Dkt. Shoo ni Mkuu wa KKKT au ni Askofu mkuu wa KKKT? Maana kuna tofauti hapo!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,875
141,809
Kwa mfano Kanisa Katoliki wao Mkuu wa Kanisa ni Papa na kila Dayosisi inajitegemea chini ya askofu wake aliyeteuliwa na Papa.

Ila kuna Rais wa baraza la maaskofu (TEC) yeye hutokana miongoni mwa maaskofu lakini hana nguvu kwenye shughuli za kila Dayosisi.

Anglican wao Askofu mkuu anaingia hadi kwenye shughuli za kila Dayosisi na anaweza kufanya maamuzi hata ya kumsimamisha askofu kama amekiuka taratibu.

Sasa kufuatia mgogoro wa Dayosisi ya Konde nimesikia baadhi ya maaskofu wa KKKT wakimtambulisha Dr Shoo kama Mkuu wa Kanisa na wengine wanamtambulisha kama Askofu mkuu.

Waumini wa Konde wanadai askofu Dr Shoo ndio kiini cha huo mgogoro kwa sababu haelewani na askofu Malasusa wa DMP ambaye kiasili Konde ndiyo nyumbani kwao. Waumini wanadai askofu Dr Shoo hana mamlaka ya kuwaamulia jambo lolote.

Waumini wa KKKT naomba ufafanuzi Tafadhali.

Ni kama katiba ya ACT Wazalendo ni ngumu kujua kazi za Zitto Kabwe na Mzee Haji Duni.

Mungu wa mbinguni awabariki nyote!
 
Hivi kama viongozi wana gombea vyeo kuna utendaji WAKI MUNGU miongoni mwao kweli? ... au ndo ile usihukumu ili usije hukumiwa
 
Kwanza mpatie heshima kwa utaratibu wa kutaja cheo/Wadhifa wake katika mpangilio fasaha.

Baba Askofu Dr Shoo ni Mkuu wa KKKT ambayo zipo baadhi ya Dayosisi zipo Kenya na Congo DRC.
Kwahiyo yeye ni kiongozi mkuu wa Dayosisi na makanisa yote ya KKKT?
 
Kwahiyo askofu mkuu wa Dayosisi ndio anaamua mambo yote katika Dayosisi husika?
Ndiyo!

Na kila dayosisi ina katiba yake! Lakini ktiba ya dayosisi iko chini ya katiba ya KKKT nzima!

Walicho haribu KKKT kwenye muundo ni hii ya kila dayosisi kujiamulia mambo yake!

Mfano Bagonza wa Karagwe kuna siku alisema hii ni dayosisi yetu hakuna wa kutuamlia kitu. Na nyie wa dayosisi ya Dar inayoongozwa na Malasusa bakini na mambo yenu. Hii ilitokana na hao maaskofu kutofautiana kiitikadi za vyama.

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Ndiyo!

Na kila dayosisi ina katiba yake! Lakini ktiba ya dayosisi iko chini ya katiba ya KKKT nzima..
Nimekuelewa.

KKKT maaskofu wenye mrengo wa vyama vya upinzani ndio huletaga sintofahamu.
Hata askofu mstaafu Mdegela alipokuwa Chadema alitaka kuitenga Dayosisi yake!
 
Kwa mfano Kanisa Katoliki wao Mkuu wa Kanisa ni Papa na kila Dayosisi inajitegemea chini ya askofu wake aliyeteuliwa na Papa.

Ila kuna Rais wa baraza la maaskofu (TEC) yeye hutokana miongoni mwa maaskofu lakini hana nguvu kwenye shughuli za kila Dayosisi...
Si kweli kwamba Askofu Shoo haelewani na Askofu Malasusa. Askofu Shoo aliunda kamati ikachunguze huo mgogoro na Askofu Malasusa alikuwa mwemyekiti wa hiyo kamati.

Kama hawaelewani asingekubali awe mwenyekiti. Mgogoro haumhusu Askofu Shoo au Askofu Malasusa. Maaskofu hawa wawili wamijitahidi kusuluhisha huu mgogoro ili kanisa la Mungu lisipasuke.
 
Kwa mfano Kanisa Katoliki wao Mkuu wa Kanisa ni Papa na kila Dayosisi inajitegemea chini ya askofu wake aliyeteuliwa na Papa.

