguzi ulikuwa batili, hao Covid wangeanzisha chama chao wapeleke wabunge kiasi chochote watakacho.
Kama uchaguzi ulikuwa batili. Mwenyekiti anaendaje kuonana na Rais batili, mnaandika barua kwa bunge batili, kwa muktadha huu itakuwa na nyie ni batili
 
Mimi hili suala hata silielewi. Hivi kwa nini Spika hakuwaita wakina Halima na NEC ili watoe uthibitisho kuwa barua waliyompa ni halali? Maana kama kweli walimpa barua basi Spika ndio injured party na ni yeye ndie aliyepaswa kuchukua hatua dhidi ya waliomdanganya kwa kumpa nyaraka za kughushi. Ukimya wake kwenye suala hii ndio unanitia wasiwasi kuwa hamna nyaraka iliyowasilishwa kuwatambulisha wakina Halima kuwa wateuliwa wa Chadema. Hii ndio inayonifanya nione tuhuma za kughushi hazina mashiko. Labda sasa Chadema watumie Mahakama kumlazimisha NEC atoe nakala za barua alizopokea kutoka Chadema.

Amandla...
Mkuu Fundi Mchundo , vitu vingine sio vya kuuliza ni kutaka tuu kumuonea Spika.
Uchaguzi unasimamiwa na NEC, Wabunge wote wanapewa barua ya utambulisho ya NEC ndio wanatinga Bungeni. Sii kazi ya Bunge au Spika kuhoji wamepatikanaje, as long as Barua ya utambulisho ya NEC imemfikia then ni authentic letter, Bunge halina sababu yoyote kuhoji utambulisho wa NEC.

Humu JF wengi wana mahaba na Chadema hivyo they are just too blind to see jinsi inavyofanya mambo ya hovyo. Hili jambo ni Chadema wenyewe wameli mishandled toka mwanzo.
Naomba niunganishe na hoja ya Mkuu Nguruvi3 nizijibu kwa pamoja kuwaonyesha makosa ya Chadema ya kijinga kabisa.
Mkuu P , kuna hoja moja tusaidie kuielewa ili tusimuonee Spika.

Spika Tulia kasema asubuhi ya jana, 'kuna shauri lipo mahakamani hatawazuia COVID19 bungeni''
Jioni Jaji Mgeta anatoa kauli ya mahakama ya 'status quo' kwa Wabunge

Swali, Spika alipata wapi taarifa za COVID19 kwenda mahakamani?
Kuna sheria gani inayomkataza asiwazuie kuingia Bungeni kabla ya 'hukumu' ya mahakama?
Swali la mwisho, je, Tundu Lissu ambaye shauri lake lipo mahakamani ni Mbunge halali?

