Allency
JF-Expert Member
- Jan 27, 2011
- 13,672
- 13,067
Mkuu umeshirikisha ubongo kweli?Mkuu kwenye maendeleo zinatumika zaidi dhana mbili; Rostow's Stages of Development na Marxist Stages of Development kutegemea una mrengo gani kisiasa. Wote wanakubaliana kwamba Maendeleo ya Watu ndio hatua ya juu kabisa (High Mass Consumption kwa Rostow) na (Communism kwa Marxism) ya maendeleo ya mwanadamu.
Kama ninyi na Lissu wenu mnaweza kutuaminisha tofauti kwamba unaweza kusafiri kwa haraka kati ya Mwanza na Dar (maendeleo ya watu) bila ndege au SGR au watu kuwa na umeme wa uhakika (maendeleo ya watu) bila kuzalisha umeme wa kutosha na wa uhakika inawezekana, mimi nitaunga mkono hoja.