Dkt. Tulia amjibu Mbunge aliyehoji kuhusu Uwanja wa Ndege Msalato. Asema Rais kashasema utajengwa

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326


Katika kipindi cha maswali na majibu, Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, amesema Naibu Waziri hawezi kusema kitu tofauti na alichozungumza Rais.

Amesema hayo baada ya Mbunge Kunti Majala kuhoji ni lini Serikali itajenga Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato akisema haupo kwenye Bajeti ya 2021/22.

Dkt. Tulia ameeleza, "Rais amesema Uwanja utajengwa, kwa hiyo kama upo au haupo kwenye Bajeti Rais kashasema, ndio Sheria hiyo".
 
Dah! Maspika wetu hawa yaani

Hili swali ilitakiwa kabisa spika ndio aulize au kama mbunge akiuliza basi ilitakiwa spika amuunge mkono kuhitaji majibu kujua iwapo uwanja bajeti yake haijatengwa utajengwaje!

Angalia jibu lake lakini "Rais amesema Uwanja utajengwa, kwa hiyo kama upo au haupo kwenye Bajeti Rais kashasema, ndio Sheria hiyo"
 
Dah! Maspika wetu hawa yaani

Hili swali ilitakiwa kabisa spika ndio aulize au kama mbunge akiuliza basi ilitakiwa spika amuunge mkono kuhitaji majibu kujua iwapo uwanja bajeti yake haijatengwa utajengwaje!

Angalia jibu lake lakini "Rais amesema Uwanja utajengwa, kwa hiyo kama upo au haupo kwenye Bajeti Rais kashasema, ndio Sheria hiyo"
Rais kasema uwanja utajengwa. Period!
 
Rais most of time yuko Dar sijui kama ana interest na Dodoma!

Commitment ya Dodoma na Uwanja wa Msalato vilikuwa ni wazo la JPM!

Sijui kwa nini kuhamia Dodoma kuliharakishwa bila maandalizi, pesa na sababu za msingi!

Wafanyakazi wamestaafu sasa wana mwaka hawajalipwa mafao yao kwa vile serikali haina pesa- leo unaharakisha kujenga uwanja wa ndege Msalato!

Watz Tunajua vipaumbele kiusahihi kweli?
 
Uwanja huo una tija gani? Wakati kimbinyiko tu dakika sifuri yuko DOM, Dom kuna treni ya mwendokasi ndio iwe kipaumbele unashuka KIA au JKNIA unakula bombadia, kimbinyiko, ABC, Super sonic, Shabiby, au treni kwenda Dodoma.

Hakuna uhitaji wa madege makubwa hapo DODOMA, hiyo pesa bora tuyachukue majengo ya NSSF kule Kigamboni tuyageuze hospitali ya rufaa
 
Msalato Airport inajengwa kwa mkopo kutoka AFDB ambao ulishapitishwa kitambo sana, kuna tatizo kubwa kwa hawa wawakilishi wa wananchi, kabla ya kuropoka bungeni wanatakiwa kufanya utafiti

Ni wazi pia Dkt. Tulia hana ufahamu wa kinachoendelea kwa namna alivyomjibu kiwepesi huyo mbunge
 
Miradi mingi iliyoachwa na JPM haitaendelezwa kwa sababu uwezo wa kukusanya fedha wa serikali hii ni mdogo sana watakuja na visingizio kua haina tija tunaipiga chini ukweli ni kwamba hawana fedha
 
Manenno halisi aliyosema Naibu Spika yako wapi? Kuna video au audio?
 
Msalato Airport inajengwa kwa mkopo kutoka AFDB ambao ulishapitishwa kitambo sana, kuna tatizo kubwa kwa hawa wawakilishi wa wananchi, kabla ya kuropoka bungeni wanatakiwa kufanya utafiti

Ni wazi pia Dkt. Tulia hana ufahamu wa kinachoendelea kwa namna alivyomjibu kiwepesi huyo mbunge
Hata kama inajengwa na AFDB lazima ionekane kwenye mipango ya nchi
 
Back
Top Bottom