JokaKuu Fundi Mchundo
Kwa faida ya wengine naomba nianzie mbali.
  1. Hili jambo limeanzishwa na Chadema kususia kutambua matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita, ikasema hailitambui Bunge na haitambui Rais
  2. NEC ikatoa nafasi 19 za viti maalum, Chadema wakasema hawateua na hawana time.
  3. Mdee of course, accompanied by Bulaya, wakam consult a very high ranking Kigogo wa Chadema on the benefits of hizo nafasi 19, Kigogo huyo not only gave them a go ahead, but also facilitated them!.
  4. Introduction credentials from Chadema (a bone of contention) introduced the 19 to NEC.
  5. NEC wakawapa barua za utambulisho, authentic bonafide genuine certificates wakaziwasilisha Bungeni, hivyo Kibunge, hawa ni Wabunge halali kabisa!.
  6. Spika/Bunge has nothing to do with the process iliyotumika kumpata mbunge yoyote, as long as ameteuliwa na NEC.
  7. Kukitokea mgogoro wowote wa Uchaguzi, kwa mtu yoyote kupinga ushindi wa mgombea mahakamani, huyo Mbunge ataendelea kuwa mbunge mpaka mahakama itakapotoa hukumu.
  8. Na kukitokea mgogoro wa kichama, mbunge yoyote kufutwa uanachama na chama chake, anapaswa kupoteza ubunge wake automatically ila akiliarifu Bunge kuwa amepinga mahakamani kuvuliwa kwake uanachama, Bunge litamkingia kifua kusubiria aumuzi wa mahakama.
  9. Hivi ndivyo ilivyofanyika kwa Hamad Rashid Mohammed, David Kafulila na Zitto Kabwe. Na baada ya uamuzi wa mahakama, walivuliwa ubunge, Zitto alijivua na kuaga rasmi Bunge.
  10. Hivyo jana asubuhi kupitia Bunge live, Spika alizungumza huku nikimuona kwa macho yangu na kumsikia kwa masikio yangu, alitangulia kupokea taarifa ya kina Mdee kufungua kesi mahakamani kupinga kuvuliwa uanachama, kwa kutaja siku, saa na dakika, kabla ya kupokea taarifa rasmi ya Chadema kuwafuta uanachama. Hivyo Spika Tulia yuko right na Bunge liko right kuwakingia kifua.
  11. Haya sasa ninayoendelea nayo ni yangu. Watu wengi humu wana mahaba niue na Chadema, na siku zote mapenzi yakizidi huleta upofu hivyo hamuoni makosa ya Chadema.
  12. Baada tuu ya Wabunge hao kuapishwa na Chadema kuwakana, sisi washauri wa bure tukawashauri Chadema wafanye a due process wameingiaje Bungeni, barua ya utambulisho toka Chadema imeandikwa na kusainiwa na nani.
  13. Hii due process ingebainisha kuna forgery, forgery ni jinai, walipaswa kuripoti polisi ili uchunguzi wa kijinai ufanyike na hiyo barua yao ya utambulisho, iwe authenticated na ingebainika ni forgery, wala sio Bunge bali ni NEC ndio wangetengua zile barua zao za uteuzi na wangevuliwa ubunge.
  14. Chadema ina katiba yake katiba hiyo imeweka sheria taratibu na kanuni za nidhamu. CC ni mamlaka ya nidhamu ya wabunge, kwanini waliliendesha shauri la wabunge hao Kikangroo bila kufuata taratibu na kanuni zao. Kwanini CC ya Chadema wawatimue wabunge hao bila kufanyika kwanza kwa a due process?!
  15. CC ya Chadema sio mamlaka ya nidhamu ya Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee, mwisho wa mamlaka ya CC ya Chadema kwa Mwenyekiti wa Bawacha ni kumsimamisha tuu, lakini mamlaka yake ya nidhamu ni Baraza Kuu, sasa hiyo CC ya Chadema, ilipata wapi mamlaka ya kumtiimua Halima Mdee?.
  16. Kikao cha Baraza Kuu kilipoitishwa kwanini hawakupeleka shauri la Mdee kwenye mamlaka yake sahihi ya rufaa?.
  17. Baraza Kuu linapokaa kama mamlaka ya rufaa kwa wale wabunge 18, ukimuondoa Halima Mdee, kabla ya kupiga kura kuridhia maamuzi ya CC, walipaswa kujiridhisha kuwa taratibu zilifuatwa.
  18. Kile kikao cha CC ya Chadema mimi nimekiita CC ya Chadema imekaa kama a Kangaroo Court, na ule uamuzi wa CC ya Chadema, mimi niliuita ni uamuzi wa Kikangroo, kitendo cha Baraza Kuu kuyabariki maamuzi batili ya Kikangroo bila kufanyika kwanza kwa a due process, kumepelekea Baraza Kuu Chadema kufanya Ukangaroo as well.
  19. A way forward ni Mahakama ambayo ni a proper court itayapindua maamuzi ya Kikangroo ya CC ya Chadema yaliyobarikiwa na Baraza Kuu na kuamuru a due process ifanyike.
  20. Wito wangu kwa wapenzi wa Chadema, seek the truth and the truth will set you free. Iambieni Chadema ukweli, ndio mtaijenga Chadema kuwa ni chama mbadala kuireplace CCM. Kwa haya madudu na maroroso kama haya, Ikulu yetu wangeweza?.
Paskali
 
Tunachouliza watanzania, hivi hilo Bunge lina double standards, Katika maamuzi yake?

Iweje wabunge wa CUF walipovuliwa uanachama wao, papo hapo, wakafukuzwa na ubunge wao, kwa kuwa Bunge lilieleza wazi kuwa haliwezi kuendelea na wabunge wasiotokana na chama chochote cha siasa!

Hivi inakuwaje sasa kwa Hawa wabunge wa Chadema, Spika aendelee kuwakumbatia Hadi pale mhimili wa Mahakama utapotoa hukumu??
Umemsikiliza lakini spika kasemaje?
 
Mkuu Fundi Mchundo , vitu vingine sio vya kuuliza ni kutaka tuu kumuonea Spika. Uchaguzi unasimamiwa
Mkuu P , kuna hoja moja tusaidie kuielewa ili tusimuonee Spika.

Spika Tulia kasema asubuhi ya jana, 'kuna shauri lipo mahakamani hatawazuia COVID19 bungeni''
Jioni Jaji Mgeta anatoa kauli ya mahakama ya 'status quo' kwa Wabunge

Swali, Spika alipata wapi taarifa za COVID19 kwenda mahakamani?
Kuna sheria gani inayomkataza asiwazuie kuingia Bungeni kabla ya 'hukumu' ya mahakama?
Swali la mwisho, je, Tundu Lissu ambaye shauri lake lipo mahakamani ni Mbunge halali?

