Burnaboy
JF-Expert Member
- Dec 2, 2019
- 1,070
- 1,437
Dr W. Slaa kaingia Tanzania jana Jumanne 10/03 usiku. Leo amefanya interview kwenye kipindi cha "Kumepambazuka" cha Radio One.
Amezungumza mengi kama vile diplomasia ya uchumi nk ila kuhusu siasa hizi ni dondoo muhimu kwenye interview hiyo:
1. Alijiuzulu siasa za vyama (active party politics). Hajarudi CCM na hategemei kurudi CCM. Si lazima arudi CCM (awe mwanachama) ili alitumikie taifa lake.Yeye kule Sweden hamuwakilishi mwenyekiti wa CCM, anamuwakilisha Rais.
2. Slaa anasema kama wapinzani walishindwa kuiondoa CCM 2015 hawataweza kuiondoa tena. Chama tawala kimebeba na kutekeleza agenda iliyoipa umaarufu upinzani 2015. Anasema upinzani unajenga mawazo chama tawala kinatekeleza. Hakuna kosa kwa chama tawala kuiba mawazo. Vyama vya upinzani vinapewa ruzuku kuwa "Viwanda vya Mawazo" ambayo chama tawala kinayatumia sababu upinzani hawana mahali (platform) ya kutekeleza mawazo yao.
3. Slaa anasema hakuna waraka (decree) unaowazuia wapinzani kuendesha shughuli zao. Serikali haifanyi kazi kwa matamko. Anasema kilichotokea ni kwamba kuna matamko ya upinzani (Chadema) yalileta sura ya kuchafua utulivu (Civil Disobedience). Walisema wataandamana kila kona - mkoa hadi mkoa, kijiji hadi Kijiji, mtaa hadi mtaa. Anasema kwa tafsiri yake, sheria inayotumika kudhibiti shughuli za wapinzani ni ya kipolisi sababu ikifika mahali unakwamisha mambo hauwezi kuachwa.
Anatoa mfano ofisi yake ya ubalozi Sweden ilipokea taarifa ya "Maandamano ya Mange Kimambi." Mamlaka ya Serikali ya Sweden ilitaka maelezo ya kina (details) za waandamanaji ikiwemo majina yao. Mamlaka hiyo ilielekeza idadi yao, sehemu ya kusimama na masharti mengine kama kutotumia vipaza sauti, nk. Anasema hii ni kuonyesha hata kwenye nchi kama Sweden, masharti yapo ili kuepuka kusumbua wananchi. Kati ya wale 100 walioruhusiwa kuandamana ni 6 tu walijitokeza.
Slaa anasema aliwaasa Chadema wajirekebishe kuhusu hili ila wameshindwa. Anasema ukombozi haupatikani kwa "Red Brigade" kuwa barabarani.
Anawaasa wanaotaka kujua Chadema ilipoanza kukosea wasome kitabu chake cha "Nyuma ya Pazia"
Amezungumza mengi kama vile diplomasia ya uchumi nk ila kuhusu siasa hizi ni dondoo muhimu kwenye interview hiyo:
1. Alijiuzulu siasa za vyama (active party politics). Hajarudi CCM na hategemei kurudi CCM. Si lazima arudi CCM (awe mwanachama) ili alitumikie taifa lake.Yeye kule Sweden hamuwakilishi mwenyekiti wa CCM, anamuwakilisha Rais.
2. Slaa anasema kama wapinzani walishindwa kuiondoa CCM 2015 hawataweza kuiondoa tena. Chama tawala kimebeba na kutekeleza agenda iliyoipa umaarufu upinzani 2015. Anasema upinzani unajenga mawazo chama tawala kinatekeleza. Hakuna kosa kwa chama tawala kuiba mawazo. Vyama vya upinzani vinapewa ruzuku kuwa "Viwanda vya Mawazo" ambayo chama tawala kinayatumia sababu upinzani hawana mahali (platform) ya kutekeleza mawazo yao.
3. Slaa anasema hakuna waraka (decree) unaowazuia wapinzani kuendesha shughuli zao. Serikali haifanyi kazi kwa matamko. Anasema kilichotokea ni kwamba kuna matamko ya upinzani (Chadema) yalileta sura ya kuchafua utulivu (Civil Disobedience). Walisema wataandamana kila kona - mkoa hadi mkoa, kijiji hadi Kijiji, mtaa hadi mtaa. Anasema kwa tafsiri yake, sheria inayotumika kudhibiti shughuli za wapinzani ni ya kipolisi sababu ikifika mahali unakwamisha mambo hauwezi kuachwa.
Anatoa mfano ofisi yake ya ubalozi Sweden ilipokea taarifa ya "Maandamano ya Mange Kimambi." Mamlaka ya Serikali ya Sweden ilitaka maelezo ya kina (details) za waandamanaji ikiwemo majina yao. Mamlaka hiyo ilielekeza idadi yao, sehemu ya kusimama na masharti mengine kama kutotumia vipaza sauti, nk. Anasema hii ni kuonyesha hata kwenye nchi kama Sweden, masharti yapo ili kuepuka kusumbua wananchi. Kati ya wale 100 walioruhusiwa kuandamana ni 6 tu walijitokeza.
Slaa anasema aliwaasa Chadema wajirekebishe kuhusu hili ila wameshindwa. Anasema ukombozi haupatikani kwa "Red Brigade" kuwa barabarani.
Anawaasa wanaotaka kujua Chadema ilipoanza kukosea wasome kitabu chake cha "Nyuma ya Pazia"