Dkt. Tulia Ackson onesha uungwana. Omba radhi kwa kutumia jeneza na msalaba wakati wa kampeni 2020

Milonji

Senior Member
May 26, 2022
153
494
Salaam wapendwa.

Dk. Tulia Ackson Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sasa, aliwahi Kufanya kosa la KIIMANI akiwa katika harakati za kutafuta Ubunge.

Dk. Tulia aliwahi Kutumia Jeneza na MSALABA kama Ishara ya kuizika CHADEMA kwa Mkoa wa Mbeya.

Watu walipopiga kelele kwenye Mitandao ya Kijamii Dkt. Tulia hakujali kitu na akanyamaza kimya kama vile ni sawa na ni haki yake.

Majuzi mashabiki wa Simba wakarudia kitu kile kile tena kwa kuweka na Vionjo vya aina ya Mavazi vinavyofana na yale yanayotumika katika Misa na au Ibada Takatifu.

Watu wakiwamo na Viongozi wa Dini wakajitokeza hadharani kukemea dhihaka iliyofanywa na Mashabiki wa Simba.

Ukimya wa Dkt. Tulia kwa kosa lile la KIIMANI alilofanya inawezekana lilisababisha Washabiki wa Simba waone ni kitu cha kawaida wakaingia mkenge kwa kuiga na kuongeza vionjo vyenye makwazo zaidi. Inawezekana kabisa kama Dk. Tulia asinge shupava shingo yake wakati kwa kuomba Msamaha Simba wasingefanya Jambo lile. Dhihaka ndogo imetengeneza Dhihaka kubwa.

Simba waungwana wamechutama na Wameomba Msamaha. Naamini KIIMANI Wamesamehewa.

Dkt. Tulia ni wakati wako wa kuonyesha uungwana. Chutama na uombe Msamaha kwa kitendo kile ulichokuwa umefanya ili Jamii ijue kwamba lilikuwa Jambo baya na wasije Kufanya kama wewe.

Hili ni ombi langu kwako Dkt. Tulia Ackson popote ulipo.
 
Wakristo tumeumbwa na msamaha

Tumeshamsamehe lililobaki ni yeye na Mungu wake
Ili umsamehe mtu lazima aombe msamaha hii inamaana kuwa mhusika atakuwa amejutia kosa lake na hivyo hataki kulirudia tena (Na hata YESU anasisitiza kutafuta upatanisho na adui yako kabla hujafika kwa Kadhi). Kuomba msamaha kunatoa uhakikisho wa kutokurudia kosa.

Kwahiyo, kama mtu hajaomba msamaha halafu ukaamua kutokuhesabu kosa lake UTAKUWA UMEPUUZA HUYO MTU( siyo umemsamehe).
 
Mbona mna complicate mambo? Nyie ni wakristu kweli au wa mchongo?

Msalaba wa Simba na wa Dr. Tulia ni vipande vya mbao tu.

Hamuelewi hata ukristu ni nini mnashangaza pamoja na maaskofu wenu uchwara mnautia aibu ukristu.
 
Dk. Tulia aliwahi Kutumia Jeneza na MSALABA kama Ishara ya Kuizika CHADEMA kwa Mkoa wa Mbeya.
Tafsiri yake ni kwamba kifo ni adhabu na mtu akifa hana thamani, dhambi hiyo itaitafuna nafsi yake polepole
 
CCM ndio inayotakiwa kuomba msamaha na si Dr. Tulia, kama ambavyo Simba alivyolazimishwa aombe msamaha na si msanii Tundaman
 
Tupia ka picha, wengine hilo tukio la Tulia hatukuliona ili tuungane kumwambia aombe msamaha ili kuondokana na mambo ya hovyo hovyo kama haya kufanyika tena, halafu ukizingatia yeye ni msomi na mheshimiwa......
 
"Wabongo" acheni kukuza mambo .................👇👇👇👇
1 Kor 1:18
Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
 
Mbona mna complicate mambo? Nyie ni wakristu kweli au wa mchongo?
Msalaba wa Simba na wa Dr. Tulia ni vipande vya mbao tu.
Hamuelewi hata ukristu ni nini mnashangaza pamoja na maaskofu wenu uchwara mnautia aibu ukristu.
Wewe unaujua ukristo kama Mtume PAULO?, Ambaye anasema msalaba kwetu ni wokovu ila kwa wayunani ni upuuzi.

Hawa wanaotetea heshima ya msalaba ni wakristo wa kweli. Wale wanaoona msalaba ni vipande vya mti tu, ni wakristo wa mchongo.

Unaruhusu vipi njia yako ya wokovu kufanyiwa dhihaka?
 
Wewe unaujua ukristo kama Mtume PAULO?, Ambaye anasema msalaba kwetu ni wokovu ila kwa wayunani ni upuuzi.
Hawa wanaotetea heshima ya msalaba ni wakristo wa kweli. Wale wanaoona msalaba ni vipande vya mti tu, ni wakristo wa mchongo.
Unaruhusu vipi njia yako ya wokovu kufanyiwa dhihaka?
Haya kapigane nao unaoona wanaudhihaki.
 
Ndio tatizo la dini za kutengenezwa na binadamu..
Mawazo yako ya ovyo Sana.
Hakuna dini iliyoletwa na MUNGU dini zote zimeletwa na binadamu.
Wewe umemwona MUNGU anatetea dini yako wapi?, Ni binadamu tu ndio unaowaona wanatetea dini yako.
(Acha kuwa brain washed).
 
Demi hii ni kauli ya kuishiwa hoja..!! Wakristo hawapo hivyo..!!
Wakristu hawalalamiki mambo ya kipuuzi kama hivi. Msalaba unakuwa na maana pale tu unapotumika na wanaoelewa maana yake.
Pia tumefundishwa kumwachia mungu mambo ambayo yapo nje ya uwezo wetu. Kwani Mungu yeye haoni? Atawaadhibu aonavyo yeye.
Kwanini uhangaike na mtu asiyejua maana ya kitu?
Kama wangechukua msalaba uliowekwa kanisani wakaufanyia walichofanya ingekuwa issue nyingine.

Wameokota mbao wametengeneza msalaba wala haujabarikiwa na mtumishi wa mungu tunapiga kelele.

Mbona kuna madhehebu mengi ya kikristu yote yanatumia msalaba lakini mafundisho yanapingana hamlalamiki?

Tuache unafiki.
Msalaba unakuwa na maana pale tu unapotumika kwa maana iliyokusudiwa. Mbali na hapo ni maigizo yasiyokuwa na maana yoyote.
 
Back
Top Bottom