JokaKuu Fundi Mchundo
 
Wale wa cuf sababu za kufukuzwa kwao hazikuwa na adhari kwenye utendaji wa Bunge

Chadema iligoma kupeleka wabunge viti maalum, Jambo la viti maalum ni Jambo la kisheria

So wakina mdee walivuliwa uanachama wao Kwa kutiii sheria ya viti maalum


Hapo sasa ndio chadema watafeli hata mahakamani
Hapo ndio shida ukisema Chadema walikataa viti maalumu kina Mdee wakaenda kina Mdee ndio nani chama cha siasa? sheria ziko wazi watu wanateuliwa na chama chao sio unajipeleka tu mwenyewe kwenye hili tuweke ushabiki huko hawa na sote tunajuwa nani aliwaweka bila kufuata utaratibu Bunge linatambua Chama sio watu mmoja mmoja. Haya ya CUF na Chadema hakuna tofauti yoyote. Speaker anasema ni jukumu lake kufuatilia kesi mahakamani sio kuletewa hukumu kama wasomi wetu wa sheria wanaongea hivi basi kuna shida kubwa katika nchi hii. Speaker katangaza hukumu kabla mahakama haijatoa hukumu jana kawahi sana Mama sasa anafanya damage control. Kufungua kesi mahakamani haina maana yoyote bila kuwa na hukumu angesubiri hukumu ndio angesema nilikuwa nataka kutangaza nafasi lakini nimepokea hukumu makahakamani kusimamisha ila bahati mbaya katoa hukumu yeye asubihi mahakama ikaleta tu karatasi baadae. Tulia aibu yako kama msomi wa sheria ndio wewe basi tusitegemee miujiza nchi hii sijui utawafundisha nini watoto zako. shame kwa wasomi wetu
 
Mkuu Pascal Mayalla , kwavile wiki nzima na ushee umekuwa mstari wa mbele katika kusimamia ''masilahi' ya Taifa bila kujali chama, na kwakuwa unaona COVID19 wameonewa na Chadema kufukuzwa ;

a) Kwanini wanataka kubaki na Ubunge kwanza na si shauri la msingi la uanachama?

b) COVID19 wanawakilishwa na Mawakili wa Serikali. Kuna kifungu gani kinachowapa fursa ya kuwakilishwa na serikali ikiwa mgogoro ni suala la ndani ya Chama? Kumbuka mgogoro si ubunge?

Ukishatufahamisha majibu ya #117 tusaidie kufafanua a na b hapo juu

JokaKuu Fundi Mchundo
 
Umemsikiliza lakini spika kasemaje?
Speaker bora angekaa kimyaa ndio kaharibu kabisa. Kasema alivyoambiwa wamefungua kesi hakusubiri mahakama imuambie jukumu lake kufuatilia kujiridhisha ila yeye alishatoa hukumu kwa niaba ya mahakama kabla hata mahakama haijatoa hukumu. Kufungua kesi haina maana sheria isifuatwe hukumu ikitoka unaletewe nakala ya hukumu ndio unachukuwa sheria. Bunge limejivua nguo wao kuwa ndio watu wa kuvunja sheria za nchi. Katiba ndio sheria Mama hakuna aliyekuwa juu ya katiba hivi hili linahitaji mahakama? hatuna wagombea binafsi ukiwa sio mwanachama hata ukijivua au kuvuliwa unapoteza sifa za ubunge haki unazitafuta nje ya bunge sio ndani ya bunge.
 
Mkuu Pascal Mayalla , kwavile wiki nzima na ushee umekuwa mstari wa mbele katika kusimamia ''masilahi' ya Taifa bila kujali chama, na kwakuwa unaona COVID19 wameonewa na Chadema kufukuzwa ;

a) Kwanini wanataka kubaki na Ubunge kwanza na si shauri la msingi la uanachama?

b) COVID19 wanawakilishwa na Mawakili wa Serikali. Kuna kifungu gani kinachowapa fursa ya kuwakilishwa na serikali ikiwa mgogoro ni suala la ndani ya Chama? Kumbuka mgogoro si ubunge?

Ukishatufahamisha majibu ya #117 tusaidie kufafanua a na b hapo juu

JokaKuu Fundi Mchundo
Mkuu,huyo unayemuomba muogozo huwa hapendi kuusimamia ukweli (siyo muongo)nadhani U-CCM umemjaa kuliko ukweli.Anapindishapindisha maneno na kujinukuu nyuzi zake nyingi ili akubabaishe.Na si kukupa ukweli na haki.Msubiri.
 
Back
Top Bottom