Dkt. Tulia Ackson: Ilani inasema barabara ya Tanzam upembuzi yakinifu umekamilika Serikali inasema utafanyika mwakani. Tuiamini CCM au Wizara?

Thubutu aulize swali kama hili enzi za dhalimu!!! Hizi ni dalili tosha kwamba ndani ya maccm mama ana hali ngumu sana.

Hapana BAK, hizi ni dalili za kuwa sasa watu wamepata nafasi ya kuwa binadamu tena!! Mwendazake aliwafanya watu wawe nusu maiti; vichwa vilijaa pumba tu!! Mpaka Gwajima akawaaminisha Watu wajinga kuwa yeye angeweza kufufua maiti mithiri ya nabii Issa bin Mariam!!
 
Unadhani watu wasingekuwa waoga ndani ya Maccm na Serikali ya kumkabili kwa wingi bila woga kila alipokiuka katiba na taratibu za nchi angevimbisha kichwa na kufanya maovu mbali mbali aliyoyafanya Mkuu? Wapuuzi hao na walikuwa chanzo cha nchi yetu kupitia kipindi kigumu kuliko vyote tangu tupate uhuru. Watubu hadharani kwa kukaa kimya kuruhusu dhalimu aingamize nchi kwenye kila sekta na kuumiza Watanzania wengi sana.


Hapana BAK, hizi ni dalili za kuwa sasa watu wamepata nafasi ya kuwa binadamu tena!! Mwendazake aliwafanya watu wawe nusu maiti; vichwa vilijaa pumba tu!! Mpaka Gwajima akawaaminisha Watu wajinga kuwa yeye angeweza kufufua maiti mithiri ya nabii Issa bin Mariam!!
 
Mbunge wa Mbeya mjini Dr Tulia Ackson amesema kuna mkanganyiko mkubwa kati ya Ilani ya uchaguzi ya CCM na bajeti ya wizara ya Ujenzi kuhusu Ujenzi wa barabara ya Tanzam.

Ilani inasema upembuzi yakinifu umekamilika lakini waziri katika bajeti yake anasema upembuzi yakinifu utafafanyika mwaka ujao wa fedha, sasa tumwamini nani CCM au Serikali? Anauliza Dr Tulia ambaye pia ni naibu Spika wa bunge.

Chanzo: Bungeni
Tulia siyo strategist. Alitegemea huruma za Mwendazake ndiyo amsaidie kuweka mafungu kama alivyomsaidia kupata ubunge wa Mbeya Mjini.

Strategist mzuri kwa nafasi yake kama NS angecheza na Budget officers wa Wizara ya ujenzi na fedha ili waiingize hiyo barabara kwenye mpango kazi wa 2020/21. Kipindi cha kufanya hayo ni miezi ya November- Jan 2021. Alidhani Mwendazake hatakufa, tunamsubiri 2025
 
Tulia siyo strategist. Alitegemea huruma za Mwendazake ndiyo amsaidie kuweka mafungu kama alivyomsaidia kupata ubunge wa Mbeya Mjini.

Strategist mzuri kwa nafasi yake kama NS angecheza na Budget officers wa Wizara ya ujenzi na fedha ili waiingize hiyo barabara kwenye mpango kazi wa 2020/21. Kipindi cha kufanya hayo ni miezi ya November- Jan 2021. Alidhani Mwendazake hatakufa, tunamsubiri 2025
Yaani Tulia hakuusoma mchezo!
 
ukiona hivyo taa ishawaka mbeya labda jimbo jingine litaftwe haraka au achague kujitoa kwenye list yawasomi wanaokalia mawazo yao chanya kisa chama
 
Wabunge wa Mbeya /Songwe wakomalie hii miundo mbinu ya mikoa hii.
Ukitoka pale Igawa kuelekea Mbeya barabra ni mbaya mbaya mno, unaweza hata kupoteza rim ya gari na kuingia korongo(Igawa-Mbeya ni 100km na Mbeya-Tunduma ni ~100km)

Mkapa hakuwahi kukarabati
Kikwete hakuwahi kukarabati.
Mwendazake alikuwa busy na fly over ya Busisi kwenda kwao.