Ila kuna Rais wa baraza la maaskofu (TEC) yeye hutokana miongoni mwa maaskofu lakini hana nguvu kwenye shughuli za kila Dayosisi...
mkuu umenichekesha sana hapo kwenye katiba ya ACT kusema kweli mi sijui kazi ya zito kabwe
 
Si kweli kwamba Askofu Shoo haelewani na Askofu Malasusa. Askofu Shoo aliunda kamati ikachunguze huo mgogoro na Askofu Malasusa alikuwa mwemyekiti wa hiyo kamati. Kama hawaelewani asingekubali awe mwenyekiti. Mgogoro haumhusu Askofu Shoo au Askofu Malasusa. Maaskofu hawa wawili wamijitahidi kusuluhisha huu mgogoro ili kanisa la Mungu lisipasuke.
sasa kwanini wasifunge na kuomba badala yake imekua vita kama ya simba na yanga mtifuano kweli kweli hadi wanaharibu image ya kanisa kkkt inaonekana ya wahuni
 
sasa kwanini wasifunge na kuomba badala yake imekua vita kama ya simba na yanga mtifuano kweli kweli hadi wanaharibu image ya kanisa kkkt inaonekana ya wahuni
Kufunga na kuomba ni sawa lakini lazima maamuzi yafanyike. Mungu hutenda kazi kupitia wanadamu na kikatiba masuala ya KKKT huamuliwa kupitia mkutano mkuu. Mkutano mkuu uliokaa Mbeya ulikuwa wa kikatiba na ndiyo ulioamua maamuzi yaliyotokea. Hawa wengine wahuni tu ndiyo wanatupotosha. Askofu Shoo na tume aliyoiunda hakukosea. Tume ilitoa mapendekezo lakini wahusika hawakutekeleza yale mapendekezo ya kuliponya kanisa. Mungu hawezi kushuka kutoka mbinguni aje kutatua huu mgogoro, lazima utatuliwe na watu. Ndiyo maana Askofu anahangaika kutatua huu mgogoro.
 
Si kweli kwamba Askofu Shoo haelewani na Askofu Malasusa. Askofu Shoo aliunda kamati ikachunguze huo mgogoro na Askofu Malasusa alikuwa mwemyekiti wa hiyo kamati.

Kama hawaelewani asingekubali awe mwenyekiti. Mgogoro haumhusu Askofu Shoo au Askofu Malasusa. Maaskofu hawa wawili wamijitahidi kusuluhisha huu mgogoro ili kanisa la Mungu lisipasuke.
Kwa mujibu wa askofu Mdegela wanaopaswa kusuluhisha ni wazee wa huko zkonde akina Prof Mwandosya na wenzake siyo kamati ya maaskofu.

Mchawi mpe mwanao amlee ndicho alichotaka kufanya Shoo!
 
Wewe Mkatoliki mambo ya Lutheran yanakuhusuje kama sio umbeya tu.
Kwa mfano Kanisa Katoliki wao Mkuu wa Kanisa ni Papa na kila Dayosisi inajitegemea chini ya askofu wake aliyeteuliwa na Papa.

Ila kuna Rais wa baraza la maaskofu (TEC) yeye hutokana miongoni mwa maaskofu lakini hana nguvu kwenye shughuli za kila Dayosisi.

Anglican wao Askofu mkuu anaingia hadi kwenye shughuli za kila Dayosisi na anaweza kufanya maamuzi hata ya kumsimamisha askofu kama amekiuka taratibu.

Sasa kufuatia mgogoro wa Dayosisi ya Konde nimesikia baadhi ya maaskofu wa KKKT wakimtambulisha Dr Shoo kama Mkuu wa Kanisa na wengine wanamtambulisha kama Askofu mkuu.

Waumini wa Konde wanadai askofu Dr Shoo ndio kiini cha huo mgogoro kwa sababu haelewani na askofu Malasusa wa DMP ambaye kiasili Konde ndiyo nyumbani kwao. Waumini wanadai askofu Dr Shoo hana mamlaka ya kuwaamulia jambo lolote.

Waumini wa KKKT naomba ufafanuzi Tafadhali.

Ni kama katiba ya ACT Wazalendo ni ngumu kujua kazi za Zitto Kabwe na Mzee Haji Duni.

Mungu wa mbinguni awabariki nyote!
 
Kuleta migogoro ya makanisa mitandaoni au sehemu nyingine nje ya kanisa ni ujinga, ujuha na uwezo duni wa kufikiri. Kama kanisa ulilopo lina migogoro kwa nini msimalize wenyewe huko ndani ya kanisa washiriki na viongozi wenu husika ? Kama imeshindikana kabisa kufikia muafaka kwa nini msiachane na hilo kanisa mkaenda madhehebu mengine, kama hilo nalo ni gumu pia kwa nini msianzishe kanisa lenu wenyewe?

Tanzania ina uhuru mkubwa wa kiimani, mtu unaweza kuhamia dhehebu lingine au dini nyingine kabisa wakati wowote bila kikwazo. Pia Tanzania ni sehemu rahisi sana kuanzisha kanisa lako tofauti na nchi kama Rwanda, kama mnaona mnashindwana na wenzenu anzisheni kanisa lenu msiparuane na kulazimisha upande wenu mnaoona ni sahihi kwenu.
 
Back
Top Bottom