Uchaguzi 2020 Dkt. Tulia atangazwa mshindi Mbeya Mjini, Sugu apoteza kiti chake cha Ubunge

Dr. Tulia Ackson Ashinda kwa kishindo kikubwa Jimbo la Mbeya mjini. (Sugu na Mbowe siyo wabunge Tena wa JMT).
Tazama picha ya matokeo hapo chini.

ed4b2c9fc52548ef85b09c95ab694dab.jpg
 
Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Mbeya Mjini amemtangaza Dkt.Tulia Ackson kuwa Mbunge wa Jimbo hilo baada ya kupata kura 75225 huku mbunge aliyemaliza mda wake Joseph Mbilinyi (SUGU) akipata jumla ya kura 37591.

PIA SOMA:
= >
 
Hongera Sana Tulia Ackson ....kazi kazini ...hiki ndio kikosi cha maendeleo
 
Mitandao na upambe wa kijinga wa vijana wa ufipa ndo umewaponza Wagombea wengi wa CDM katika Uchaguzi huu.
Sasa kwa Mfano Dr. Tulia aliwekeza nguvu nyingi zaidi katika kusaidia jamii na kujitoa katika matukio mbalimbali ya kijamii kabla na wakati wa uchaguzi, Ila ndugu yangu Sugu yeye alikuwa busy tu kufoka twiter na kujifariji mitandaoni na kwenye vyombo vya habari halafu unategemea kushinda.

Iwe fundisho kwa Wapinzani wote jaribuni kuwekeza nguvu kwa Wananchi huko na siyo kuendelea kubwabwaja tu huku online.
Upinzani Ni mhimu Sana katika kuleta maendeleo ya Taifa Ila lazima ujitambue kwanza.
 
Back
Top Bottom