Ni wakati kudai barabara hii na nyingine Mkoani Mbeya /Songwe zijengwe, tumenyanyapaliwa mno.
Afu nimeshangaa kwenye bajeti barabara kuu na za muhimu.kitaifa hazina pesa au zimepewa pesa kiduchu ila kibarabara uchwara cha kwenda Chato sijui nyamirembe port Chato ginery wametenga pesa nyingi

Huu ni upuuzi ,Kazi ya barabara kuu za kuunga mikoa na nchi bado afu huyu Waziri anafanya mambo ya kijinga.

Hicho kibarabara kinaweza kweli kulingana na barabara ya Mbeya Tabora)Singida? Au kama ile ambayo mbunge alitaka kupiga sarakasi?

Mh Rais ikiwezekana punguza pesa kwenye miradi ya reli peleka pesa kwenye barabara ndiko kwenye tija.
 
Wabunge wa Mbeya na Songwe wasipokomaa sasaivi miundombinu ya ule Mkoa ndo inaenda kuwa mfu kabisa. Haiwezekani mikoa inayochangia kwa kiwango kikubwa uchumi wa Taifa hili kutokana na kuwa njia kuu ya mizigo kwenda nchi kama 5 alafu inakuwa na miundombinu mibovu kiasi kile.
Ni kweli mkuu kila parameter ya uchumi huikosi Mbeya ila kwenye allocation ya funds haitendewi inavyostahiki,hizi sio akili ccm waelewe hili
 
Inajengwa kwa awamu wameishia Igawa sasa hv,wanatakiwa kwenda Mbeya then Tunduma border
Ile sio barabara ya kujengwa kwa awamu,ni moja ya barabara nyeti Sana kwa Nchi,unajenga kwa awamu kwani ni ya kwenda Chato kubeba punda?
 
Wabunge wa Mbeya /Songwe wakomalie hii miundo mbinu ya mikoa hii.
Ukitoka pale Igawa kuelekea Mbeya barabra ni mbaya mbaya mno, unaweza hata kupoteza rim ya gari na kuingia korongo(Igawa-Mbeya ni 100km na Mbeya-Tunduma ni ~100km)

Mkapa hakuwahi kukarabati
Kikwete hakuwahi kukarabati.
Mwendazake alikuwa busy na fly over ya Busisi kwenda kwao.

Ni wakati kudai barabara hii na nyingine Mkoani Mbeya /Songwe zijengwe, tumenyanyapaliwa mno.
Uko sahihi nikiwa na Drive kwenda kwetu Makete kupitia Mbeya(Uyole - Isyonje- Igoma- Kitulo) nikivuka Daraja la Igawa tu napunguza speed mpaka 60km/hr. Barabara ni chakavu sana
 
Wabunge wa Mbeya /Songwe wakomalie hii miundo mbinu ya mikoa hii.
Ukitoka pale Igawa kuelekea Mbeya barabra ni mbaya mbaya mno, unaweza hata kupoteza rim ya gari na kuingia korongo(Igawa-Mbeya ni 100km na Mbeya-Tunduma ni ~100km)

Mkapa hakuwahi kukarabati
Kikwete hakuwahi kukarabati.
Mwendazake alikuwa busy na fly over ya Busisi kwenda kwao.

Ni wakati kudai barabara hii na nyingine Mkoani Mbeya /Songwe zijengwe, tumenyanyapaliwa mno.
Mara ya mwisho umepita lini hio njia..?
 
Uko sahihi nikiwa na Drive kwenda kwetu Makete kupitia Mbeya(Uyole - Isyonje- Igoma- Kitulo) nikivuka Daraja la Igawa tu napunguza speed mpaka 60km/hr. Barabara ni chakavu sana
Ile barabara ilipuuzwa kwa makisudi na Mwendazake.
 
Mara ya mwisho umepita lini hio njia..?
Mwezi uliopita!
Igawa-Mbeya ni Mbovu sana,
Mbeya Tunduma ni Mbovu zaidi-pale, Iwambi-Mbalizi barabara ya kimataifa sasa ni one way , one lane!

Halafu tunasema serikali ipo, huku inajenga flyover baharini na Busisi.
 
Back
Top Bottom