Vandetta
JF-Expert Member
- Dec 5, 2013
- 1,537
- 1,896
Mitandao na upambe wa kijinga wa vijana wa ufipa ndo umewaponza Wagombea wengi wa CDM katika Uchaguzi huu.
Sasa kwa Mfano Dr. Tulia aliwekeza nguvu nyingi zaidi katika kusaidia jamii na kujitoa katika matukio mbalimbali ya kijamii kabla na wakati wa uchaguzi, Ila ndugu yangu Sugu yeye alikuwa busy tu kufoka twiter na kujifariji mitandaoni na kwenye vyombo vya habari halafu unategemea kushinda.
Iwe fundisho kwa Wapinzani wote jaribuni kuwekeza nguvu kwa Wananchi huko na siyo kuendelea kubwabwaja tu huku online.
Upinzani Ni mhimu Sana katika kuleta maendeleo ya Taifa Ila lazima ujitambue kwanza.
Jamaa waliwekeza Twitter na kugoma goma...wenzao wakawekeza kwa wananchi