Dkt. Slaa: Bunge la Ulaya limetuhukumu Tanzania bila kusikilizwa (2019 Video)

Iwensanto

JF-Expert Member
Mar 7, 2019
1,173
1,092
Habari za asubuhi wakuu,

Nimemsikia Dkt. Slaa akieleza kwa uchungu kuwa Bunge la Ulaya limeiadhibu Tanzania kwa kosa la kuminya Demokrasia.

Na nchi zote za Umoja wa Ulaya hazitafanya biashara na Tanzania kwa kosa hilo, lakini jambo hilo limefanyika huku Bunge hilo likivunja Demokrasia kwa kutokuipa Tanzania nafasi ya kujieleza katika Bunge hilo kama Demokrasia inavyotaka.


Wataalamu wa mambo ya kisiasa na uchumi watueleze, nini athari ya maamuzi haya kwa Tanzania?
 
Hatari namna ya kuepukana na athari hizi
Athari ni kubwa sana. Uchumi wa nchi utadorora sana. Tujitafakari juu ya kukwezwa kuwa nchi ya uchumi wa kati. Huenda tukashushwa kurudi kwenye nchi maskini duniani. Yaliyotokea Zimbabwe sasa yananukia Tanzania.
 
Hasira zao zinawapelekea kuzira kama demu siyo?

Kwamba wanazuia watalii kuja na kutofanya biashara kuja kwetu, Kwani Dunia ina nchi ngapi na ulaya ina nchi ngapi?

Raisi wa ulaya na spika wao ni washamba Sana aisee!!

Hiyo ni adhabu Sawa na mke azire kumpikia Mume na badala yake mume awe anajipikia Wakati naye ni mtaalamu wa kupika
Tutajipikia
 
Okay sawa hakuna misaada tunayopatiwa kutoka nchi hizo
wewe unayesema safi sana,kuna nini unachotumia au kukimiliki kutoka ulaya?
unafurahia ujinga,tanzania haiwezi kuathirika kwa lolote..sisi washirika wetu wanatoka bara Asia zaidi..
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom