MTAZAMO
JF-Expert Member
- Feb 8, 2011
- 19,640
- 33,421
Wakuu,
Naona mjadala mzuri sana TBC kuhusu chanjo za UVIKO. Lakini hoja yangu ni moja tu, kwanini mijadala yao wanaalika tu wenye mitazamo chanya na chanjo? Kwanini wapinga chanjo maarufu kama Askofu Gwajima na Mh Polepole wasialikwe?
Si mjadala? Mbona mngekata mzizi wa fitna kirahisi tu? Waletwe wapinga chanjo na wataalam wao na wasiopinga tuwasikilize.
Mpaka sasa wapinga chanjo hakuna chombo cha habari kilichowahoji na wanapotumia platform zao kupinga wanaonekana wahaini hasa kwa waliochanja. Kwanini kusiwe na mijadala huru tu?
Kama kuchanja au kutochanja ni hiari kwanini haturuhusu mijadala huru? Wanahabari mnaogopa nini kutoa fursa kwa wapinga chanjo pia ili sisi kalaghabao tuamue kama wakati wa uchaguzi? Mbona hao "makanjanja" mngewazima kirahisi kwa hoja zenu makini?
Naona mjadala mzuri sana TBC kuhusu chanjo za UVIKO. Lakini hoja yangu ni moja tu, kwanini mijadala yao wanaalika tu wenye mitazamo chanya na chanjo? Kwanini wapinga chanjo maarufu kama Askofu Gwajima na Mh Polepole wasialikwe?
Si mjadala? Mbona mngekata mzizi wa fitna kirahisi tu? Waletwe wapinga chanjo na wataalam wao na wasiopinga tuwasikilize.
Mpaka sasa wapinga chanjo hakuna chombo cha habari kilichowahoji na wanapotumia platform zao kupinga wanaonekana wahaini hasa kwa waliochanja. Kwanini kusiwe na mijadala huru tu?
Kama kuchanja au kutochanja ni hiari kwanini haturuhusu mijadala huru? Wanahabari mnaogopa nini kutoa fursa kwa wapinga chanjo pia ili sisi kalaghabao tuamue kama wakati wa uchaguzi? Mbona hao "makanjanja" mngewazima kirahisi kwa hoja zenu makini?